Shule sita nchini kufundisha Kichina

Shule sita nchini kufundisha Kichina

Asprin Achaean kunuu watu vibaya, hujaambiwa kuwa ili upate ajira lzm ujifunze kichina. Soma tena nilichokiandiki, usikurupuke tu, halafu eti elimu elimu elimu.Sasa kwa hapo ninani anahitaji elimu kama sio wewe?
 
Watanzania mlioamka mnajua fika kuwa AJIRA ndo msingi pekee wa maendeleo ya wanetu. !

Neno "ajira" nafikiri wengine maana yake hawajui.Utakuta mtu anaongelea kujiajiri lakini hajui kuwa msomi yeyote anategemea ajira.Mfano mtu umesomea uinjinia wa ujenzi ukaanzisha kampuni yako ya ujenzi.Hiyo kampuni bado itakuwa inategemea ajira.Utasubiri mtu akuajiri umjengee nyumba.Au ukianzisha kampuni ya consultancy hiyo kampuni itategemea kupata ajira mahali ili ifanye kazi.Ajira inakuwa ndio msingi wa maendeleo wa hiyo kampuni.Tatizo wanasiasa huongelea hilo neno "Ajira" mara ingine kwa kebehi kiasi kuwa linaonekana linahusu zaidi waajiriwa wa maofisini!!!! Wakati si kweli.Hata ukiwa na kampuni yako linakuhusu sana.

Nasema watoto wasome kichina waongeze uwezo wao wa kuajiriwa iwe serikalini au wawe kwenye kampuni zao binafsi

Tatizo wengi ukizungumzia ajira wanawaza tu ile ya kuajiriwa serikalini au kwa muhindi na kulipwa kimshahara kila mwezi.Kazi nyingi za kisomi zinategemea ajira.
 
Tatizo watanzania sio watu wanaoona mbali. Kwani hamuoni kama kujifunza lugha yoyote inakufungulia milango kupata opportunities zaidi. Hata hao wazungu sa hivi wanaenda China kujifunza kichina kwa sababu wanajua umuhimu wake kwa sasa katika uchumi.
 
Kiingereza chenyewe tumeshindwa kukifundisha sasa tumerukia kichina.
 
Kuna ma GT humu ni bure kabisa yaani hivi kujifunza lugha tofauti ni kosa...eti mtu unadiliki kusema kiingereza kimetushinda kichina cha nini, kwahiyo kama kiingereza hatuwezi ndio tusijifunze kichina?

Hiyo ni lugha tu na ina faida nyingi zaidi ya hasara, wala hakuna mtu atachomoka nyama kwa kujua kiingereza au kichina au atakuwa masikini.

Ukienda kusoma China kama ya kuanza mwaka wa Masomo ni lazima usome lugha yao mwaka mzima sasa kupunguza adha hiyi kwanini usijifunze tu hapa hapa nyumbani kabla?! Utapungukiwa nini?!
Lugha yako ya taifa inakupiga chenga, unaang'ang'ania lugha za watu. Mchina hakuendelea kwankujifunza lugha za wengine... kadhalika mjapani, mjerumani na wengine wengi.
 
Ningekuwa mimi ningeimarisha zaidi somo la kiingereza. Huwezi kupinga kwamba lugha namba moja duniani ni English. Hata ukienda huko China kwenyewe wanagombania madarasa ya kiingereza. Ukikutana na mfaransa, mGerman, Mreno, MuItaliano wanajua sana lugha zao lakini utashangaa hata English wanajua. English ni lugha ya dunia ambayo ukiijua ina fursa nyingi mno. Leo hii Mtanzania ukitaka uombe scholarship Marekani na UK bila cheti cha lugha (TOEFL) hupokelewi wakati nchi za Africa magharibi wao cheti cha form four yao tu kinatosha. Tunakosa scholarship mamia wanabaki kwenda watoto wa vigogo tu waliosoma English Mediu. Leo mnatuletea kichina sisi wana wa maskini inauma.

Ni wakati muafaka kwa kukitambua Kiingereza kuwa lugha ya taifa kama ilivyo Kiswahili.Katiba itamke wazi kukitambua Kiingereza.Tuache unafiki.Tuwaige wenzetu Kenya.
 
Neno "ajira" nafikiri wengine maana yake hawajui.Utakuta mtu anaongelea kujiajiri lakini hajui kuwa msomi yeyote anategemea ajira.Mfano mtu umesomea uinjinia wa ujenzi ukaanzisha kampuni yako ya ujenzi.Hiyo kampuni bado itakuwa inategemea ajira.Utasubiri mtu akuajiri umjengee nyumba.Au ukianzisha kampuni ya consultancy hiyo kampuni itategemea kupata ajira mahali ili ifanye kazi.Ajira inakuwa ndio msingi wa maendeleo wa hiyo kampuni.Tatizo wanasiasa huongelea hilo neno "Ajira" mara ingine kwa kebehi kiasi kuwa linaonekana linahusu zaidi waajiriwa wa maofisini!!!! Wakati si kweli.Hata ukiwa na kampuni yako linakuhusu sana.

Nasema watoto wasome kichina waongeze uwezo wao wa kuajiriwa iwe serikalini au wawe kwenye kampuni zao binafsi

Tatizo wengi ukizungumzia ajira wanawaza tu ile ya kuajiriwa serikalini au kwa muhindi na kulipwa kimshahara kila mwezi.Kazi nyingi za kisomi zinategemea ajira.
Umeeleza vizuri sana. Lakini kwasababu Ukawa wamesomea ubishi na kupinga, hakuna wanachoelewa
 
Lugha yako ya taifa inakupiga chenga, unaang'ang'ania lugha za watu. Mchina hakuendelea kwankujifunza lugha za wengine... kadhalika mjapani, mjerumani na wengine wengi.
Wapo wachina wanajifunza Kiingereza Kirusi na Lugha nyingine nyingi tu na wala usijifunge ndani ya hilo box

Kujifunza lugha ni kupanua tu uelewa wako wa vitu na lugha tofauti...

Sijui umechukulia kichina ni kama kusoma labda Engineering, au Profession flani? Ile ni lugha tu

Mbona kifaransa kinafundishwa mashuleni lakini si kila mtu kasoma ni mapenzi tu na kuona kama itakusaidia mbeleni wala hulazimishwi...ukiona kichina kwako akina maana basi kuna watu watakiona kina maana

Sio wote wanaoenda china, kuna wengine sisi ni wahapa hapa hata ndege hatujawahi kupanda na hatuoni kama lugha nyingine ni msaada kwetu kiswahili hichi hichi kinachotushinda kinatutosha...

NB:Sio kwasababu mchina ameendelea bila kujifunza lugha nyingine ndio kwamba hakuna wachina wanaoongea kiswahili wapo kibao
 
Dah! Tanzania sijui tuna laan gani! kiingereza chenyewe hatujui, kiswalihi ndio usisema watu badala ya kuandika 'kura' wanasema 'kula'. Kifaransa sijui kilifia wapi, then leo tunakuja na kichina! then what?......................!!! kweli hapa kazi tu
Pole sana ndo wawekezaji waliojaa mpaka kijijini kwenu, huko hakuna mfaransa wala mwingereza ni miaooo tu kwenda mbele
 
Tatizo kuna watanzania wamelala!!! Wawekezaji wakubwa sasa hivi wanaoibukia duniani ni wachina.Ukiwa na ujuzi na ukawa unajua kichina ni rahisi kuajiriwa na wawekezaji wa kichina popote duniani.Nakumbuka kuna kipindi kampuni moja ya mafuta ilikuwa ikitaka marketing manager mtanzania awe na digrii moja ya marketing lakini awe anajua kifaransa.Hakupatikana walipatikana watanzania wana hadi PHD za marketing lakini hawajui kifaransa hadi wakaomba kibali kuajiri raia wa nje na raia waliyempata ni mkenya ambaye alikuwa na digrii ya marketing na alijisomea mwenyewe kwa kujilipia kusoma kifaransa hadi akakimudu barabara.Walipoulizwa kwa nini wanataka mtu ajuaye kifaransa wakasema wanataka asimamie soko lao la mafuta lililoko kongo na burundi ambako wanatumia kifaransa.

Taabu ya baadhi ya watanzania hasa UKAWA huwa ni kubeza tu kila kinachofanywa na serikali!

Watoto wanatakiwa waandaliwe kimataifa ili washindane ajira kimataifa ziwe za kichina,kifaransa,kiingereza n.k Naipongeza serikali ya Magufuli.

Kichina muda si mrefu kitakuwa moja kati ya lugha kubwa mno duniani kutokana na influence yake kwa dunia.

Kila kitu mtalaumu UKAWA ............. kingereza chenyewe tumeshindwa kukimudu. Nafikiri tatizo nalo ni UKAWA!!
 
Kweli mkuu maana huko ndiko rahisi kwa mtoto kufundishika kirahisi. Mtoto anashika lugha haraka kuliko mtu mzima. Sijui kwa nini hawajifunzi kupitia shule za ptimary za mchepuo wa kiingereza. Watoto wansongea kiingereza kuliko hata mwanafunzi wa f4 au 6. Kwa level ya sekondari itasumbua sana
KWA NINI WASIFUNDISHE PRIMARY SCHOOL HICHO KICHINA WAMEENDA KWA SECONDARY SCHOOLS
 
Hio inakuwa optional au ?, Kama ni Optional basi ni Vema ila kama ni Lazima....., basi haina Tija
 
Dah! Tanzania sijui tuna laan gani! kiingereza chenyewe hatujui, kiswalihi ndio usisema watu badala ya kuandika 'kura' wanasema 'kula'. Kifaransa sijui kilifia wapi, then leo tunakuja na kichina! then what?......................!!! kweli hapa kazi tu

Aheri ingekuwa laana kuliko huu upumbavu!! Huu ni zaidi ya ujinga! Kichina cha nini, au ni ili tuweze kutawaliwa na wachina vizuri!!?

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
KWA NINI WASIFUNDISHE PRIMARY SCHOOL HICHO KICHINA WAMEENDA KWA SECONDARY SCHOOLS

Unafikiri wakifundisha primary ndo itasaidia nini kwani?


Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
Mimi kwa uelewa wangu na elimu yangu ya la saba

Mbona mi kuna masomo nilikuwa nafanyavema napata maksi mpaka 95,80 na mengine nilikuwa nachemsha napata mpaka60?
Kweli umeishia la saba. Haiwezekani usome kooote marks za chini kuliko zote upate 60 Hahaha
 
Ni kweli, nilijichanganya mwishoni nikajiunga na makundi mabovu hatimae ni kachemsha ila niliumia sana, lkn mwanzoni nilikuwa napasua sana pamoja na kuchora. Nimekula sana vichori na ice cream kwa kuwachorea ramani mabinti hasa jiografia
 
kitakachoua elimu yetu hapa nchini ni kitendo cha wizara ya elimu kutoshirikisha wadau katika sekta ya elimu. ndalichako asipokuwa makini elimu yetu itazidi kusambaratika...
 
Back
Top Bottom