Si kwamba wanaoshabikiwa wana uwezo mkubwa sana, bali ni matokeo ya wananchi kukata tamaa na utawala uliopo. Serikali ya awamu ya tano imechokwa,

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Mar 9, 2015
14,243
34,899
Anaandika Mwanahabari Huru

Wapo watu waliochoka kusikia habari za mateso kwa viongozi wao wa vyama vya upinzani.

Wapo waliochoka kusikia habari za kubambikia kesi watu maarufu, wenye msimamo kinyume na matakwa ya serikali.

Wapo waumini wa dini waliochoka kuona viongozi wao wananyanyasika ndani ya nchi yao, kisa wana misimamo tofauti.

Wapo waliochoka kufanya biashara katika mazingira magumu.

Wapo waliochoka kusikia fulani amenyimwa fursa ya biashara, au kuandaa shughuli, tamasha la shangwe nk kisa ana 'bifu' na wateule wa Rais. Mfano; #NyamaChoma #Fiesta

Wapo watumishi wa umma waliochoka kuona na kusikia vitendo vya uonevu wanavyofanyiwa, wao au wenzao, chini ya mkono wa wateule wasio na utashi wa kuongoza.

Wapo waliochoka kusikia habari za kutekwa na kuuawa kwa wananchi wengine, huku vyombo vya dola vikionesha kutojali, tena kuwashughulikia wanaohoji mambo hayo.

Wapo waliochoshwa na sera za ukandamizaji, zinazoashiria kifo cha mfumo wa demokrasia; sheria za habari, sheria ya takwimu, muswada wa vyama vya siasa, kikokotoo kipya cha malipo ya pensheni nk.

Ndio maana, ni rahisi sana kwa mtu mwenye ushawishi kiasi, kuonekana kwamba ndio hasa mbadala wa hatamu iliyopo. Vijana, wapinzani na wasio wapinzani watamshabikia na kumpa kura nyingi, mamilioni. Kwasababu wamechoshwa na 'ujuha' wa utawala/watawala wa awamu ya tano. Hii si hadithi mpya, ni marudio tu.

Bora 'mtu' mwenye chembe za dhambi, ni mtu, kuliko shetani mwenye chembe za wema, ni Shetani.
 
Hali ngumu,ajira hakuna.Ukilalamika unaitwa mpiga dili.Sijui vijana tunakomolewa na huyu bwana....maana sisi ndiyo tunaathirika kuliko hata wazee wetu.Wote walikuwa wagombea,sasa sisi kumpenda EL imekuwa shida mpaka makalioni.Mzee anatukomoa kabisa maana tangu aingie madarakani ajira ni vi mia mia tu akiguswa vielfu kwa kinyongo na mabango juu wakati wahitimu wa sekta nyeti kama Elimu ni maelfu elfu.Mzee toa ajira nasisi tupate ugali!
 
Nilichojifunza kwa watanzania wezangu toka mfumo wa vyama vingi uingie nchini ni kutokufanya maamuzi sahihi zaidi ya kulalamika, hii inatokana na wengi wetu kutokushiri uchaguzi na kuogopa
 
Anaandika Mwanahabari Huru

Wapo watu waliochoka kusikia habari za mateso kwa viongozi wao wa vyama vya upinzani.

Wapo waliochoka kusikia habari za kubambikia kesi watu maarufu, wenye msimamo kinyume na matakwa ya serikali.

Wapo waumini wa dini waliochoka kuona viongozi wao wananyanyasika ndani ya nchi yao, kisa wana misimamo tofauti.

Wapo waliochoka kufanya biashara katika mazingira magumu.

Wapo waliochoka kusikia fulani amenyimwa fursa ya biashara, au kuandaa shughuli, tamasha la shangwe nk kisa ana 'bifu' na wateule wa Rais. Mfano; #NyamaChoma #Fiesta

Wapo watumishi wa umma waliochoka kuona na kusikia vitendo vya uonevu wanavyofanyiwa, wao au wenzao, chini ya mkono wa wateule wasio na utashi wa kuongoza.

Wapo waliochoka kusikia habari za kutekwa na kuuawa kwa wananchi wengine, huku vyombo vya dola vikionesha kutojali, tena kuwashughulikia wanaohoji mambo hayo.

Wapo waliochoshwa na sera za ukandamizaji, zinazoashiria kifo cha mfumo wa demokrasia; sheria za habari, sheria ya takwimu, muswada wa vyama vya siasa, kikokotoo kipya cha malipo ya pensheni nk.

Ndio maana, ni rahisi sana kwa mtu mwenye ushawishi kiasi, kuonekana kwamba ndio hasa mbadala wa hatamu iliyopo. Vijana, wapinzani na wasio wapinzani watamshabikia na kumpa kura nyingi, mamilioni. Kwasababu wamechoshwa na 'ujuha' wa utawala/watawala wa awamu ya tano. Hii si hadithi mpya, ni marudio tu.

Bora 'mtu' mwenye chembe za dhambi, ni mtu, kuliko shetani mwenye chembe za wema, ni Shetani.
Mtoto ambaye hajawahi kumuona baba yake humuita kila mwanaume baba
 
Kabisa hatuna matumaini kwa chuki,visasi,Kiburi cha madaraka
 
Nikweli imechokwa na Wahuni wapiga dili wachache
Endeleeni kuchoka
ila mkumbuke Bado miaka 7
kwenu nikama miaka 70
Magu ni mpaka 2025
Hupendi Hama nchi
 
Hali ngumu,ajira hakuna.Ukilalamika unaitwa mpiga dili.Sijui vijana tunakomolewa na huyu bwana....maana sisi ndiyo tunaathirika kuliko hata wazee wetu.Wote walikuwa wagombea,sasa sisi kumpenda EL imekuwa shida mpaka makalioni.Mzee anatukomoa kabisa maana tangu aingie madarakani ajira ni vi mia mia tu akiguswa vielfu kwa kinyongo na mabango juu wakati wahitimu wa sekta nyeti kama Elimu ni maelfu elfu.Mzee toa ajira nasisi tupate ugali!
Mlimpenda huyo kwakuwa hayuko ccm
shida yenu
Vibendera hamueleweki
 
Anaandika Mwanahabari Huru

Wapo watu waliochoka kusikia habari za mateso kwa viongozi wao wa vyama vya upinzani.

Wapo waliochoka kusikia habari za kubambikia kesi watu maarufu, wenye msimamo kinyume na matakwa ya serikali.

Wapo waumini wa dini waliochoka kuona viongozi wao wananyanyasika ndani ya nchi yao, kisa wana misimamo tofauti.

Wapo waliochoka kufanya biashara katika mazingira magumu.

Wapo waliochoka kusikia fulani amenyimwa fursa ya biashara, au kuandaa shughuli, tamasha la shangwe nk kisa ana 'bifu' na wateule wa Rais. Mfano; #NyamaChoma #Fiesta

Wapo watumishi wa umma waliochoka kuona na kusikia vitendo vya uonevu wanavyofanyiwa, wao au wenzao, chini ya mkono wa wateule wasio na utashi wa kuongoza.

Wapo waliochoka kusikia habari za kutekwa na kuuawa kwa wananchi wengine, huku vyombo vya dola vikionesha kutojali, tena kuwashughulikia wanaohoji mambo hayo.

Wapo waliochoshwa na sera za ukandamizaji, zinazoashiria kifo cha mfumo wa demokrasia; sheria za habari, sheria ya takwimu, muswada wa vyama vya siasa, kikokotoo kipya cha malipo ya pensheni nk.

Ndio maana, ni rahisi sana kwa mtu mwenye ushawishi kiasi, kuonekana kwamba ndio hasa mbadala wa hatamu iliyopo. Vijana, wapinzani na wasio wapinzani watamshabikia na kumpa kura nyingi, mamilioni. Kwasababu wamechoshwa na 'ujuha' wa utawala/watawala wa awamu ya tano. Hii si hadithi mpya, ni marudio tu.

Bora 'mtu' mwenye chembe za dhambi, ni mtu, kuliko shetani mwenye chembe za wema, ni Shetani.
Mtanyooka tu na vihabari vyenu uchwara!
 
47216986_339773040151727_4044552775449706496_n.jpg
 
Anaandika Mwanahabari Huru

Wapo watu waliochoka kusikia habari za mateso kwa viongozi wao wa vyama vya upinzani.

Wapo waliochoka kusikia habari za kubambikia kesi watu maarufu, wenye msimamo kinyume na matakwa ya serikali.

Wapo waumini wa dini waliochoka kuona viongozi wao wananyanyasika ndani ya nchi yao, kisa wana misimamo tofauti.

Wapo waliochoka kufanya biashara katika mazingira magumu.

Wapo waliochoka kusikia fulani amenyimwa fursa ya biashara, au kuandaa shughuli, tamasha la shangwe nk kisa ana 'bifu' na wateule wa Rais. Mfano; #NyamaChoma #Fiesta

Wapo watumishi wa umma waliochoka kuona na kusikia vitendo vya uonevu wanavyofanyiwa, wao au wenzao, chini ya mkono wa wateule wasio na utashi wa kuongoza.

Wapo waliochoka kusikia habari za kutekwa na kuuawa kwa wananchi wengine, huku vyombo vya dola vikionesha kutojali, tena kuwashughulikia wanaohoji mambo hayo.

Wapo waliochoshwa na sera za ukandamizaji, zinazoashiria kifo cha mfumo wa demokrasia; sheria za habari, sheria ya takwimu, muswada wa vyama vya siasa, kikokotoo kipya cha malipo ya pensheni nk.

Ndio maana, ni rahisi sana kwa mtu mwenye ushawishi kiasi, kuonekana kwamba ndio hasa mbadala wa hatamu iliyopo. Vijana, wapinzani na wasio wapinzani watamshabikia na kumpa kura nyingi, mamilioni. Kwasababu wamechoshwa na 'ujuha' wa utawala/watawala wa awamu ya tano. Hii si hadithi mpya, ni marudio tu.

Bora 'mtu' mwenye chembe za dhambi, ni mtu, kuliko shetani mwenye chembe za wema, ni Shetani.
Kula vumbi mkuu, hii spidi mpaka 2025 na watanzania tunafikiria kuitupilia mbali katiba jamaa tumkalishe hapo hadi 2035.
 
Nikweli imechokwa na Wahuni wapiga dili wachache
Endeleeni kuchoka
ila mkumbuke Bado miaka 7
kwenu nikama miaka 70
Magu ni mpaka 2025
Hupendi Hama nchi
Neno la usiku wa leo walahi
 
kusoma namba sababu wengine eti hawafuati bajeti ni janga la kudekeza. Waziri wa fedha amekwishaonyesha udhaifu wake. Kuidhinisha fedha kinyume na bajeti ni ukiukwaji wa matumizi. Hatufuati mipango bali bajeti tunapiga jukwaani na kuanza kuitekeleza.
Tukumbuke haya
1. Tetemeko la Kagera wahanga walilizwa
2. Zoezi la vyeti wengi wamelizwa
3. Ajali ya wanafunzi Lucky vincent wahanga wamelizwa
4. Kwa sasa hivi wastaafu wanalizwa kwa kikokotoo 25%
Hivi nani ataweka tabasamu kama siyo itakuwa unafiki
 
kusoma namba sababu wengine eti hawafuati bajeti ni janga la kudekeza. Waziri wa fedha amekwishaonyesha udhaifu wake. Kuidhinisha fedha kinyume na bajeti ni ukiukwaji wa matumizi. Hatufuati mipango bali bajeti tunapiga jukwaani na kuanza kuitekeleza.
Tukumbuke haya
1. Tetemeko la Kagera wahanga walilizwa
2. Zoezi la vyeti wengi wamelizwa
3. Ajali ya wanafunzi Lucky vincent wahanga wamelizwa
4. Kwa sasa hivi wastaafu wanalizwa kwa kikokotoo 25%
Hivi nani ataweka tabasamu kama siyo itakuwa unafiki
Mv Nyerere
Acha uvivu bavicha magoti lofaaaaa
 
2025 jaffo anabeba nchi kweupeeee weka kumbukumbu haya maneno
 
Back
Top Bottom