Shule binafsi hawana hoja-NECTA

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,463
911,172
Shule binafsi hawana hoja-NECTA


Na Mwandishi Wetu

BARAZA la Mitihani Tanzania (NECTA) limesema kuwa madai ya Chama cha wamiliki na mameneja wa shule na vyuo visivyo vya
serikali (TAM0NGSCO) ya kutoridhishwa na usahihishaji wa mitihani ya kidato cha nne hayana msingi kwa kuwa taratibu zote zilizingatiwa.

Akizungumza na Majira kwa simu jana, Katibu Mtendaji wa NECTA, Dkt. Joyce Ndalichako alisema pamoja na uhuru wa maoni wa wamiliki hao, hoja zao hazikufanyiwa kazi ya kutosha hivyo kukosa usahihi.

Dkt. Ndalichako alikuwa akijibu madai ya wamiliki hao waliotaka matokeo ya mitihani ya kidato cha nne 2010 yafutwe na mtihani usahihishwe upya kwa sababu hawakuridhishwa na utaratibu uliotumika katika usahihishaji.

Kwa mujibu wa chama hicho usahihishaji wa mtihani kwa mwaka jana haukuwa mzuri kwa sababu ulichukua muda mfupi kutokana na bajeti ya baraza la mitihani kuwa ndogo.

Lakini Dkt. Ndalichako alisema hakukuwa na upungufu wowote wa bajeti kwa kuwa serikali iligharamia shughuli nzima ya kusahihisha mitihani kwa asilimia 100, na kwa kuzingatia ongezeko la watahiniwa mwaka 2010 ukizinganishwa na mwaka uliotangulia.

Alisema muda waliodai kuwa ni mfupi kusahihisha mitihani hiyo haukuwa na tofauti na uliotumika mwaka 2009, na kuwa NECTA ilipanga walimu wa wengi zaidi wa kusahihisha kwa kuzingatia idadi ya wanafunzi waliotahiniwa.

"Mwaka 2009 tulikuwa na makers (wasahihishaji) 3,054 na mwaka jana tuliongeza idadi hadi 4,546 ili kukidhi ongezeko la wanafunzi, hivyo hatukuwa na upungufu na uliotumika ulikuwa sawa sawa," alisema Dkt. Ndalichako.

Dkt. Ndalichako alitoa mfano wa somo la Kiswahili lililochukua muda mrefu kusahihishwa kuwa lilitumia siku 32, walimu 293 mwaka 2009; na mwaka jana likatumia siku 36, walimu 539.

"Kwa hiyo hapo utaona kuwa tulizingatia ongezeko la wanafunzi, tukaongeza wasahihishaji na siku zilikaongezeka. Kwa masomo mengine siku zinatofautiana kulingana na idadi ya watahiniwa na walimu tuliopanga," alisema.

Kuhusu madai kuwa ufaulu mdogo umechangiwa na mtaala mpya, Dkt. Ndalichako alisema ni kweli mtaala ni mpya, lakini hoja hiyo haina ukweli kwa kuwa mkupuo wa kwanza kuhitimu chini ya mtaala huo ni mwaka 2008, hivyo isingekuwa rahisi matokeo mabaya yakawakuta tu wanafunzi wa 2010, miaka mitatu baadaye.

Alipoulizwa sababu za ufaulu mdogo mwaka 2010, alisema yeye hayuko shuleni hivi sasa, lakini kwa ujumla ufaulu unategemea kuwapo kwa walimu wanaojituma kufundisha, wanafunzi wenye ari ya kujifunza na mazingira mazuri ya shule.

"Siwezi kusema moja kwa moja nini kimetokea huku shuleni kwa kuwa mimi sipo huko, na sijafanya uwiano wa kuangalia nani amefaulu au kufeli na kwa sababu gani," alisema.

 
HTML:
Lakini Dkt. Ndalichako alisema hakukuwa na upungufu wowote wa bajeti kwa kuwa serikali iligharamia shughuli nzima ya kusahihisha mitihani kwa asilimia 100, na kwa kuzingatia ongezeko la watahiniwa mwaka 2010 ukizinganishwa na mwaka uliotangulia.
 
Alisema muda waliodai kuwa ni mfupi kusahihisha mitihani hiyo haukuwa na tofauti na uliotumika mwaka 2009, na kuwa NECTA ilipanga walimu wa wengi zaidi wa kusahihisha kwa kuzingatia idadi ya wanafunzi waliotahiniwa.
 
"Mwaka 2009 tulikuwa na makers (wasahihishaji) 3,054 na mwaka jana tuliongeza idadi hadi 4,546 ili kukidhi ongezeko la wanafunzi, hivyo hatukuwa na upungufu na uliotumika ulikuwa sawa sawa," alisema Dkt. Ndalichako.
 
Dkt. Ndalichako alitoa mfano wa somo la Kiswahili lililochukua muda mrefu kusahihishwa kuwa lilitumia siku 32, walimu 293 mwaka 2009; na mwaka jana likatumia siku 36, walimu 539.
 
"Kwa hiyo hapo utaona kuwa tulizingatia ongezeko la wanafunzi, tukaongeza wasahihishaji na siku zilikaongezeka. Kwa masomo mengine siku zinatofautiana kulingana na idadi ya watahiniwa na walimu tuliopanga," alisema.

Asiyekubali kushindwa siyo mshindani..............................
 
Back
Top Bottom