Ningekuwa mimi ningeimarisha zaidi somo la kiingereza. Huwezi kupinga kwamba lugha namba moja duniani ni English. Hata ukienda huko China kwenyewe wanagombania madarasa ya kiingereza. Ukikutana na mfaransa, mGerman, Mreno, MuItaliano wanajua sana lugha zao lakini utashangaa hata English wanajua. English ni lugha ya dunia ambayo ukiijua ina fursa nyingi mno. Leo hii Mtanzania ukitaka uombe scholarship Marekani na UK bila cheti cha lugha (TOEFL) hupokelewi wakati nchi za Africa magharibi wao cheti cha form four yao tu kinatosha. Tunakosa scholarship mamia wanabaki kwenda watoto wa vigogo tu waliosoma English Mediu. Leo mnatuletea kichina sisi wana wa maskini inauma.