Shtuka ukipewa sifa hii na mpenzi wako

Shtuka ukipewa sifa hii na mpenzi wako

Andie

JF-Expert Member
Joined
Oct 11, 2011
Posts
712
Reaction score
1,643
Salaam wanajukwaa,

Hii ni kwa wanaume. Kama mke, au mchumba wako anakusifia kwa watu kwamba wewe ni muelewa, shituka kuna sehemu unazembea na mbele ya safari itakugharimu.

Nimekua natafiti wanawake walio comfartable sana kwa wapenzi wao "mume wangu ni muelewa" nimegundua hua wanapewa uhuru zaidi ya kawada. Naweza sema wanaume wao hua wanakua ni loose bolts.

Binafsi hii sifa ya kua muelewa sijawahi kupewa, sitaki kua muelewa na sitaki kuelewa. Usipokua na mipaka wanawake hua hawatosheki na uhuru wanaopewa ukimpa moja atataka mbili, ukimpa mbili atataka tatu na nne.

Kuna staff mwenzetu alikua anazungumza na staff wengine anamsifia mumewe " mimi sina rafiki wanawake marafiki zangu wanaume, hata kwenye simu 98% contacts ni wanaume, mume wangu ni muelewa." Nilimuangalia mara mbili nikaendelea kufanya shughuli zangu.

Ukimruhusu kurudi saa mbili usiku atarudi saa nne huku kasindikiza (nisindikize tu mume wangu ni muelewa) ukimruhusu kupiga story na majirani wanaume, ataenda mpaka kuoga nao bafuni, "twende tu kuoga, mume wangu ni muelewa. (teheee hapa nimeongeza chumvi kidogo ila nadhani unaipata picha) ukimruhusu kujiunga jf atajiunga mpaka Tinder na Badoo (teheee hee na hapa nimeongeza kachumvi)

Vipi we jamaa na wewe ni muelewa? Tuambizane. Vipi na wewe dada mume wako ni muelewa?
 
Mimi pia ni wale raia wasiopenda kuelewa,yani mimi usijaribu kunielewesha maana sitoelewa

na hata nikielewa sitokuonyesha nimeeelewa yani mimi tu ndio ntajua moyoni kua nimekuelewa.

ila eti tuanze argument ya kitu flani utegemee ntakwambia sawa mama nimekuelewa,Haipo hiyo...

Jibu langu huwa ni 1 tu nikikuelewa "Tuache hii topic please tusivurugane zaid,we endelea tu lakini"
 
Uko sawa ilinikuta hiyo dem ananiambia eti mimi mwelewa tena sana hapo nilikuwa nabembeleza tunda huku napewa majibu ya uvumilivu, haikupita mda mrefu naona ugeni wa Brevis halafu jioni naona salam ya kinafiki "my mambo" nikamjibu kiuelewa safi mamaaa, nikaanza kunyanyuka mdogomdogo
 
Kwani kama unataka uhuru si msiolewe muwe masingle mazeri, muwe huru mnaumiza vichwa nini kutafuta kuolewa ?? Simue majamvi ya wageni tu.


Ni lini mara ya mwisho uliona mwanamke analalamikia kuhusu kuolewa hapa JF? 90% ya walalamikaji na wanaolialia kuhusu mapenzi ni wanaume, ni nadra sana kuoana Mwanamke kaanzisha uzi kulalamika na kulia lia, ...
 
Mimi pia ni wale raia wasiopenda kuelewa,yani mimi usijaribu kunielewesha maana sitoelewa

na hata nikielewa sitokuonyesha nimeeelewa yani mimi tu ndio ntajua moyoni kua nimekuelewa.

ila eti tuanze argument ya kitu flani utegemee ntakwambia sawa mama nimekuelewa,Haipo hiyo...

Jibu langu huwa ni 1 tu nikikuelewa "Tuache hii topic please tusivurugane zaid,we endelea tu lakini"
Blaza wewe visa sana 😀😀😀
 
muelewa ndio si kamchukulia kama ulivyo na upumbavu wake
Na yeye anapiga matukio yake sema hamweki wazi uyo mkewe
Ogopa sana mtu muelewa[emoji23] kama sio na yeye ni winga wa kushoto basi amekudharau tu
 
Mie nina calibre hiyo pia ila ni katika conflict resolutions zaidi!

Kwenye mambo ya kishwaini siwezi kukuelewa.
 
Back
Top Bottom