Jamani mimi hata mwanamke awe mzuri namna gani, kama anachonga/ananyoa/anapunguza nyusi lazima anishinde. Sipendi kuona nyusi za mwanamke zimechongwa.
Yaani niko tayari kumvumilia mwanamke mchafu, mvaa mawigi, muweka mikope ili mradi tu hachongi nyusi. Siku hizi najitahidi sana ninapozungumza na mwanamke simkazii fikra kwenye nyusi ili nisikereke na nisimkere na yeye. Nikitizama nyusi tu nikaona zimekatwa katwa/zimepunguzwa/zimechongwa basi naahindwa hata kuendelea kuongea nae.
Baadhi yao (majirani) washanishtukia maana nikiongea nao siwatazami usoni. Hapo naondoka na "jioni nikiwa free ntakutafuta"
Niliwahi kumpenda mwanamke kwa sababu moja tu: HAPENDI KUCHONGA NYUSI ZAKE, na nilidumu nae sana, nikataka nifunge nae ndoa ila tu alikuwa wa imani na mtazamo tofauti ikashindikana.
Hata hivyo, yawezekana ni mimi tu ila kuna wanaume wenzangu wanapenda mwanamke akate kate nyusi au hawajali kabisa kuhusu hilo ila binafsi nimeshindwa kupuuzia. Namwambiaga mke wangu ajae (japo sijamjua), "ukichonga nyusi tutashindwa kutazamana usoni kabisaaa".
Sorry kwa ambao nimewakera ila ni mtazamo tu.
Kuna wale ndugu zangu watakaohisi labda nikikua nitabadilika, Kwa sasa nipo kwenye early 30, nimeshakuwa na nnazeeka sasa hivi ila hii tabia bado nnayo toka niko 19.
Yaani niko tayari kumvumilia mwanamke mchafu, mvaa mawigi, muweka mikope ili mradi tu hachongi nyusi. Siku hizi najitahidi sana ninapozungumza na mwanamke simkazii fikra kwenye nyusi ili nisikereke na nisimkere na yeye. Nikitizama nyusi tu nikaona zimekatwa katwa/zimepunguzwa/zimechongwa basi naahindwa hata kuendelea kuongea nae.
Baadhi yao (majirani) washanishtukia maana nikiongea nao siwatazami usoni. Hapo naondoka na "jioni nikiwa free ntakutafuta"
Niliwahi kumpenda mwanamke kwa sababu moja tu: HAPENDI KUCHONGA NYUSI ZAKE, na nilidumu nae sana, nikataka nifunge nae ndoa ila tu alikuwa wa imani na mtazamo tofauti ikashindikana.
Hata hivyo, yawezekana ni mimi tu ila kuna wanaume wenzangu wanapenda mwanamke akate kate nyusi au hawajali kabisa kuhusu hilo ila binafsi nimeshindwa kupuuzia. Namwambiaga mke wangu ajae (japo sijamjua), "ukichonga nyusi tutashindwa kutazamana usoni kabisaaa".
Sorry kwa ambao nimewakera ila ni mtazamo tu.
Kuna wale ndugu zangu watakaohisi labda nikikua nitabadilika, Kwa sasa nipo kwenye early 30, nimeshakuwa na nnazeeka sasa hivi ila hii tabia bado nnayo toka niko 19.

