Sijutii kukataa kupewa nyumba nzuri na baba mkwe, nina amani sana na familia yangu kwenye nyumba ya kawaida niliyopanga

Sijutii kukataa kupewa nyumba nzuri na baba mkwe, nina amani sana na familia yangu kwenye nyumba ya kawaida niliyopanga

mkata uzi

JF-Expert Member
Joined
Aug 3, 2025
Posts
1,910
Reaction score
5,450
Wakati wa kufunga ndoa, baba mkwe alipendekeza kutupatia nyumba yake, Ilikuwa ni nyumba ya kisasa, ikiwa na baadhi ya samani tayari.

Baada ya kutafakari kwa kina, niliamua kukataa pendekezo hilo. Badala yake nilirudi na mke wangu kwenye nyumba ndogo ya kupanga. Ingawa ilikuwa ndogo, amani ya moyo niliyokuwa nikiipata ilikuwa ya thamani kubwa sana.

Hata baada ya familia yetu kuongezeka, niliendelea kushawishiwa kuhamia kwenye ile nyumba kubwa, lakini niliendelea kusimamia uamuzi wangu.

Nilijibana, nikapangisha nyumba kubwa zaidi kulingana na uwezo wangu, ambayo tunaishi hadi sasa, huku nikiendelea na ujenzi unaokaribia kukamilika.

Uamuzi wangu ulitokana na misingi kadhaa.

sikutaka kuingia katika hali ya kujiona mnyonge au kuhisi kuwa nalazimika kuishi kwa neema ya familia ya mke wangu.

nilielewa kuwa msaada wa aina hiyo unaweza kugeuka fedheha, nikimaanisha uwezekano wa kuja kutupiwa mabegi nje na kufukuzwa kwenye nyuma ambayo sio yako, hii inatokeaga mkipishana kauli na mke wako akirudi kwao unatishwa kufukuzwa au baba mkwe akifariki na watoto wake hawakuupenda uamuzi wake wa kukupa nyumba, watakufukuza kwa kukudhalilisha.

Zaidi ya hayo, nilitambua kuwa msaada unaweza kubadilika na kuwa chombo cha kukumbushia au kudai shukrani kupita kiasi, kiasi cha kudhoofisha heshima na uhuru wangu. utaanza kuambiwa wazi wazi kuwa shukrani ya punda ni mateke, ulipewa nyumba bure kwanini wewe husaidii, n.k.

Pia, hata masuala ya umiliki kama hati ya nyumba yangeweza kuwa chanzo cha migogoro, familia ya mke wangehisi hofu juu yangu kutaka kuuza nyumba yao.

Sikutaka kumpa nafasi hata siku moja mke wangu apate kiburi kuwa ninaishi kwao. Nilijua wazi kwamba siku moja tungeweza kugombana, na angeanza kusema "mwaname gani wewe unakaa nyumba ya baba mkwe", “niache kwanza hapa ni kwetu” Au pengine siku nikichelewa kurudi, wangeweza kumwambia anifungie nje kwa sababu hiyo ni nyumba yao.

Kwa ujumla, nilijifunza kuwa amani ya moyo, uhuru wa maamuzi, na kujitegemea ni misingi muhimu sana katika kujenga maisha ya familia yenye heshima na utulivu.
 
Umejiumiza bure tu ungekaa kwenye hiyo nyumba then hela uliyotumia kujengea kwa mateso na damu ungeizungushia kwenye biashara leo ungekuwa tajiri mkubwa tu na ungeweza kujenga nyumba 2, baba mkwe ungemrudishia nyumba yake kwa furaha na vigelegele tena ungemwambia nyumba yake imezaa nyumba 2 na 1 umepangisha.
 
Mimi nililazimishwa tukakae ukweni kisa mama mtu alikuwa mgonjwa mgonjwa kwa lengo kwamba wife awe anamuhudumia kwa ukaribu. Wife naye alikuwa kashadadia tukakae tu kwani itatupunguzia ugumu wamaisha.

Nilichowaambia ni kwamba nimeoa kwa lengo la kujiongezea ugumu wa maisha sio kurahisisha maisha. Mama mkwe aliniona Nina roho mbaya sana.
 
baba mkwe ungemrudishia nyumba yake kwa furaha na vigelegele tena ungemwambia nyumba yake imezaa nyumba 2 na 1 umepangisha.
Hiki ndicho alichokataa.
Maisha yake yote angehisi mnyonge anapaswa kushukuru kubebwa na mkwewe.
Kwa lugha nyingine kubebwa na mkewe.
Ipo siku angekuja kuambiwa yeye bila baba mkwe wake hasingweza kujenga angekufa masikini nyumba ya kupanga.
 
Hongera,jirani hapa mara atupiwe nguo nje,mara akapange,ndugu zake wakija wanasimangwa na kufukuzwa,,huyu mwanaume ni nes sijui Dr lkn Hana ajira anajishikiza kwenye vihospital,mwanamke nae Hana ajira now kafunguliwa ofisi ya muamala na baba yake ,mwanamke kwao pesa zipo na wapo watoto wawili TU, huyu mwanaume ni manyanyaso tupu🙌

Alifukuzwa karudi tena,anasema anarudi kwaajili ya watoto. Anafokewa kama mtoto daah,inasikitisha.
 
Kipindi naoa, baba mkwe alitaka kutupa nyumba yake bure kabisa, ni nyumba ya kisasa na kulikuwa na baadhi ya vitu kama samani.

Jambo hilo nilikataa kabisa, nilirudi na wife kajumba kadogo nilikopangisha lakini amani niliyokuwa nikiipata ni kubwa sana.

Bado waliendelea kuniomba nihamie nyumba kubwa lakini niliwatolea nje hadi wakachoka.

Baada ya familia kuwa kubwa tukahamia nyumba kubwa kidogo ambayo tupo hadi sasa huku ujenzi ukiendelea ambao unaelekea kumalizika.

Peace of mind ni kitu muhimu san
Mshukuru mke wako! Ni wife material na anakupenda kwa dhati
 
Back
Top Bottom