Hakuna haja y kwenda,kawaida yy ndio anatakiwa aende nyumbani kumuona mtoto. Hiyo ya kumpelekea mtoto ni dharau kubwa na ndio itakuwa sbb ya kukusimangia kwamba ndio maana ulijileta.
Huwezi kumkwepa maisha yako yote, ni mzazi mwenzako. Kama mama alivyosema, aje nyumbani ili ajibu hayo maswali. Kwa nini alikutelekeza? Kwa nini hakutaka kuja kumuona mtoto wake? Na kwa nini Leo aone ndio wakati wa wewe kuonana nae?
Nina wasiwasi jamaa anataka kuosha dushe hana lolote...!