Sakhalala
JF-Expert Member
- May 2, 2011
- 575
- 445
Great thinker, mke wa Lisu anahusikaje hapa?Lisu ni mnafiki wa taifa. Ngoja aishi jela kwanza, akitoka huko akute na mke wamelamba na hapo ndipo atajua maana ya uhuru huyu mnafiki
Kuweni na heshima nyinyi watoto, jukwaa hili si la dhihaka na upumbavu ni mahali pa kudadavua hoja ili taifa hili lisonge mbele. Tunatakiwa kujadili hoja na si personalities ili vijana wa nchi hii wapate mikopo ya elimu, wapate ajira, tujikomboe na utegemezi wa fikra na kiuchumi. Tukiwaza ngono na upumbavu tu hatutafika mahali popote, kwanini wewe umeliona la mke wa Lisu wakati tunajadili hoja ya uhalali wa Lisu kukamatwa bila kufikishwa mahakamani na uhalali ya hoja alizoziweka wazi kwenye ule mkutano na waandishi wa habari kama zina mashiko na kuwa na mchango wo wote wa kututoa hapa tulipo ili kusonga mbele. Mkumbuke hili jukwaa linafuatiliwa na watu wengi makini duniani kote, ingawa kwa bahati mbaya kuna watu kama wewe na wengine wanaodhani jukwaa hili ni la mtaani kwenu na la rika lako tu.