Sielewi sababu za Mbeya kuwa jiji

Sielewi sababu za Mbeya kuwa jiji

Itakuwa milioni 7...Sugu tu amepigiwa kura za ubunge million 2+ Most voted MP
Huyo jamaa aliesema watu karibia laki 7 anaota yaani watu laki 7 upewe jiji wakati hao watu hata wilaya moja ya mbeya inahao watu angesema mbeya inawatu ml 5 hadi 6 nmgemuelewa maana naskia dar ndo jiji linaloongoza kwa idada kubwa ya watu na inayofuata ni hiyo mbeya kisha mwanza sasa kama inafuata kuifikia dar kwa idadi ya watu iweje ile laki 7 tu!?? Dar ina watu karibia mil 7 maana yake wikaya 1 ya jiji la dar inawatu mil 1 na ushehe
 
Hata mm ni mwenyeji wa mbeya ukijaji kwa huduma za kijamii na miundombinu na madhari kweli mbeya haistahili kuwa kijij hata kidogo ila kwa Kigezo cha watu basi wanastahili
Well said
 
moja ya sifa ya mkoa kupewa hadhi ya JIJI ni makusanyo ya mapato na uzalishaji

nahisi nitakuwa nimekusaidia mleta uzi ni kwann mbeya ilipewa hadhi ya jiji..

kilichobaki fanya homework yako ya mikoa inayoongoza kukusanya mapato hapa tz na ukishaiona Mbeya ipo nafasi ya ngapi nahisi utarejea maelezo yangu ya juu kabisa pale
nautakuwa umepeta jibu lako


hii chini ni ripoti ya BOT ya mwaka 2013

Kwa mujibu wa ripoti ya Benki kuu ya Tanzania(BOT),Dsm ndio mkoa unaoongoza kwa kuchangia pato la taifa.

1. Dar-es-salaam(GDP-7.5 trilion)
2. Mwanza(GDP-4.09 trilion)
3. Mbeya(GDP-3.2 trilion)
4. Shinyanga
5. Iringa
6. Morogoro
7. Arusha(GDP-2.1 triliom)
8. Tanga(GDP-2.09 trillion)
9. Kilimanjaro(GDP-2.03 trillion)


na hayo ndiyo majiji matano kwa hiyo hadi hapo umeshajua hadhi ya jiji inatona na nini
 
Kama kichwa cha mada kinavyojieleza,

Mimi ni mwenyeji wa Mbeya mjini, kwa muda mrefu lakini mi ukweli sioni sababu za msingi za kuipatia Mbeya hadhi ya jiji yaani mji upoupo tu labda wajuvi mnieleze kama kuna sababu za kufanya Mbeya kuwa jiji.

Nawasilisha.
nenda TANUSEMI waulizee sababu nini
 
Kama kichwa cha mada kinavyojieleza,

Mimi ni mwenyeji wa Mbeya mjini, kwa muda mrefu lakini mi ukweli sioni sababu za msingi za kuipatia Mbeya hadhi ya jiji yaani mji upoupo tu labda wajuvi mnieleze kama kuna sababu za kufanya Mbeya kuwa jiji.

Nawasilisha.
Bro ingia TAMISEMI utaona vigezo vya majiji...
Kama utaona hakipo sawa utarudi hapa
 
Sasa ww mtoa mada hii ulitaka Mby iwe wilaya au ubaki kuitwa mkoa? Maana hujaainisha kasoro ulizoziona za mko wa Mby kupewa hadhi ya kuitwa jiji! Weka wazi ili usaidiwe!
 
Kwahiyo mleta mada unasema walikosea kuipa mbeya hadhi ya jiji?

Unaposema huelewi sababu, maana yake vigezo vya mkoa kuitwa jiji unavijua. Ni vyema ungevitaja ili tufananishe na mbeya kama vipo au havipo
 
Tuwe wakweli Tanzania jiji ni moja tu Dar. Mwanza na Arusha ndo zinakuja kwa mbaali kidogo.Hizo nyingine zilipewa hadhi ya jiji kwa sababu wanazijua wao tu.
Hata mm ni mwenyeji wa mbeya ukijaji kwa huduma za kijamii na miundombinu na madhari kweli mbeya haistahili kuwa kijij hata kidogo ila kwa Kigezo cha watu basi wanastahili
Miundombinu gani ya kijamii na kiuchumi ambayo ww umeona haipo
 
Huyo jamaa aliesema watu karibia laki 7 anaota yaani watu laki 7 upewe jiji wakati hao watu hata wilaya moja ya mbeya inahao watu angesema mbeya inawatu ml 5 hadi 6 nmgemuelewa maana naskia dar ndo jiji linaloongoza kwa idada kubwa ya watu na inayofuata ni hiyo mbeya kisha mwanza sasa kama inafuata kuifikia dar kwa idadi ya watu iweje ile laki 7 tu!?? Dar ina watu karibia mil 7 maana yake wikaya 1 ya jiji la dar inawatu mil 1 na ushehe
Kwa taarifa yako,Mbeya ina wa kazi 385,000,,Dar 4300,000 na Kwanza 700,102,,Arusha 415,000 na Morogoro 315000 na Tanga ni chini ya lake 3,hii ni idadi ya wa kazi waishio eneo la mji husika kwa sensa ya 2012,so vigezo vya jiji sio magorofa tu,,ingekuwa hivyo Dodoma na Morogoro ingeitwa jiji
 
Back
Top Bottom