Kwanini vijana wengi wanalilia kuajiriwa? Hivi huna jamaa vijijini ukaenda kule kununua japo kuku,mbuzi kwa mkopo halafu ukaleta mjini na kuuza. Ukarejesha hela yao na faida ukaanza kuizungushia. Au nenda kijijini kwa mwaka halafu wakati wa mavuno chukuwa asilimia flani ya mazao kwa njia ya mkopo. Ukishauza rejesha hela yao na bakia na faida rudi tena kijijini nunua bidhaa zitakazo leta faida mjini. Kuna njia za kujinyayua kimaisha huhitaji hata jero, yaani vijana wengi wana akili kama rafiki yangu. Ana hiyari abaki kitaa lakini anataka apate kazi ya ofisini na mpaka leo mwaka wa 3 hana lolote.
Ndukiiiii

♂️

♂️

♂️