youngsharo
JF-Expert Member
- Jan 8, 2015
- 2,491
- 500
Wanajukwaa,
Kwanza nianze kwa kuwapa pole wale ambao walishazoea kupata ulaji kupitia mgongo wa CCM, kwa hali ilivyo sasa najua mnaumiza sana vichwa kufikiria juu ya hili, na sidhani tena kama mtakuwa na msaada wowote.
Katika kipindi hiki kigumu ningewashauri muanze kutafuta kazi za kufanya mapema kabisa ilimradi mpate vijisenti vya kujikimu, Bomba la kupatia hela linaenda kufungwa.
Ccm kwa sasa inajaribu kukikimbia kifo lakini siamini kama kifo huwa kinakimbiwa, na hii inatokana na kulemaa wao wenyewe walijisahau wakadhani bado wapo kwenye mfumo wa chama kimoja.
Kwa sasa ni nani mwenye ujasiri wa kutamka neno "CCM" mbele ya mhadhara wa watu tofauti na jukwaani? na likitamkwa ujue si kwa mazuri bali uozo wake na halufu mbaya inayotoka.
Mwanzoni nilijua ni siasa za Tanzania za miaka yote, lakini nimekuja kugundua ni tofauti kabisa, nasikitika kuona chama tawala kuonyesha udhaifu namna hii,Nasubiri Wosia wa mwisho wa chama hiki wakati kinakabidhi majukumu kwa wapinzani KWAHERI CCM.
Kwanza nianze kwa kuwapa pole wale ambao walishazoea kupata ulaji kupitia mgongo wa CCM, kwa hali ilivyo sasa najua mnaumiza sana vichwa kufikiria juu ya hili, na sidhani tena kama mtakuwa na msaada wowote.
Katika kipindi hiki kigumu ningewashauri muanze kutafuta kazi za kufanya mapema kabisa ilimradi mpate vijisenti vya kujikimu, Bomba la kupatia hela linaenda kufungwa.
Ccm kwa sasa inajaribu kukikimbia kifo lakini siamini kama kifo huwa kinakimbiwa, na hii inatokana na kulemaa wao wenyewe walijisahau wakadhani bado wapo kwenye mfumo wa chama kimoja.
Kwa sasa ni nani mwenye ujasiri wa kutamka neno "CCM" mbele ya mhadhara wa watu tofauti na jukwaani? na likitamkwa ujue si kwa mazuri bali uozo wake na halufu mbaya inayotoka.
Mwanzoni nilijua ni siasa za Tanzania za miaka yote, lakini nimekuja kugundua ni tofauti kabisa, nasikitika kuona chama tawala kuonyesha udhaifu namna hii,Nasubiri Wosia wa mwisho wa chama hiki wakati kinakabidhi majukumu kwa wapinzani KWAHERI CCM.