Shuleni walikupa jina gani la utani na kwasababu gani?

Pununkila

JF-Expert Member
Jan 7, 2021
689
1,692
Kipindi Niko shule ya msingi ,sekondari ,na chuo karibia wanafunzi na waalimu walikuwa na majina ya utani

Nakumbuka mm wakati Niko shule ya msingi walikuwa wananiita mtambo kutokana na kukarua hesabu Sana.

O-level ,likaja jina jingine la mr.president hii ni kutokana na siku moja kuwatetea wanafunzi wenzangu ambao walipewa adhabu ya kufyatua tofali na kung'oa visiki kwa kosa ambalo hawakulitenda. Hili jina lilivuma Sana mpaka walimu wakawa wananiita hivyo kwa hiyo shule ikawa na president na head prefect.

Advance ,nikaitwa katekista hii ni ni kutokana na kusoma shule ya seminary ya wakatoliki huko nikabadilika kabisa muda wote mikono iko kifuani.

Chuo, huko nikaitwa mgiriki Hilo jina lilitokana na kuongoza maandamano ya kudai pesa za kujikimu.

TUELEZE WW WALIKUPA JINA GANI NA KWA SABABU GANI..
 
Mapua shule ya msingi👊.
Hapo nilikua mdukuzi sana tu,napendapenda kunusa mambo ya watu
Badae Aurlus Mabele😂😂😂.
Hapo napiga show za bolingo mbaya sana.
Mambo ya Evelyna burkina fasso soukoss la diblo utahama.
Doctor chapombe yapo tu nishabatizwa mpaka leo😁.
 
Duh jamaa o'level waliniita Kirusi au Virus kwasababu nilikuwa nimekonda kinyama. Advance nikapata cheo cha Mess Officer halafu nikawa nipo fair sana wakaniita Humble.

Chuoni nilisoma na machalii zangu wengi wa Arusha wakawa wananita Chalii mpaka class letu lote wakajua ndio jina langu. Wote walikuwa wananiita Chalii.
 
Chris brown coz waliniambia nimefanana nae wakawa wananiambia ww utaondoka tu kwenda kuishi nje hio imekua kweli ila hili la kufanana sikubali
 
Kitaa walikua wananiita mbu coz ya wembamba wangu ila nilikua nachukia, pia walikua wananita tall coz nilikua nacheza kikapu kuanza standard 7
 
Mimi waliinita kibanga kutokana na kuigiza kibanga ampiga mkoloni kwenye somo la kiswahili shule ya msingi, sekondari wakaniita Nyerere kutokana misimamo ya kutetea wanafunzi dhidi kusiginwa hako zao, japo pia kulikuwa na majina mengine ya dhihaka na kuudhi, kule kuudhika tu ni furaha kwa wanaokuita hivyo. Maisha ya shuleni na vyuoni hayakosi visa na vituko.
 
Ahsante mleta mada nami acha niseme jina la utani la shule

Waliniita Mwanasheria na hiyo nikutokana na kuwa nauwezo mkubwa wa kuchanganua masuala ya kisiasa na kijamii

Wakaenda mbali zaidi wakaniita professor hiyo kutokana na bag nililokua natumia la mkanda mmoja hiyo ilikuwa O_ level ingawa mwishowe nilitoka kapa yaani nilizungusha zero nzuri sana
 
Nilikuwa naitwa "VINODI " shule naingia kwa kuchelewa saa mbili asubuhi ,pita nyuma ya vyoo ,mpaka weka begi juu ya dirisha darasana mpaka nazama class....

ikifika saa saba mchana naondoka zangu ,kiufupi nilikuwa sifuati ratiba za shule ...

Nimepigwa Sana bakora za utoro ,kula Sana fimbo za uchafu lakini namaliza hata siku tatu shule siendi ,nikifanya paper ,mtihan wangu unakuwa marking scheme ,nanyoosha 98% na mtihan unanikuta nyumban,muda mwingine mwalimu anabaki nao ,anaufanyia correction ....

Lakini nilikuwa naongoza darasa ,piga divisio one mitihan yote ya mock ,wilaya na mkoa .......


Hilo ndio lilifanya niendelee kukaa shule,vinginevyo ningeshafukuzwa shule ... Kwan nilikuwa naenda kutengeneza one necta ,kitu ambacho mkuu wa shule alikuwa anataka kuongeza idadi ya ufaulu shuleni ....
 
Shule ya msingi - masinzi
Secondary - dogo cheusi
Advance - Yaya toure ( nilikua kiungo moja hatari sana)
 
Shule ya msingi: jini - sabab niliepuka adhabu zote ata kam tukiw staff nlikua napotea chap sana

Sekondari: Vampire - waliniita t wadau labd sabab ya kuw na uwez wa kupigan na kupenda fujo kuliko masom

Advance: Luteni au poti - sabab nlikua kiongoz wa mageng ya kihalif ya shule nakumbuka tushawai tafutwa na polisi miez miwil yan hatupo shulen ila tulkua tunalal bwenin au msituni ila msos kwny mashamb ya shule pamoja na mifug ya walimu tulikula san kuku nakumbuka
 
Back
Top Bottom