sir.JAPHET
JF-Expert Member
- May 18, 2012
- 699
- 133
[h=2][/h] Jumamosi, Septemba 01, 2012 06:29 Na Pendo Fundisha, Mbeya
ALIYEKUWA Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa Mbeya, Kapteni Sambwee Shitambala na kuhamia Chama Cha Mapinduzi (CCM), amejitokeza na kuchukua fomu ya kugombea nafasi ya ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) kupitia Wilaya ya Mbeya Mjini.
Shitambala alichukua fomu ya kugombea nafasi hiyo na kuirejesha ofisi za CCM wilayani humo, akiwa ni mwanachama wa 12 kati ya waliochukua fomu za nafasi hiyo kuwania nafasi hiyo.
Akizungumza baada ya kurejesha fomu hiyo kwa Kaimu Katibu wa CCM wilayani humo, Julius Msaka, Shitambala alisema nia yake ni kuwatumikia wananchi wote bila kujali itikadi za vyama.
Alisema nia na dhamira ya kugombea nafasi hiyo ni kuwatumikia wananchi ambao kwa sasa wanahitaji mabadiliko ya kweli katika uchumi na kijamii kwa ujumla.
Nia na dhamira yangu ni kuwatumikia wananchi na kukiwakilisha chama changu kwa nia moja ya kutekeleza ilani ya CCM na kuwaletea maendeleo wananchi na niwahakikishie kuwa CCM bado ina nafasi kubwa ya kuongoza nchi, alisema Shitambala.
Wanachama wengine wa CCM waliochukua fomu ya kuwania nafasi hiyo ni pamoja na Obadia Mbilinyi, Shua Mwasanguti, Aggrey Mwasanguti, Dk. Stephen Mwakajumilo, Burton Mwankunda, Frank Mahemba, Edson Kajigili, Maria Nyagawa, Fatuma Kasenge, Richard Shanghvi na Daniel Fusi.
Kwa upande wake, Msaka alisema wanachama wote wamepewa onyo la kutojinadi wala kuchumbia wapiga kura hadi siku ya uchaguzi na vikao vinavyohusika kupendekeza majina ya wagombea waliokidhi vigezo vya nafasi hiyo.
[h=4]Toa Maoni yako kwa habari hii[/h]
ALIYEKUWA Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa Mbeya, Kapteni Sambwee Shitambala na kuhamia Chama Cha Mapinduzi (CCM), amejitokeza na kuchukua fomu ya kugombea nafasi ya ujumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) kupitia Wilaya ya Mbeya Mjini.
Shitambala alichukua fomu ya kugombea nafasi hiyo na kuirejesha ofisi za CCM wilayani humo, akiwa ni mwanachama wa 12 kati ya waliochukua fomu za nafasi hiyo kuwania nafasi hiyo.
Akizungumza baada ya kurejesha fomu hiyo kwa Kaimu Katibu wa CCM wilayani humo, Julius Msaka, Shitambala alisema nia yake ni kuwatumikia wananchi wote bila kujali itikadi za vyama.
Alisema nia na dhamira ya kugombea nafasi hiyo ni kuwatumikia wananchi ambao kwa sasa wanahitaji mabadiliko ya kweli katika uchumi na kijamii kwa ujumla.
Nia na dhamira yangu ni kuwatumikia wananchi na kukiwakilisha chama changu kwa nia moja ya kutekeleza ilani ya CCM na kuwaletea maendeleo wananchi na niwahakikishie kuwa CCM bado ina nafasi kubwa ya kuongoza nchi, alisema Shitambala.
Wanachama wengine wa CCM waliochukua fomu ya kuwania nafasi hiyo ni pamoja na Obadia Mbilinyi, Shua Mwasanguti, Aggrey Mwasanguti, Dk. Stephen Mwakajumilo, Burton Mwankunda, Frank Mahemba, Edson Kajigili, Maria Nyagawa, Fatuma Kasenge, Richard Shanghvi na Daniel Fusi.
Kwa upande wake, Msaka alisema wanachama wote wamepewa onyo la kutojinadi wala kuchumbia wapiga kura hadi siku ya uchaguzi na vikao vinavyohusika kupendekeza majina ya wagombea waliokidhi vigezo vya nafasi hiyo.
[h=4]Toa Maoni yako kwa habari hii[/h]