Siasa za Mwigulu Nchemba

Siasa za Mwigulu Nchemba

zmalima

Member
Joined
Dec 29, 2012
Posts
12
Reaction score
3
Nimesoma katika gazeti la Mwananchi leo, nikajikuta nasistushwa sana na kauli ya Mwigulu Nchemba, kwamba watumishi wengi wa umma wanatumia muda mwingi kazini kushabikia siasa hasa vyama vya upinzani badala ya kufanya kazi, na hivyo kukwamisha utekelezaji wa ilani ya CCM. Na anaonya kuwa watumishi wa namna hiyo wajitoe mapema.

Najiuliza: Who is Mwigulu Nchemba?
Je, watumishi wa umma wote lazima wawe wana-CCM?

Waungwana nisaidieni kuhusu kauli hii.
 
Nimesoma katika gazeti la Mwananchi leo, nikajikuta nasistushwa sana na kauli ya Mwigulu Nchemba, kwamba watumishi wengi wa umma wanatumia muda mwingi kazini kushabikia siasa hasa vyama vya upinzani badala ya kufanya kazi, na hivyo kukwamisha utekelezaji wa ilani ya CCM. Na anaonya kuwa watumishi wa namna hiyo wajitoe mapema. Najiuliza: Who is Mwigulu Nchemba? Je, watumishi wa umma wote lazima wawe wana-CCM? Waungwana nisaidieni kuhusu kauli hii.

Kumsuta Mwigulu Nchemba kwa kauli yake ni dalili ya kutojua historia au kuwa na mtazamo finyu. WaTz mnajifanya wajanja sana wa kurukia uongo ili kuficha nyongo zenu na tama zenu. Kwa mfano ikifika kwenye kutaka uRais kila mmoja anataka au yeye mwenyewe au kumpa mtu wa kabila lake au dini yake. Kikwete wetu huyu mpaka kampeni zilimwangusha akazirai, Mchaga usipomtajia CHADEMA au Mbowe wewe ni mpumbavu anaacha hata kuongea na wewe. Mwenendo huu umesababisha WaTz kuishia kuwa watu wa kuganga “majeraha yanayokana na ajali za kujiandalia wenyewe”.

Anayosema Mwigulu Nchemba ni majeraha tu ya ajali ilikwisha kutokea baada ya Ali Hassan Mwinyi kung’oa usukani wa gari lenu na nyie mkampa Mkapa na Kikwete waliendeshe hivyo hivyo. Lazima liende mrama na kutumbukia mikenge na sasa wote mmo ndani ya mkenge mnamlaumu Mwigulu Nchemba kuwa ndiyo kawatokea huko.

Bwana Mkubwa Ali Hassan Mwinyi alikuwa na mahangaiko mengi sana ndani ya Ikulu, moja wapo kuwepo vyama vingi au kuendelea na chama kimoja. Tuakaambiwa kuwa kulipigwa kura ya maoni lakini WaTz wote mkataka kibaki chama kimoja, CCM. Lakini Mheshimiwa sana Mwinyi (alisema) kwa kujali kuwepo kwa demokrasia na kwa kulingana na upepo wa mageuzi uliokuwa ukivuma dunia nzima akaamua (kinyume na kura yenu ya maoni?) kuanziasha mfumo wa vyama vingi. Akaalika watu wenye uwezo wa kifedha kuanzisha vyama vyao ili vishindane na CCM. Hivyo CCM ikiwa imetokea TANU na ikiwa na miaka karibu hamsini mpaka leo bado mnashindana nayo.

Kwenye siasa angalia tu jengo la UVCCM barabara ya Morogoro utaelewa Usalama wa Taifa Wanatengenezwa hapo hapo na viongozi wanaorithi uongozi wa kulinda viongozi walioko madarakani wanatoka hapo hapo. Kwenye ajira ni juzi tu mmekelele watoto wa vigogo Benki Kuu mpaka mkawataja kwa majina, hamjauliza katika mawizara kuna watoto wa akina nani. Mimi binafsi nimebughudhiwa sana na watoto ndani ya Wizara baada ya kuajiriwa na Mama zao. Watoto hawa walikuja kunivuruga kwa kutumwa na mama zao majumbani. Na vurugu katika mawizara ni pamoja na kuchaniana barua na hata kupotezeana majalada mazima. Unaandikiwa barua ya kuitwa kwenye interview mtoto wa jirani anaificha wewe bila kujua hata kama uliandikiwa barua hiyo.

CHADEMA wamebahatika kidogo kuwa na wezi waliokwishaunda umoja wa kujihami mapema. Ukiambiwa Wachaga wanakwenda Xmas kuhesabiwa amini ni kweli kwa sababu si kuhesabiwa tu bali zamani walikuwa wakienda kuunda mikakati ya kuchukua shule zote na ofisi zote , sasa wana mikakati ya kuchukua nchi. CCM inaliona hili kama CCM na wanaCCM Wachaga (ambao bado wana kimfupa cha kuguguna) wanapambana na CHADEMA huku wakijiandaa mara watakapobaini kimfupa hakiana hata juisi ndani yake wanahamia CHADEMA.

Makundi haya ni ya kijasusi na vita ni vya kijasusi kwa hata kufikia viwango vya kurogana na kulishana sumu. Hivyo badala ya kuvunja ukabila, udini na makundi Mwinyi aliimarisha kundi moja la wahuni (CCM) na kukaribisha kuundwe makundi mengine ya wahuni kupambana na CCM. Niwie radhi kuita “wahuni” kwa sababu makundi haya ndiyo yanazalisha wizi, ufisadi, ukabila na udini. Linalobishaniwa sasa ni matokeo tu tarajiwa kwa sababu Mwigulu Nchemba anasemea kundi lake, na anayemsuta naye anahoji kwa nini kundi lake Mwigulu Nchemba halitambui? Kwa hiyo Mwinyi amewatengenezea mzunguko unaitwa "viscious circle".
 
huyu ni pacha wa Malaria Sugu, mtu anayemchukulia huyu mbwiga serious na yeye ni sehemu ya tatizo/
 
Eti huyo ndo mchumi wa BoT, CCM Ni janga kwa taifa letu, mwigulu na lusinde lao moja! Vilevile mfumo wa ccm ni wa kupata viöngozi mavuvuzela!
 
.......Bwana Mkubwa Ali Hassan Mwinyi alikuwa na mahangaiko mengi sana ndani ya Ikulu, moja wapo kuwepo vyama vingi au kuendelea na chama kimoja. Tuakaambiwa kuwa kulipigwa kura ya maoni lakini WaTz wote mkataka kibaki chama kimoja, CCM. Lakini Mheshimiwa sana Mwinyi (alisema) kwa kujali kuwepo kwa demokrasia na kwa kulingana na upepo wa mageuzi uliokuwa ukivuma dunia nzima akaamua (kinyume na kura yenu ya maoni?) kuanziasha mfumo wa vyama vingi. Akaalika watu wenye uwezo wa kifedha kuanzisha vyama vyao ili vishindane na CCM. Hivyo CCM ikiwa imetokea TANU na ikiwa na miaka karibu hamsini mpaka leo bado mnashindana nayo. .....

Sidhani kama ni kweli!
 
Mchemba nadhani kama ndio first class zinazoajiliwa ikulu, basi kazi wanayo, hawajawi kuongea lolote wosomi wakamuelewa, kawa mwanasiasa mjinga kabisa

Eti huyo ndo mchumi wa BoT, CCM Ni janga kwa taifa letu, mwigulu na lusinde lao moja! Vilevile mfumo wa ccm ni wa kupata viöngozi mavuvuzela!
 
Nimesoma katika gazeti la
Mwananchi leo, nikajikuta nasistushwa sana na kauli ya Mwigulu Nchemba,
kwamba watumishi wengi wa umma wanatumia muda mwingi kazini kushabikia
siasa hasa vyama vya upinzani badala ya kufanya kazi, na hivyo
kukwamisha utekelezaji wa ilani ya CCM. Na anaonya kuwa watumishi wa
namna hiyo wajitoe mapema.

Najiuliza: Who is Mwigulu Nchemba?
Je, watumishi wa umma wote lazima wawe wana-CCM?

Waungwana nisaidieni kuhusu kauli hii.

Mwingulu anaweza kufungua zip tu hamna siasa pale, Ni malaya wa kimataifa cjui kajua K... ukubwani!
 
mwigulu nchemba keep ahead brother now nyiramba we are proud with you and others like kitila mkumbo.
 
Sidhani kama ni kweli!
Hizi ndiyo siasa za WaTz, huyu anadhani si kweli hata mambo yaliyotokea wakati huo wote tukiyaona. Watu hawa ndiyo wale ambao ukisema ukweli kumhusu anatoa kauli za ubabaishaji tu halafu anakwenda kukuvizia gizani. Kesho yake utasikia anajigamba kuwa wenye vidomodomo wote huishia kupata ajali (kama iliyokupata). Sema basi Mwinyi alileta mageuzi ya vyama vingi kwa namna ipi unayo"ikumbuka wewe? Wasomi wnahistoria na falsafa wapo watatukosoanani kasema ukweli wewe aua mimi?!
 
Kachelewa!Yeye huo ubunge wa viti maalum?Ina maana kaanza siasa baada ya kuwa mbunge?Kaanzia chuo kikuu,kaendelea nayo B.O.T!Hapo B.O.T ni makao makuu ya Ccm?Kwasababu yeye kapata hataki na wenzake waukwae ubunge?Huwezi acha kuzungumzia siasa,wakati hao wanasiasa kwa nchi tusiojua kutumia sanduku la kura ndio wamiliki wa maisha yetu!Tunamwogelea shetani tukiwa kanisani,tunawaongelea Ccm ktk kila nyaja ya maisha yetu! Mbona wao hawaongelei matatizo wanaongelea Chadema tu,utafikiri ndio ilani yao au ndio maisha bora waliyo ahidi!
 
Mwigulu ni Tatizo, Siana uhakika kama anajua kwa undani watanzania wwengi wanachofikiri
 
Guys kuna watu ambao wakija jamvini na hoja zao ziacheni maana they are useless naweka wachache wewe ongeza

Kinana
Nape
Mwigulu
Willian Malecela

Endeleza hapa chini ili tuwajue tuwe tunaokoa muda kujadili mada za maana hapa
 
Hizi ndiyo siasa za WaTz, huyu anadhani si kweli hata mambo yaliyotokea wakati huo wote tukiyaona. Watu hawa ndiyo wale ambao ukisema ukweli kumhusu anatoa kauli za ubabaishaji tu halafu anakwenda kukuvizia gizani. Kesho yake utasikia anajigamba kuwa wenye vidomodomo wote huishia kupata ajali (kama iliyokupata). Sema basi Mwinyi alileta mageuzi ya vyama vingi kwa namna ipi unayo"ikumbuka wewe? Wasomi wnahistoria na falsafa wapo watatukosoanani kasema ukweli wewe aua mimi?!

Naaminishwa na uchambuzi wako kwamba wewe hukuwepo nchini(aidha ulikuwa mdogo) wakati ule tunapiga kura ya kukubali au la vyama vingi! Misifa unayomlundikia Mzee Mwinyi inatokana zaidi na simulizi za upande mmoja na hazina mshiko wa kisayansi. Pili, hayo usemayo kuhusu wachagga, ni simulizi za magengeni, hazina mshiko wowote wa kisayansi na ndiyo maana umejikanyaga pale ulipohisi wachagga wamo pia CCM. Ungejikanyaga zaidi ungeshituliwa kuwa Wachagga wapo pia CUF,NCCR, UDP na hata kwenye kile kikosi cha UAMSHO kule Zanzibar. Ungejisikia hoi, ungejua wafuasi wa vyama vya siasa hawavutwi na ukabila bali sera za mwanzilishi. Na yumkni sera za mwakilishi zinaweza kuficha haya maovu ya udini, ukabila na ubaguzi. Lakini sio kiwazi wazi. Kwa hivyo kama wewe unataka uaminike, ni lazima uchimbe zaidi uonyeshe na ukamue kilichofichika lakini sio kusemea juu....

Tuliokuwepo tunakumbuka kazi ya ziada aliyoifanya JK Nyerere kuwaaminisha waTZ pamoja na wengi kushabikia Chama Kimoja, muda ulikuwa umefika kwa Vyama Vingi! Sio Ali Hassany Mwinyi aliyefanya kazi hio. Na kwa kuwa kila kitu kwako kimekaa kikabila, kidini na kiubaguzi, umeshindwa kumtaja Nyerere kwenye hili, ili kusudio lako la kumpaisha chati Mwinyi (mwenye imani yako pengine au kabila lako)! Unapinda ukweli mwanangu! Si vizuri kupinda ukweli!
 
Back
Top Bottom