Sijui kwanini namchukia binamu yangu

ofisa

JF-Expert Member
May 15, 2011
4,137
3,763
Habari zenu,

Nina mdogo wangu (binamu) namchukia toka kipindi ambacho nipo ndani ya ndoa sababu ni hivi;

Nilioa mke na yeye (dada yangu) aliolewa na mtu tajiri na kila mara akawa anamtambia mke wangu na mawifi wengine kwenye vitu mbali mbali vya kununua nunua simu, kubadili gari, swiming pool ya kununua na mambo kedekede kila kukicha mke wangu akawa ananiendesha ile mbaya kwamba mimi simpendi, sijui ku care, mara hivi mara vile mwishowe ''demand'' ya vitu na vijimigorogoro vikawa vingi na mimi sijaishi kwenye maisha ya kutatua ,kusuluhisha, kushtakiwa, kulaumiwa, au kulaumu, kusingiziwa mabaya au kutenda mabaya katika ujana wangu wote tuliachana na mke wangu.

Shida niliyonayo yule dada yangu kila leo anapost vitu vizuri vizuri kwenye group moja la whatsaap la familia na mimi nakumbuka vile vijigogoro vilivyopita na aliyekuwa mke wangu.

Sasa sijui tabia yangu ya kumchukia kwa tabia yake hii mimi itaniisha lini maana dogo anakimbiza mpaka mawifi zake wengi kinawauma.
 
Hapana sina roho mbaya ukweli namuonea huruma na yeye hajitambui,ndoa nyingi hufa kutokana na too much over demanding na ni ukweli ndoa za hivi karibuni hazidumu sababu ya over demanding za wake.
 
Pambana nawe uwe na uwezo wa kununua vitu vyako, kumchukia haitasaidia kitu.
 
TATIZO KUMBU KUMBU YA YALE MAISHA YA NDOA NI KAMA ANATONESHA
 
HI,
HABARI ZENU,NINA MDOGO WANGU(BINAMU) namchukia toka kipindi ambacho nipo ndani ya ndoa sababu ni hivi,
Nilioa mke, na yeye(dada yangu) aliolewa na mtu tajiri na kila mara akawa anamtambia mke wangu ,na mawifi wengine kwenye vitu mbali mbali vya kununua nunua (simu,kubadili gari,swiming pool ya kununua, na mambo kedekede kila kukicha) mke wangu akawa ananiendesha ile mbaya kwamba mimi simpendi /sijui ku care,mara hv mara vile mwishowe demand ya vitu na vijimigorogoro vikawa vingi na mimi sijaishi kwenye maisha ya kutatua /kusuruhisha/kushtakiwa /kulaumiwa/au kulaumu/kusingiziwa mabaya/au kutenda mabaya katika ujana wangu wote tuliachana na mke wangu,
shida nliyonayo yule dada angu kila leo anapost vitu vizuri vizuri kwenye group moja la whatsaap la familia na mimi nakumbuka vile vijigogoro vilivyopita na aliyekuwa mke wangu. sasa sijui yangu ya kumchukia kwa tabia yake hii mimi itaniisha lini maana dogo anakimbiza mpaka mawifi zake wengi kinawauma.

Shukuru sana hiyo ndoa imevunjika, hapo hukuoa mke!! Mke mwema hababaishwi na vipitavyo bali angejenga juhudi katika kukupa wewe ari ya kusaka shilingi na yeye angejumuika nawe ili kuhakikisha mnakuwa na vyenu vya halali!!

Dada yako nae ni kwamba halmashauri ya kichwa chake ni dhaifu, anawatambia ili iweje sasa??
 
UKIPATA MWANAMKE USIKAE NAYE KARIBU NA NDUGUZO,ISHI NAYE MBALI NA FAMILIA YAKO YENYE KUHARIBU NDOA KAMA HIVYO
 
Hivi kuna swimming pool kubwa ya kununua,tofauti na zile ndogo za kujaza upepo kija unajaza maji
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom