Shikamoo kilimo

H ata hapa kwenyewe sijaona mahala popote aseme hilo aina ya zao alilopanda zaidi ya kutaja million 10 tu,anafkiri kilimo ni kwa vijana mpeche mpeche ni shughi ya wanaume hiyo tena aliyeenda jando.
 
Kaza moyo kilimo kigumu
 
kwa mkoa gani milioni kumi inafanya hayo yote? nilivoona kichwa cha uzi nilicheka kabla hata sijafungua nikajua kuna mtu kapigwa na kitu kizito😀
 
Pole mkuu,hiyo m10ungeinunulia mazao mwaka huu ingezaa zaidi ya hiyo!
 
Ndio kuanza na kuanza na 10M?
Kweli watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa
Mkuu kwenye utafutaji hizi ni changamoto za kawaida.
Maadam tatizo ni mvua ambalo like nje ya uwezo wake, sio issue kubwa sana. Huyu mkuu apewe maua yake kwa ujasiri na uthubutu huo.

Miaka 3 iliyopita nililima ekari 22 za ufuta lakini kwenye hizo ekari 22 nilikuja kupata 1.4M tu hebu jaribu kuwaza gharama ambazo nilitumia kuanzia kukodi eneo na kulima na vibarua pia. Lakini pamoja na hasara niliyoipata sikukata tamaa, nilichukulia positively na nikajifunza kitu. Na sikukichukia kilimo na niliendelea kujaribu kidogo kidogo kusahihisha makosa nilipokosea.
Mwaka huu nimelima ekari 20 za mpunga, pamoja na kwamba mvua mwaka huu mvua sio nyingi ila eneo nililolima ni bondeni sana hivyo mpunga haujaathirika. Kwa neema ya Mungu mwaka huu nitapata mavuno mazuri.

Nilichojifunza ni kutokukata tamaa na kutokusikiliza sana mawazo ya watu hasa wanaowaza katika kushindwa.
 
Milioni kumi unaweza kuchimba kisima na kuweka pump ya solar???
 
Hili nalo ni kosa lingine.
 
Hakuna tofauti yeyote kati ya kilimo cha mvua na Kamari
 
Pole sana ndugu yangu sema m naona kama unataka kulima moja kwa moja lazima uwaze kuhusu upatikanaji wa maji maana nadhani ndio factor kuu ukiachana na mbegu bora na rutuba ya udongo.... nadhani ungewaza juu ya kilimo cha umwagiliaji maana kwa mtazamo wangu naona kama unataka kulima ni bora ukawaza juu ya kilimo cha umwagiliaji ukiwaza mvua mmmm itakuwa changamoto pole sana ndugu yangu
 
Kwamba ningeanza na pesa kidogo mvua ndio ingenyesha? Stupid.
Take it easy bro. Mwaka huu wengi tunalia. Kumbuka tu huu sio mwisho wa maisha. Somo ambalo binafsi nimejifunza miaka ya nyuma ni never ever, kulima sehemu ambayo hakuna maji mbadala ya mvua ili umwagiliaji ufanyike Mambo yanapotaka kuharibika completely. Mabadiliko ya tabia nchi yanatugharimu. Pole mkuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…