Kijana kuwa na subira, Kuna miradi mkubwa wa maji ya kutoka chanzo Cha Nyangao, mradi huu ukikàmilika utahudumia kata za njiani za Malolo, Nandagala,Mnacho, Chienjele, Nkowe , Likunja na kata zote za mjini(kata za Ruangwa na Nachingwea), na vijiji baadhi vya wilaya ya Nachingwea mfano baadhi ya vijiji vya kata ya Chiola(Mtimbo, Chiola A na B, Namauni na Chingunduli).
Kwa Sasa mradi upo katika hatua ya kuunganisha mabomba ya line kuu, Kwa upande wa ujenzi wa matanki tayari umekamilika. Kata ya Malolo Tanki limejengwa kati ya Kijiji Cha Michenga na Chimbila A, pia Kuna Tanki lingine limejengwa juu milimani katika Kijiji Cha Chimbila A, Tanki lingine katika Kijiji Cha Nandagala