Joseph midimu
Senior Member
- Mar 8, 2024
- 191
- 326
Ulishawahi kukutana na jaribu gani mpaka ukaamini kuwa kweli MUNGU yupo!🙏📌
Ngoja nikuwekee vizuriUlishawahi kukutana na jaribu gani mpaka ukaamini kuwa kweli MUNGU yupo!🙏📌
Sasa unaaminije,, kitu ambacho hukijui wala huna sababu nacho.?Sina sababu kuu ila Mungu kweli yupo!
Ahahahaha!Mimi ni mali yake tu na yeye mwenyewe aliahidi hawezi kuniacha niaibike na ndio maana hata kwenye kesi za ugoni amenitetea mara 3
Toa ushuhuda!Aiseee
Zaburi 23:1-6
[1]BWANA ndiye mchungaji wangu,
Sitapungukiwa na kitu.
[2]Katika malisho ya majani mabichi hunilaza,
Kando ya maji ya utulivu huniongoza.
[3]Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza
Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.
[4]Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti,
Sitaogopa mabaya;
Kwa maana Wewe upo pamoja nami,
Gongo lako na fimbo yako vyanifariji.
[5]Waandaa meza mbele yangu,
Machoni pa watesi wangu.
Umenipaka mafuta kichwani pangu,
Na kikombe changu kinafurika.
[6]Hakika wema na fadhili zitanifuata
Siku zote za maisha yangu;
Nami nitakaa nyumbani mwa BWANA milele. ...siwezi elezea ila Kwa MDA huu wacha niimbe hii zaburi na mfalme daudi
Toa ushuhuda!Mimi binafsi ni muujiza unaotembea. Mwaka jana nilikoswa na ajali ambayo bila mkono wake nisingekuwa hapa.
Hujawahi kusikia?Sasa unaaminije,, kitu ambacho hukijui wala huna sababu nacho.?
Siamini!Mjinga anapokosa jibu la tatizo/changamoto/siri ya jambo hutafuta kisingizio cha kubeba hilo jambo liwe jawabu la tatizo/changamoto/siri hiyo
Uwepo wa Mungu haupimwi kwa kukutana na matatizo/kupata suluhisho la tatizo ambalo hukuwa na jawabu.
Tuache kusingizia hizi imani, tuipe akili+asili sehemu yake badala ya kutafuta sababu za kusingizia.
Mungu hausiki na hayo matatizo+changamoto zako...wake up guys