Siku 365 hazitoshi kukupatia Mafanikio ya kweli katika Maisha

Keagan Paul

JF-Expert Member
Jul 19, 2018
500
3,057
Wakuu Nisiwachoshe sana

Nazungumzia mafanikio ya kweli katika maisha, sio mafanikio ya janja janja. Mafanikio ya janja janja ni kwamba leo una pesa nyingi, magari ya kifahari halafu baada ya miezi/miaka kadhaa unarudi tena kwenye maisha ya kuungaunga\kukosa pesa.

Ndugu zangu kama unataka kuwekeza kwenye jambo lolote ambalo litakukwamua kuondokana kwenye umaskini wa kudumu basi wekeza kwenye Miradi ya muda mrefu. Pengine wekeza kwenye miradi ya zaidi ya miaka 3 na zaidi. Hapo ukifanikiwa unakuwa umefanikiwa mazima. Ndani ya hiyo miaka 3 na zaid unakuwa ulishajifunza hasara na faida za huo mradi.

Wengi wetu tunapenda kupata faida za haraka hivyo hupelekea kufanya miradi ya kutupatia pesa za haraka. Kufanya miradi ambayo tutapata return ndani ya muda mfupi, lakini unatasahau kwamba uwezekano kwa kurudi nyuma ni wa muda mfupi hivyo hivyo.

Anza biashara yako polepole bila kuitegemea hiyo biashara yako muda wa miaka 3 na zaid lazima utaona mafanikio, lazima mtaji utakua.

Mfano: Nenda kanunue Hisa, Nenda kapande miti mingi ya mbao huko Njombe, Iringa, miti ya matunda huko Tanga, Lushoto. Ndani ya miaka 5 mpaka 7 unakuwa umepiga hatua kubwa kimaisha.

Nenda pole pole siku 365 pekee hazitoshi kukupatia mafanikio ya kudumu. Endelea kukuza mtaji wako. Usitumie hata senti 1 kutoka kwenye biashara yako changa ulioianzisha mpaka baada ya miaka 3 na zaidi lazima utatoboa. Hakuna mafanikio ya kweli chini ya siku 365.

Hata unayemuoa leo amefanikiwa kupitia Bar, aliwekeza kwenye hiyo Bar kwa zaidi ya siku 365, ndo leo wewe na mimi tunaona amefanikiwa sana. Kwa mtu wa kawaida kama mimi na wewe, hata ujenge nyumba ili iwe nzuri kwa kiwango fulani ni lazima ujenzi huo utazidi simu 365, sasa kwa nini unadhani unaweza kufanikiwa kwenye maisha kwa chini ya siku 365?

Pambana bila kukata tamaa, usitumie kwenye mambo yako binafsi huo mtaji wako mdogo kama bado kujatoboa siku 365, achana na mambo ya kusaidia ndugu ovyo kama kweli unataka kufanikiwa. Utawasaidia mbele ya safari.
 
Mfano ukakalima mwaka mmoja kilimo cha mazao ya mda wa miezi mitatu maxmum huwezi toboa chini ya siku 365?
 
Wacha tuendelee tu kujifariji. Mwingine ananiambia mafanikio sio kupata mahela ila kutimiza ndoto zako.
Wakuu Nisiwachoshe sana

Nazungumzia mafanikio ya kweli katika maisha, sio mafanikio ya janja janja. Mafanikio ya janja janja ni kwamba leo una pesa nyingi, magari ya kifahari halafu baada ya miezi/miaka kadhaa unarudi tena kwenye maisha ya kuungaunga\kukosa pesa.

Ndugu zangu kama unataka kuwekeza kwenye jambo lolote ambalo litakukwamua kuondokana kwenye umaskini wa kudumu basi wekeza kwenye Miradi ya muda mrefu. Pengine wekeza kwenye miradi ya zaidi ya miaka 3 na zaidi. Hapo ukifanikiwa unakuwa umefanikiwa mazima. Ndani ya hiyo miaka 3 na zaid unakuwa ulishajifunza hasara na faida za huo mradi.

Wengi wetu tunapenda kupata faida za haraka hivyo hupelekea kufanya miradi ya kutupatia pesa za haraka. Kufanya miradi ambayo tutapata return ndani ya muda mfupi, lakini unatasahau kwamba uwezekano kwa kurudi nyuma ni wa muda mfupi hivyo hivyo.

Anza biashara yako polepole bila kuitegemea hiyo biashara yako muda wa miaka 3 na zaid lazima utaona mafanikio, lazima mtaji utakua.

Mfano: Nenda kanunue Hisa, Nenda kapande miti mingi ya mbao huko Njombe, Iringa, miti ya matunda huko Tanga, Lushoto. Ndani ya miaka 5 mpaka 7 unakuwa umepiga hatua kubwa kimaisha.

Nenda pole pole siku 365 pekee hazitoshi kukupatia mafanikio ya kudumu. Endelea kukuza mtaji wako. Usitumie hata senti 1 kutoka kwenye biashara yako changa ulioianzisha mpaka baada ya miaka 3 na zaidi lazima utatoboa. Hakuna mafanikio ya kweli chini ya siku 365.

Hata unayemuoa leo amefanikiwa kupitia Bar, aliwekeza kwenye hiyo Bar kwa zaidi ya siku 365, ndo leo wewe na mimi tunaona amefanikiwa sana. Kwa mtu wa kawaida kama mimi na wewe, hata ujenge nyumba ili iwe nzuri kwa kiwango fulani ni lazima ujenzi huo utazidi simu 365, sasa kwa nini unadhani unaweza kufanikiwa kwenye maisha kwa chini ya siku 365?

Pambana bila kukata tamaa, usitumie kwenye mambo yako binafsi huo mtaji wako mdogo kama bado kujatoboa siku 365, achana na mambo ya kusaidia ndugu ovyo kama kweli unataka kufanikiwa. Utawasaidia mbele ya safari.
 
Mfano ukakalima mwaka mmoja kilimo cha mazao ya mda wa miezi mitatu maxmum huwezi toboa chini ya siku 365?
Labda ukalime pareto,ufuta au vanilla...
Sio umelima mahindi yako ya gobo halafu utuambie umetoboa
 
Ukitaka mafanikio ya haraka lima mpunga, ukitaka ya muda wa kati panda miti ya mbao na ya muda mrefu msomeshe mtoto ~ unknown
 
Mafanikio n Juhudi zako na kujiongeza pia Mungu, Imani, mipango imara na kuamini...
Mwezi wa Saba mwaka huu nilianza kazi na dada mmoja kwenye kampuni x Mimi nikiwa Kama kiongozi wake baadae Yule dada kazinguana na wakubwa akaacha kazi.
Juzi ananitafuta kapata kazi mshahara ni Mara tano zaidi ya pale aliponiacha....
Ni chini ya siku 365 kila kitu kimebadilika sahivi kwenda south Africa kufanya shopping kwake sio story kabisa...
 
Back
Top Bottom