Huku mjini ndio walikuwa wanatoka saa nane na nusu....ila nilipohamishiwa huko Geita mzee..shule ni hadi saa kumi na nusu jioni...tena madarasa yalikuwa ni ya kugeukiana...yani sisi darasa la tatu na la tano tulikuwa class moja...mnapeana migongo tu..na la nne wanakaa na la sita..alaf la saba ndo wanakaa pekeyao...
ratiba ilikuwa saa mbili kamili asbui mnaingia class hadi saa nne break fupi..mnarudi class...kutoka tena ni saa sita kamili mchana mnarudi nyumbani kula hadi saa nane kamili.mnaingia class tena hadi saa tisa na nusu..hapo sasa mnaanza stadi za maisha...kama ni kulima shamba la shule, kwenda kwa mwalimu mkuu kujenga nyumba yake ya udongo, au kutafuta kuni kwa mwalimu wa zamu..u name it...hadi kumi unusu tunarejesha majeshi nyumbani