Wakati Kenya,Uganda, Rwanda na Burundi wamo katika mazungumzo ya kuunda shirikisho la kisiasa na kuitema kando Tanzania, ni wazi kabisa hiyo ni ujanja wa kuitisha Tanzani ili ikurupuke na kujiunga kichwakichwa kwa hofu ya kutengwa. Haiwezi kuwa EAC pasipo Tanzania. Kinacho fanyika sasa ni hasira za mkizi za hawa viongozi masalia walafi wanao waburuza raia wao. Lazima ifahamike wazi kuwa mlengwa mkuu ktk kile kilicho tarajiwa kuwa Shirikisho la Afrika Mashariki si mwingine bali Tanzania na rasilimali zake. Asilimia kubwa ya Wanachama wa EAC mathalan Rwanda,Burundi hawana cha maana kuchangia zaidi ya kutegemea kufaidi fursa na rasilimali za watanzania. Nawapongeza Serikali ya Tanzania kwa kutokukurupukia Shirikisho la "kichovu" na badala yake mkakati uelekezwe SADC kwenye mataifa yenye "akili" na nia ya dhati kuwaondoa wanachama katika umaskini. Fikiria mfano ambapo EAC mnaondoa vikwazo vya usafiri na makazi: Watutsi wote, wakenya, warundi na waganda watalundikana Tanzania kuliko nchi yeyote katk umoja huu wa kinafiki. Mfanö rahisi ni utitiri wa wahamiaji haramu kutoka mataifa hayo ambao hawataki kurudi katika nchizao za halali. Kama vikwazo havijaondølewa hali ndio hii, je pasina vikwazo wakaachiwa waingie tu hali itakuwaje? Je, mtanzania anaweza anaweza kupata ardhi Kenya, Rwanda, burundi kirahisi, ilhali raia husika familia yake haijawahi kumiliki ardhi? Angalia mfumo/aina ya utawala/serikali ya Kigali na Kampala(dictatorship form of governments) kisha linganisha na Kenya na Tanzania hapo utaona ni sawa na kufuga kuku,kunguru na bundi kwenye tundu moja kitu kisichøwezekana. Wacha "waungane" japo muungano wao hautadumu maana ni mungano unao weza kufananishwa na sherehe ya fisi, wageni watarajiwa wamo mbuzi, swala, simba na nyka. "URAFIKI WA MASHAKA"