Siibiwi kweli?

Siibiwi kweli?

kiipwi

Member
Joined
Apr 30, 2013
Posts
66
Reaction score
22
Hallow wana MMU, nahitaji msaada kwa hili linalonitokea kwa sasa.
Kuna binti niko nae kwenye mahusiano huu ni mwaka wa saba sasa, kwakweli nampenda sana na yeye analijua hilo, tatizo lililopo sasa ni kwamba kwa miaka ya hivi karibuni amekua akibadilikabadilika sana yaani simuelewi.

Mwaka jana ilianza kujitokeza hali hii ambapo alipunguza mawasiliano na mimi, ikawa kila nikimsihi tuonane ananipiga chenga. Siku moja alikuja kwangu na akaniomba msamaha akakiri kuwa alikuwa na mahusiano na mtu mwingine.

Nilihuzunika sana, lakini kwasababu nampenda, nikamsamehe.

Tokea mwezi wa nne mwaka huu, hatujaonana wala kukaa pamoja kuzungumza pamoja na jitihada zangu zote za kumsihi tuonane.

Naomba nieleweke, sio kwamba anakataa moja kwa moja, anakubali lakini siku ikifika hatokei na pengine simu asipokee.

Kwasababu nampenda najua kuwa atakuwa amechoka maana anafanya kazi mpaka jumamosi.

Siku moja nikakuta comment ya kajamaa kwenye picha moja aliyoipost Instagram ikanipa shaka kidogo ikanibidi nitake kumfahamu huyo mtu. Huko ndiko nikakutana na picha aliyopiga na mpenzi wangu na comments za kutosha as if ni wapenzi.

Nikamtumia hiyo Picha whatsapp alishtuka, akaanza kuniuliza hiyo picha nilikoitoa, baada ya muda akanipigia simu na kunielezea kuwa nisishtuke kwa hiyo Picha, walipiga tu na huyo mtu kwasababu wanafanya kazi pamoja lakini hamna chochote kinachoendelea kati yao, nikakubali nikamuomba tuonane weekend iliyofuata, hakutokea.

Na mimi nikaacha kumuomba kuonana nae tena. Alhamisi ya wiki iliyopita akanipigia simu akaniahidi angekuja kwangu jumamosi iliyopita, hakuja wala kunitaarifu.

Jana jumapili nikiwa kwenye mishe zangu akanipigia simu akataka aje lakini mimi nikamueleza kuwa sipo nyumbani ila baada ya saa moja hivi nitakuwa nimerudi tayari, akanikubalia.

Baada ya kurudi nikampigia simu hapokei, nikatuma na sms hajajibu mpaka Leo.

Ndugu zangu hivi huyu binti anadhamira ya kweli au kuna kamchezo hapa kanaendelea mimi sina habari, naombeni ushauri.
 
Sijamaliza kusoma ulichoandika maana ni ujinga mtupu huwezi kuwa na uchumba Sugu miaka 7 hujaoa halafu baadaye upate dogodogo ndio unaoa na kumpiga chini mtoto wa watu na kuja JF kuanza kuwaponda wanawake 30+ ambao hawajaolewa.

Kama ningekuwa na uwezo wa kumuona huyo mwanamke ningemshauri akupige chini na namba yako ya simu aiblock na Facebook aku-unfriend.
Huu ni ukatili dhidi ya wanawake, seven years?
 
Nilipofika kipengele hicho nimeacha kuendelea kusoma maana ni total nonsense.


Inawezekana huyu mtu ameweka chumvi kutuonesha kuwa anaweza kudumu kwenye uchumba kwa muda wote huo.
 
Miaka saba?
Unamtakia nini mtoto wa mwanamke mwenzetu?
 
Kimsingi ni kwamba ushapigwa kidochi au umewekwa kama spare tyre...
 
Huyu binti alikua anakupenda sana lakini ulitumia kigezo hicho kumnyanyasa na ukumbuke alishakudharau ndo maana anajitahidi kulipa kisasi kwa kutokupokea sim zako na tatizo wewe ulipata dogo dogo ukamtupa pembeni, miaka saba? Mlikua mnasomea udaktari wa mifugo au uchumba wa kawaida?
 
duh miaka saba kwa hiyo ulitaka uendelee kutumia papuchi bure??? naamini amechukua ustaarabu .. [picha umeziona bado unamfuata fuata hadi akutamkie???
 
kwanza nieleweshe hiyo sentensi hapo,mnauhusiano kwa miaka saba au miezi saba?kama ni miaka saba ni uhusiano wa aina gani huo?uchumba babu kubwa au nini?vyovyote viwavyo huyo binti amesha kuchoka na tayari ana mwingine ,na ni tapeli au msanii achana naye na uendelee na maisha yako.
 
Jitahidi umwone padre au mchungaji aliyewafungisha ndoa yenu amasuluhishe watoto wenu wasijepata taabu mkiachana.
 
Mnajua hiyo miaka saba imefikaje?
Nilianza nae akiwa kidato cha pili, akamaliza kidato cha nne hakufaulu, nikamshauri arudie, akarudia mtihani lakini pia hakupata credit, nikamshauri akasomee clearing and forwarding miaka miwili, jumla mingapi hapo? 6.(Sita)
Mwaka uliopita amepata kazi, nikamwambia anipeleke kwao nikajitambulishe, nimepigwa chenga, mwaka huu mara ya mwisho kuonana nikamueleza nia yangu kwamba mwakani Mungu akipenda tungefunga ndoa, yaani utafikiri ndio nilimuambia kwaheri.
Hiyo ndio miaka Saba sasa. Kuna lingine?
 
Naona siku hizi kuna jubilei za uchumba. Hata mimi angetokea mtu wa kueleweka ningemuacha tu, 7 years eeeh???

Siku hizi "mapagani" wanafanya uzinzi na ukahaba wakisingizia uchumba miaka 7 unamzini mwanamke unaita uchumba.
 
Back
Top Bottom