Eeeeh bwana eeeh umenikumbusha mbali sana - Unajua Nembe hazipo tena?. zimebakia ngere (gogogo) tu unajua tena zimekaa kama papa sangara hawezi kuwameza.
Ni hivi mkuu, wee mkulima ukivuna mazao yako sii unayapeleka sokoni? na huko sokoni unategemea nani atakuwa mteja wako kama sii mfanyakazi? Na sisi wavuvi tunawapeleka vijana wetu shule ili wapate mtaji wa maisha nasi tupate kuuza kesho samaki wetu kwa wasomi hawa bei juu tukikuza soko la ndani.
Aliyeko Dar akija likizo atuletee mtaji wa kuongeza mitumbwi na nyavu, maisha yanaendelea hatuhitaji msaada wa mzungu kutupa misaada yenye masharti. Na laukama hatukuwapeleka watoto wetu shule wangebakia kuvua samaki na kijiji kizima sote tungekuwa wavuvi sijui wangemuuzia nani hizo samaki...
Sasa ile hasira ya kulea, mifeza ulopoteza kumpeleka shule halafu haleti ngawila nyumbani, haya samaki nao wanaoza sokoni hawa wasomi wakidai bei juu ndio inatakiwa kukusukuma wewe kuingia barabarani na mabango...
Bado tu Wasu?