Shigongo unajidhalilisha sana mdogo wangu

Shigongo unajidhalilisha sana mdogo wangu

wiseboy.

JF-Expert Member
Joined
Aug 11, 2014
Posts
2,931
Reaction score
4,549
Neno la Mungu ktk kitabu cha Mithali 14:12 linasema,ipo njia ionekanayo sahihi machoni pa mwanadamu lakini mwisho wake ni njia ya mauti,mdogo wangu tayari umesahau ulipotoka mara hii tu?

Hivi unapata wapi ujasiri wa kuchukua kalamu na kuandika kuwa Magufuli ndiye suluhisho la matatizo ya watanzania?

Umejuaje wakati hata ikulu hajaingia? Kwanini umekuwa mtu wa kujipendekeza sana kwa serikali? Umesahau kuwa umaskini uliowatesa wazazi wako ulisababishwa na serikali ya CCM?

Hujui kuwa aliyekuinua wewe kiuchumi siyo CCM bali ni Mungu wako? Watanzania wenzako wanaoteseka na maisha magumu yaliyosababishwa na CCM umewasahau na kukumbatia serikali hii isiyo na upendo na watu.

Kwa taarifa yako CCM wanakupenda kwa kuwa unacho, ungekuwa kapuku usingemjua JK wala Pombe, wanakupenda kwa kuwa una media na unawafagilia.

Mtu yeyote mwenye hofu ya Mungu hachangamani na watawala wabovu na wala kunywa divai yao, hebu msome nabii Elia, unajiona uko sahihi sana kumbe unapita katika njia ambazo ni machukizo ya Mungu na hutaikwepa ghadhabu.
 
Mkuu Dilemma..bora umelisemea jambo hili, huyu jamaa kwa mda mrefu sasa amekuwa akijipendekeza kwa CCM pasipo kuwa ba sababu za msingi...juzi nimesoma kwny moja ya magazeti yake anampigia debe Magufuli kwa sababu ni msukuma mwenzake na pia akimsafisha kuwa hana tuhuma yyt ya ufisadi akisahau ile kashfa ya uuzwaji nyumba za serikali inayomkabili!

Ifike mahali Shigongo aambiwe ukweli, amezoea kuwasemea vibaya wenzie kwa kuwaandika kwny vigazeti vyake waksti yy mwenyewe ana maovu mengi tu!
 
Last edited by a moderator:
tatizo lipo tena kubwa sn

hawa jamaa watakuja na kusema mbona na EL ana shutuma za ufisadi pasopo kujua kuwa watanzania wanataka mabadiliko nje ya CCM na inawezekana nje ya mfumo wa chama cha UPINZANI pekee sio kwa ccm kamwe .

ila sasa katajirika amesahau kabisa waliomfikisha hapo kuwa ni watanzania masikini walio mwamini na kumchangia jero jero ,buku 10-10 mpaka kaweza kuwa tajiri na sio hao alionao sasa .

ila neno lako liwe kipimo cha idiot alionao
 
Mkuu Dilemma..bora umelisemea jambo hili, huyu jamaa kwa mda mrefu sasa amekuwa akijipendekeza kwa CCM pasipo kuwa ba sababu za msingi...juzi nimesoma kwny moja ya magazeti yake anampigia debe Magufuli kwa sababu ni msukuma mwenzake na pia akimsafisha kuwa hana tuhuma yyt ya ufisadi akisahau ile kashfa ya uuzwaji nyumba za serikali inayomkabili!

Ifike mahali Shigongo aambiwe ukweli, amezoea kuwasemea vibaya wenzie kwa kuwaandika kwny vigazeti vyake waksti yy mwenyewe ana maovu mengi tu!

EL ana usafi gani mbele ya magufuli na hao wamasai wote waliohmia chadema toka ccm hawamuungi mkono mmasai mwenzao EL acheni unafiki shigongo yuko sahihi huyo mtu wenu anaye hangaika kununua uongozi kaifanyia nini Tza mpaka afikie kupewa urais mara elfu mngesemea Dr. Slaa ningwaelewa kuliko huyo fisadi anayehangaika khonga apte urais shu-up yuor mouth vote for Magufuli, hata hivyo EL haijui chadema kwa sababu yeye ni CCM ndiyo maana Prof Limpumba kawaambieni CCM ina wagombea wawili kwenye uchaguzi mwaka huu EL na Dr Magufuli mnakimbia moto mnazama baharini poleni sana ukawa
 
watu bhana! Sasa kosa la shigongo liko wapi! Na mbona mzee kingunge alimnadi Lowasa tena waziwazi!! Na akazidi kuonesha mapenzi aliyonayo kwa Lowasa hata alipokatwa!! Na wachungaji waliojiingiza kwenye siasa! Na wanapayuka kabisa et Lowasa ni Chaguo la Mungu!
 
Shigongo ni opportunist tu yule

Angalia aina ya habari ambazo magazeti yake yanaandika utajua huyu jamaa yupo kimaslahi zaidi
 
watu bhana! Sasa kosa la shigongo liko wapi! Na mbona mzee kingunge alimnadi Lowasa tena waziwazi!! Na akazidi kuonesha mapenzi aliyonayo kwa Lowasa hata alipokatwa!! Na wachungaji waliojiingiza kwenye siasa! Na wanapayuka kabisa et Lowasa ni Chaguo la Mungu!

Mkuu yale ya kingunge hayakuwa mapenzi!
Bali ni mahaba niue!
 
Mkuu Dilemma..bora umelisemea jambo hili, huyu jamaa kwa mda mrefu sasa amekuwa akijipendekeza kwa CCM pasipo kuwa ba sababu za msingi...juzi nimesoma kwny moja ya magazeti yake anampigia debe Magufuli kwa sababu ni msukuma mwenzake na pia akimsafisha kuwa hana tuhuma yyt ya ufisadi akisahau ile kashfa ya uuzwaji nyumba za serikali inayomkabili!

Ifike mahali Shigongo aambiwe ukweli, amezoea kuwasemea vibaya wenzie kwa kuwaandika kwny vigazeti vyake waksti yy mwenyewe ana maovu mengi tu!

Mkuu upo sahihi kabisa, huyu jamaa amekuwa akijipendekeza ccm muda mrefu kabisa
 
Last edited by a moderator:
Bila kuangalia maisha binafsi ya Shigongo, yeye kama binadamu anahaki ya kushabikia upande wake! Kwani hakuna meadia zinazoshabikia upande? Tuache unazi. Si lazima wote wawe kwa masai! ITV inatenda haki? Habari Corperation? Je Mawio?
Nadahini heri Shigongo aliyejipambanua hadharani kuhusudu chama chake kuliko wanaojidai MEDIA HURU huku wakishabikia!
\Sidhani kama hapa JF ni mahala pa unazi na matusi. JF ni HOME OF GREAT THINKERS au sio? Basi tuwe hivyo na si ushabiki uliokubuhu.. Shigongo anafurahia haki yake!
 
Mi sizani kwamba Lowassa ni fisadi kiasi hicho kwanza lowassa alikuwa fisadi ndani ya CCM lkn kama ametoka CCM mi najua ataacha ufisadi lkn magufuli mnasema hana kashfa Ok right lkn kwenye CCM lazima atapat tu kashfa na atakuwa mfisadi sana maan kama lowassa Ndo alikuwa fisadi ndani ya serekali ya CCM na jk wake alipojiuzulu kusinge kuwa na ufisadi tena lkn baada ya kujiuzulu kwake ndo tumeona ufisadi mkubwa Sana ndani ya CCM kama ile ya escrow na mengine mengi yaani hapa cangalii mtu naangalia chama maana rais atakapokuwa madarakani atafanyakazi kulingana na ilani ya chama
 
watu bhana! Sasa kosa la shigongo liko wapi! Na mbona mzee kingunge alimnadi Lowasa tena waziwazi!! Na akazidi kuonesha mapenzi aliyonayo kwa Lowasa hata alipokatwa!! Na wachungaji waliojiingiza kwenye siasa! Na wanapayuka kabisa et Lowasa ni Chaguo la Mungu!

hao ndo bavicha kama huwajui,hawanaga logic kabisa,yani anataka kwa lazima watu wamsifie lowasa,
 
Eti naye ana historia ya maisha yake, wabongo noma
 
Wanoinusuru ccm wote ni mafisadi sijaona mwananchi wa kawaida anaipigania ccm kama tunavyoipigania chadema cuf nccr na vyama vingine huyo shigongo anataka fadhila za ccm huu ndio mwisho wao
 
shigongo ni mwanaccm sikunyingi aligombea ubunge buchosa na Tizeba mwaka 2010 yeye akapigwa chini
 
Back
Top Bottom