Siasa za CHADEMA hatimaye zaanza kutuchosha wanachama

Siasa za CHADEMA hatimaye zaanza kutuchosha wanachama

Fungo N.

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2011
Posts
252
Reaction score
43
Taratiibu sumu za ZZK zinaanza kutuingia baadhi ya wanachama na kuanza kuamini huenda zzk katengenezewa zengwe ndani ya chama.

Wote tunaona harakati za huyu mtu,kwa harakaharaka tunaweza kudharau lakin anazidi kuongeza wafuasi,kwa walioangalia habari ya star tv mtaungana na mimi kuwa zzk anazidi kuongeza iman ya wanachama juu yake.

Suala hili hakika litakigharimu sana chama kwa kuleta mgawanyiko mkubwa wa chama usio walazima.

Binafsi naweza kusema Huenda CC ya chama ilikurupuka kufanya maamuzi ndo maana ina kigugumizi kuweka hitimisho la sinema hii.

Wanachama wanaelekea kuchoka kutokana na ukimya wa uongozi wa chama huku upande wa pili ukizidi kutumia nafasi hii kujiimarisha zaidi.

Binafsi siasa za chadema zimeanza kunichosha maneno mengi bila vitendo.
 
Kaongeza wanachama gani, kama sumu yake IMEKUINGIA ni chaguo lako wewe na utashi wako na ni haki yako pia kuji associate nae. Just go to him if that is what you feel like.
 
Hiki ndicho kinachofanya nisiwaamini kabisa.... Mna mahaba sana.

Wakati flani wasiwasi ni akili pia. unashauriwa kutomwamini mtu kichwakichwa but it must work both ways.
 
CDM ina wanahis tu na mashabiki waliojaZana huku jf,ile n saccos mkuu sio chama
 
Hatuna mwana chadema mwenye akili kama zako acha kujikomba wewe gamba.

sawa mkuu,ila mimi si gamba kama unavyodhani,sijapenda ukimya wa viongozi wangu katika kuhitimisha hili.
 
Tulia tu kaka utaona namna tutakavyohitimisha hili suala kwa busara kuu na maslahi mapana ya chama.
 
Chama makini hakilazimishwi kutoa maamuzi yake kwa nguvu ya upepo bali ratiba ya vikao vyake.
 
Kama umchoka na cdm nenda kwingine mm kama mm bado naikubali sana chama changu cdm
 
Back
Top Bottom