Shule sita nchini kufundisha Kichina

Shule sita nchini kufundisha Kichina

mara ngapi mmewaona wachina hapa kwetu wakijishughulisha na kazi ndogondogo ambazo kwa kawaida ni za mtu wa maisha ya chini?i.
Nenda china kuna watanzania wengi kuliko hao wachina unawaona Tanzania wako kule wakifanya biashara ndogo ndogo za wachina wa hali ya chini pia.Huku Tanzania wamekosa cha kufanya lakini wakaenda china wakapata cha kufanya na kuna wachina hawaoni cha kufanya kule wakija huku wanaona cha kufanya ambacho yule aliyeenda china hakukiona!

Wewe ukipanda ndege kwenda marekani au uingereza kutafuta maisha usishangae angani kupishana na ndege zimejaa wamarekani na waingereza wanakuja kutafuta maisha Tanzania!!! Hilo sio ajabu
 
" Najiuliza hili swali,
Sipati jibu kamili,
Wanachoongea wabongo,
Kimombo kiswahili,
Tuongeze basi kichina,
Tuzidi pata jina,,,,,,,,,,"
Yametimia ya ule wimbo wa bongo fleva
^^
Ha ha ha mkuu umenikumbusha mbali kweli
 
Hiha hihu kobikaniha wahoeha ishikashuha,,,, hehehehe hadi raha kuwa mtanganyika
 
huyu mama nahisi ndio atakuwa wa kwanza kusombwa na dhoruba ya magufuli baadaye.
 
safi sana china language....kingereza tupilia mbali huko... kimetusaidia nini? na ndiomaana mazungu yanatudharau yanatuona mafala
 
Nchi haiishi vituko hii,hili si hitaji la waTZ kwa sasa,mbona viongozi wanakuwa malimbukeni hivi.
Kiswahili&kiingereza vitiliwe mkazo, si vinginevyo!

lugha ya kichina co mbaya..isitoshe kwa sasa wawekezaji wakichina ni wengi hapa nchini kwetu kwaivyo freshi tu....tumekalia kengeza kengeza, ndiomaana wazungu wanatudharau kuikumbatia lugha yao
 
Tatizo kuna watanzania wamelala!!! Wawekezaji wakubwa sasa hivi wanaoibukia duniani ni wachina.Ukiwa na ujuzi na ukawa unajua kichina ni rahisi kuajiriwa na wawekezaji wa kichina popote duniani.Nakumbuka kuna kipindi kampuni moja ya mafuta ilikuwa ikitaka marketing manager mtanzania awe na digrii moja ya marketing lakini awe anajua kifaransa.Hakupatikana walipatikana watanzania wana hadi PHD za marketing lakini hawajui kifaransa hadi wakaomba kibali kuajiri raia wa nje na raia waliyempata ni mkenya ambaye alikuwa na digrii ya marketing na alijisomea mwenyewe kwa kujilipia kusoma kifaransa hadi akakimudu barabara.Walipoulizwa kwa nini wanataka mtu ajuaye kifaransa wakasema wanataka asimamie soko lao la mafuta lililoko kongo na burundi ambako wanatumia kifaransa.

Taabu ya baadhi ya watanzania hasa UKAWA huwa ni kubeza tu kila kinachofanywa na serikali!

Watoto wanatakiwa waandaliwe kimataifa ili washindane ajira kimataifa ziwe za kichina,kifaransa,kiingereza n.k Naipongeza serikali ya Magufuli.

Kichina muda si mrefu kitakuwa moja kati ya lugha kubwa mno duniani kutokana na influence yake kwa dunia.
Hivi Kiingereza miaka yote kimesaidia kivipi Watanzania wengi kuajiriwa Ulaya na Marekani?
 
Swala si kwamba hiyo lugha ni namba moja au ngapi swala ni kuwa hiyo lugha ina manufaa kiuchumi kwa watu wengi au la.KWA SASA FURSA NYINGI ZA ELIMU NA KIUCHUMI kwa watanzania zinapatikana zaidi china kuliko kwenye nchi zingine zinazoongea kwa ufasaha lugha ya kiingereza.Ni rahisi watanzania wengi kwenda kufanya biashara China kuliko Uingereza au marekani.Vijana wengi na wazazi wengi wanaweza somesha watoto wao na kuweza kulipia kule ada kuliko nchi hizo za kiingereza.
Ujinga ni mzigo mzito sana,hivi lugha ya kichina itamsaidia nini hasa Mtanzania na wapi hii lugha ya Kichina itatoa mssada kwetu.Kwenye post yako moja hapo juu umeelezea kuwa China ndio nchi inayokuwa inayokuwa sana kiuchumi na hivyo inawekeza sana ukiwa na maana kuwa haina budi kusoma lugha yao,nijibu haya maswali mawili:

1:Kabla China haijafikia uchumi huu tunaouna sasa,je wao walijifunza lugha gani kwenye nchi yao kutoka katika nchi zile zilizoendelea sana miaka hiyo ya 1960+?

2:Kwa sasa uwekezaji unahama China na kuelekea zaidi Vietenam,uwezekano wa Vietenam kukua kiuchumi hapo baadae ni mkubwa zaidi,je,tutaacha lugha ya kichina na kuhamia kwenye lugha ya Vietenam tena au lugh yoyote kutoka nchi zinazokuwa kiuchumi na uwekezaji hapa nchini?
 
Kiingereza kinamsaidia nini mwananchi wa kawaida kwa mfano?
Kwenye amelekezo ya matumizi ya bidhaa mbalimbali,ajira imesaidia sana kwasababu ndio lugha ya kwanza ya kimataifa na inaongelewa popote duniani...sasa we nenda Colombia hujui kingereza na halafu ongea kichina chako uone.Ila hujanijibu hayo maswali yangu mawili
 
Kwenye amelekezo ya matumizi ya bidhaa mbalimbali,ajira imesaidia sana kwasababu ndio lugha ya kwanza ya kimataifa na inaongelewa popote duniani...sasa we nenda Colombia hujui kingereza na halafu ongea kichina chako uone.Ila hujanijibu hayo maswali yangu mawili
Bidhaa nyingi tunazotumia ni za kichina sio za uingereza wala marekani.Kuna haja ya kujua kichina ili tujue maelekezo ya bidhaa hizo yaliyoandikwa kichina.
 
Ujue mi nasikitika sana kuona watu mnaponda watu wasijifunze lugha zingine muhimu duniani. Hivi watu wakijifunza vitu muhimu vingine kuna hasara gani? Mimi kwa uelewa wangu na elimu yangu ya la saba nijuavyo ni kuwa kujifunza/ kupata ujuzi hakuna hasara isipokuwa kinyume chake, yaani usipojiongeza ni hasara sana kwa kuwa mambo mengi yatakupita, nawashangaa sana nyie mnaojiita wasomi halafu mnabeza watu wasijue lugha zingine duniani. Hivi hata kama kiingereza na kiswahili havifundishwi vema mashuleni hicho ndio kigezo kuwa hatuitaji kujifunza jambo jipya? Mmeniangusha sana leo wasomi wangu. Pia natoa mfano mwingine shuleni enzi zetu tulijifunza masomo mengi kama vile hisabati,historia,siasa(uraia),sayansi, s kilimo,kiswahili,English nk. Kwa hiyo mnataka kuniambia kuwa kama huwezi somo mojawapo basi masomo mengine yasifundishwe? Mbona mi kuna masomo nilikuwa nafanyavema napata maksi mpaka 95,80 na mengine nilikuwa nachemsha napata mpaka60? halafu mnajiita ma-gt. Bure kabisa.kumbukeni kuwa watanzania wengi kama sio Africa nzima kimbilio lao ni chini kwa kila biashara uionayo dukani leo hii unataka mfanyabiashara asafiri na mkalimani?
 
Mmenikera tena sana, nyinye ndio wasomi vyeti, ujue kusoma kitu kingine na uelewa jambo lingine. Na ndio maana hii nchi ina mambo ya ajabu utadhani hakuna alieenda shule. Ni kwa kuwa tuna wosomi-vyeti ambao hawana tija kwa taiga hili.
 
SAFI SANA. NILIKUWA NINASHANGAA KWANINI TUNACHELEWA. SASA NYINGINE ZITEULIWE ZIFUNDISHE KIHINDI PIA.
 
Kuna ma GT humu ni bure kabisa yaani hivi kujifunza lugha tofauti ni kosa...eti mtu unadiliki kusema kiingereza kimetushinda kichina cha nini, kwahiyo kama kiingereza hatuwezi ndio tusijifunze kichina?

Hiyo ni lugha tu na ina faida nyingi zaidi ya hasara, wala hakuna mtu atachomoka nyama kwa kujua kiingereza au kichina au atakuwa masikini.

Ukienda kusoma China kama ya kuanza mwaka wa Masomo ni lazima usome lugha yao mwaka mzima sasa kupunguza adha hiyi kwanini usijifunze tu hapa hapa nyumbani kabla?! Utapungukiwa nini?!
 
Mmenikera tena sana, nyinye ndio wasomi vyeti, ujue kusoma kitu kingine na uelewa jambo lingine. Na ndio maana hii nchi ina mambo ya ajabu utadhani hakuna alieenda shule. Ni kwa kuwa tuna wosomi-vyeti ambao hawana tija kwa taiga hili.
Wasomi watanzania tunasafari ndefu sana ya kutoka hapa tulipo

Na hapa tunajilaumu kwa kutokujua kiingereza lakini ukiangalia sababu kubwa ya kutoku-master lugha hiyo ni hii dharau kama wanayofanya hapa kwamba kiingereza au kichina kitatusaidia nini au kifaransa na kijerumani mwisho wa siku Wakenya haoo wanapaa unawakuta kwenye manchi ya watu na kwetu hapa wamekalia maofisi makubwa ni maboss wakubwa tunabaki kulia lia humu kwenye mitandao "eti" kichina kitatusaidia nini?

Kama huoni faida yake acha watu wasome sijaona sehemu waliposema ni lazima kusoma kichina...
 
Kweli kabisa, eti mtu anaponda hata jambo lenye faida kwa taifa. Kila sehemu watu wanaleta ushabiki
 
Tatizo kuna watanzania wamelala!!! Wawekezaji wakubwa sasa hivi wanaoibukia duniani ni wachina.Ukiwa na ujuzi na ukawa unajua kichina ni rahisi kuajiriwa na wawekezaji wa kichina popote duniani.Nakumbuka kuna kipindi kampuni moja ya mafuta ilikuwa ikitaka marketing manager mtanzania awe na digrii moja ya marketing lakini awe anajua kifaransa.Hakupatikana walipatikana watanzania wana hadi PHD za marketing lakini hawajui kifaransa hadi wakaomba kibali kuajiri raia wa nje na raia waliyempata ni mkenya ambaye alikuwa na digrii ya marketing na alijisomea mwenyewe kwa kujilipia kusoma kifaransa hadi akakimudu barabara.Walipoulizwa kwa nini wanataka mtu ajuaye kifaransa wakasema wanataka asimamie soko lao la mafuta lililoko kongo na burundi ambako wanatumia kifaransa.

Taabu ya baadhi ya watanzania hasa UKAWA huwa ni kubeza tu kila kinachofanywa na serikali!

Watoto wanatakiwa waandaliwe kimataifa ili washindane ajira kimataifa ziwe za kichina,kifaransa,kiingereza n.k Naipongeza serikali ya Magufuli.

Kichina muda si mrefu kitakuwa moja kati ya lugha kubwa mno duniani kutokana na influence yake kwa dunia.
Nimekuelewa.... watanzania waliolala hawajui umuhimu wa watoto kufundishwa kichina.

Watanzania mlioamka mnajua fika kuwa AJIRA ndo msingi pekee wa maendeleo ya wanetu. Na ili wapate ajira ya uhakika shurti wajifunze kichina..

Elimu elimu elimu

vs

Ajira ajira ajira....

Tutafika tu!!
 
Back
Top Bottom