Shibuda out

Shibuda out

never

JF-Expert Member
Joined
Apr 4, 2011
Posts
240
Reaction score
77
Wana JF

Kamati kuu ya chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) iliyokutana tarehe 30/4/2011 imeamua kumtoa Shibuda kwenye nafasi ya kukaimu nafasi ya Uenyekiti wa Mkoa wa Shinyanga. Lakini kwenye kikao hicho nusura zichapwe kati ya Lema na Zitto, baada ya Lema kumjia juu Zitto ya kuwa mambo yote hayo ya Shibuda kayasababisha yeye pale Shinyanga kwa kuwaambia baraza la uongozi la mkoa kumteua Shibuda kuwa Kaimu Mwenyekiti, wakati katiba ya chama inasema Kaimu Mwenyekiti anapaswa kutokana na Baraza la Uongozi la Mkoa,

Huku Shibuda akiwa si mjumbe wa Baraza hilo, ndipo aliposimama Zitto na kupinga kauli hizo, ndipo wabunge na wajumbe wa kamati kuu walipo kuja juu na kumkumbusha Zitto juu ya Shibuda ya kuwa aliwatukana wabunge.

Na akaambiwa aombe radhi akakataa na mpaka sasa hajaomba kwa nini Zitto unamtetea huyu jamaa, aliuliza mjumbe huyo ambaye ni swahiba wa Zitto bwana Msafiri Mtemelwa
 
ili balaa gani kati ya zito na lema,
duh mbona mapema au mkuu umechakachua hii kitu,
kuna haja ya kuwa makini na kutumia busara, kama haya yanatokea
chama kiko hatarini na hekima ya wazee inatakiwa kukinusuru chama,
na kanuni za chama zinatakiwa kufuatwa, ili zinapokosewa kuna haja ya kuongea kwa kuheshimiana
ila hii habari yako ninaifanyia uchunguzi kama ina ukweli,
 
Ujumbe wako unachonganisha watu, wabunge, na wana CDM!! hoja haikukaa vizuri. Ungeishia kusema kuwa Kamati kuu imemuengua shibuda na kumuweka fulani kwa sababu fulani; badala ya kuleta malumbano ya vikaoni ambayo hayana tija na hayaendani na hitimisho la hoja yako uliyoleta. Kwa msingi huo, naiona hoja yako imekaa kimajungu majungu tu NA INALENGO LA KUBOMOA CDM!!!
 
ili balaa gani kati ya zito na lema,
duh mbona mapema au mkuu umechakachua hii kitu,
kuna haja ya kuwa makini na kutumia busara, kama haya yanatokea
chama kiko hatarini na hekima ya wazee inatakiwa kukinusuru chama,
na kanuni za chama zinatakiwa kufuatwa, ili zinapokosewa kuna haja ya kuongea kwa kuheshimiana
ila hii habari yako ninaifanyia uchunguzi kama ina ukweli,

mkuu ni kweli kabisa aliyenena hapo juu yupo sahihi, leo nusura lema na zitto zipigwe pale lema alipo mwambia zitto ukweli kuwa aache kutumiwa na hata kaa afanikiwe kwenye mipango yake hiyo na kuwaacha wajumbe wote midomo wazi kila mmoja akishangaa kijana lema asivyo mumunya maneno na kuamua kumtolea uvivu zitto
 
Nadhani hii itasaidia viongozi wa Chadema kufanya maamuzi kikatiba badala ya maoni ya mtu kama ilivyozoeleka.
Wiki iliyopita nilimshauri Dr. Slaa hapa Jamii Forums kwamba ajaribu kutumia vikao vya chama badala ya kufanya maamuzi jukwaani kama ilivyotokea Nzega majuzi. Majibu yake yalionekana kutetea maamuzi yake, lakini ukweli unabaki maamuzi yafanyike katika vikao vya chama na hivyo kama maamuzi yanafanywa kwa uadilifu wa kufuata katiba ya chama hakuna mwenye kumnyoshea kidole fulani na hakuna mwenye kuteleza ulimi kwamba fulani ndiye aliyeamua.

Haya yatokeayo ni ishara nzuri za kujielewa mapungufu na kuweza kurekebisha kasoro ambazo chama cha Chadema wanazo na wanahtaji kufanya kazi. Kujenga chama kiwe imara si kazi ya siku moja.

Wapenzi wa Chadema acheni kushabikia tu hata viongozi wanapoteleza vinginevyo hawatajisahihisha makosa.
Ukomavu ndo kuwa mwazi, kukosoa na kushauri, huko ndiko kujenga chama.
 
Ujumbe wako unachonganisha watu, wabunge, na wana CDM!! hoja haikukaa vizuri. Ungeishia kusema kuwa Kamati kuu imemuengua shibuda na kumuweka fulani kwa sababu fulani; badala ya kuleta malumbano ya vikaoni ambayo hayana tija na hayaendani na hitimisho la hoja yako uliyoleta. Kwa msingi huo, naiona hoja yako imekaa kimajungu majungu tu NA INALENGO LA KUBOMOA CDM!!!

kamanda hii siyo ccm kila kitu kilichopo lazima kiwekwe wazi mimi naungana na mtoa mada anajua kueleza vizuri tena kwakifupi sana na mada kukaa mkao wa kusomeka kwa urahisi
 
mkuu ni kweli kabisa aliyenena hapo juu yupo sahihi, leo nusura lema na zitto zipigwe pale lema alipo mwambia zitto ukweli kuwa aache kutumiwa na hata kaa afanikiwe kwenye mipango yake hiyo na kuwaacha wajumbe wote midomo wazi kila mmoja akishangaa kijana lema asivyo mumunya maneno na kuamua kumtolea uvivu zitto

Wanajamii Forums, kweli John Shibuda kadiri ya msimamo wake alioonyesha tangu awe mbunge wa Chadema hamuoni kama Kaingia Chadema kwa ajili ya ubunge na wala si kwa mapenzi ya chama. Yeye hata alivyojieleza bungeni bado ni mpenzi wa CCM.

Zito Kabwe naye ni ndumila kuwili na kila inapotokea jukumu la viongozi wa Chadema kwenye mikutano au maandamano haishiwi visingizio, lakini kwenye kamati za bunge anakolipwa posho matatizo yote ya kifamilia huisha.

Shibuda si muafaka kwa sasa kuwa mwenyekiti wa mkoa, anahitaji kubaki chini ya uangalizi maalum kwa manufaa ya Chadema na wananchi.
 
HEKO WAHESHIMIWA ZITTO NA LEMA KWA UKOMAVU WENU KIDEMOKRASIA:
HATA SIKU MOJA WALA MSIOGOPE KUKUBALIANA KUTOKUKUBALIANA KATIKA HOJA BILA CHUKI WALA MIZENGWE


Waheshimiwa Zitto, Lema na kamati kuu zima, napenda niwapongeze tena saaana kwa jinsi mnavyohakikisha kwamba NEMBO YETU YA 'DEMOKRASIA' kweli inafanya kazi kiukweli ndani ya chama katika vyombo vyetu vyote vya maamuzi.

Huo ndio ukomavu wa kidemokrasia, uwazi wa kuendesha mambo kuonyesha utayari wa CDM kuongoza taifa bila kwepo TABAKA LA WATEULE ndani ya chama ambao kauli zao hazipingwi. Nawapongeza pia kukataa kubariki maamuzi ya barabarani katika kuteuana ukaimu mwenyekiti huko Shinyanga. Mhe Shibuda sasa ajindae tu kuingia kwenye kinyang'anyiro katika kukijenga chama huku kwa ushirikiano zaidi.

Ndio demokrasia ndani ya vyama inapokomaa na baada ya hapo wote wawili kuendelea kusalimiana na kuendeleza harakati za kufanya kazi kwa pamoja zaidi kutetea maslahi ya umma wa Tanzania.

Nasema ni ndani ya CHADEMA tu ndimo kulimo kiwango hicho cha juu cha demokrasia na misingi ya maadili ya vipi kushika uongozi KWA KUZINGATIA ITIKADI YETU YA 'NGUVU NA MAMLAKA YA UMMA' katika kila tulitendalo na maamuzi tunayoingia.

Mwisho, chama bila mikiki mikiki ya ndani lakini kwa misingi ya disciplined democratic space exercising tayari ni marehemu mtarajiwa kama kilivyo CCM ambako tofauti tu ya maoni kesho yake mtu anakolimbwa kwa kile anachokiamini.

ili balaa gani kati ya zito na lema,
duh mbona mapema au mkuu umechakachua hii kitu,
kuna haja ya kuwa makini na kutumia busara, kama haya yanatokea
chama kiko hatarini na hekima ya wazee inatakiwa kukinusuru chama,
na kanuni za chama zinatakiwa kufuatwa, ili zinapokosewa kuna haja ya kuongea kwa kuheshimiana
ila hii habari yako ninaifanyia uchunguzi kama ina ukweli,
 
Ujumbe wako unachonganisha watu, wabunge, na wana CDM!! hoja haikukaa vizuri. Ungeishia kusema kuwa Kamati kuu imemuengua shibuda na kumuweka fulani kwa sababu fulani; badala ya kuleta malumbano ya vikaoni ambayo hayana tija na hayaendani na hitimisho la hoja yako uliyoleta. Kwa msingi huo, naiona hoja yako imekaa kimajungu majungu tu NA INALENGO LA KUBOMOA CDM!!!
Alitumia uhuru wa kutoa mawazo yake hivyo si vema kulaamu, mbona ya CCM huwa inaandikwa kwa utaratibu kama huu na kujadiliwa tena kwa kicheko.
Kikubwa ninahokiona ni kwamba ndani ya Chadema kuna watu wanajiona wao ndiyo wao na baadhi ya wengine kila wakisemaau kufanya kitu wanaonekana kama wasaliti / wamekosea kama ambavyo comrade Zitto anavyoandamwa na hasa kwa kuwa kwa kiasi fulani haelewani na Slaa na Mbowe kifikra, maana Zitto ana vision kubwa hivyo anaangalia na kuchambua mambo kwa mtazamo wa hali ya juu na kuona miaka kumi mpaka ishirini ijayo.
 
Alitumia uhuru wa kutoa mawazo yake hivyo si vema kulaamu, mbona ya CCM huwa inaandikwa kwa utaratibu kama huu na kujadiliwa tena kwa kicheko.
Kikubwa ninahokiona ni kwamba ndani ya Chadema kuna watu wanajiona wao ndiyo wao na baadhi ya wengine kila wakisemaau kufanya kitu wanaonekana kama wasaliti / wamekosea kama ambavyo comrade Zitto anavyoandamwa na hasa kwa kuwa kwa kiasi fulani haelewani na Slaa na Mbowe kifikra, maana Zitto ana vision kubwa hivyo anaangalia na kuchambua mambo kwa mtazamo wa hali ya juu na kuona miaka kumi mpaka ishirini ijayo.
Too much exaggretion achambue lakini asivunje katiba ya chama kwa malengo binafsi.
 
si kweli kwa hilo jambo kwa sasa, ninavyomfahamu shibuda akiwa anataka kitu huwa nimnyenyevu sana. Yeye alikuwa anaona aibu tu sabab amekikuta chama kina watu makin, sidhan kama maamuz yanaweza kutenguliwa na kamati kuu wakati katiba ya chama ilifuatwa nadhan bwana shibuda kapewa baraka zote za kuingia cc, baada ya kupewa uongozi bwana shibuda kishatoa mikakati mingi.
 
kwa sababu za kinafiki hizo sidhani kamati kuu wali consider sana mtoa mada amekurupuka tu, nadhan maamuzi ya suala hilo si hayo.
 
Alitumia uhuru wa kutoa mawazo yake hivyo si vema kulaamu, mbona ya CCM huwa inaandikwa kwa utaratibu kama huu na kujadiliwa tena kwa kicheko.
Kikubwa ninahokiona ni kwamba ndani ya Chadema kuna watu wanajiona wao ndiyo wao na baadhi ya wengine kila wakisemaau kufanya kitu wanaonekana kama wasaliti / wamekosea kama ambavyo comrade Zitto anavyoandamwa na hasa kwa kuwa kwa kiasi fulani haelewani na Slaa na Mbowe kifikra, maana Zitto ana vision kubwa hivyo anaangalia na kuchambua mambo kwa mtazamo wa hali ya juu na kuona miaka kumi mpaka ishirini ijayo.

Hayo waweza kuwadanganya wenzako mnapokuwa kwenye vijiwe vya kahawa/tangawizi au mnapocheza bao lakini si hapa.

Too low!!

Grooaaaan!!
 
Hata mimi nilishangaa kilichomkimbiza Zitto kusimamia uteuzi wa Shibuda hata habla Magadullah hajazikwa! Lazima ana maslahi binafsi, ndio maana Lema kasema anatumiwa
 
Tujuzeni yaliyojiri baada ya Zitto na Lema kutoleana uvivu! Kuna hatua zozote zilizochukuliwa?
 
Alitumia uhuru wa kutoa mawazo yake hivyo si vema kulaamu, mbona ya CCM huwa inaandikwa kwa utaratibu kama huu na kujadiliwa tena kwa kicheko.
Kikubwa ninahokiona ni kwamba ndani ya Chadema kuna watu wanajiona wao ndiyo wao na baadhi ya wengine kila wakisemaau kufanya kitu wanaonekana kama wasaliti / wamekosea kama ambavyo comrade Zitto anavyoandamwa na hasa kwa kuwa kwa kiasi fulani haelewani na Slaa na Mbowe kifikra, maana Zitto ana vision kubwa hivyo anaangalia na kuchambua mambo kwa mtazamo wa hali ya juu na kuona miaka kumi mpaka ishirini ijayo.

wala hatukuhitaji upofu huu wa mawazo,wewe unamwona Zitto haeleweki na wenzake kwa sababu tu eti ana vision ya miaka10 mbele,yawezekana ila anatakiwa awe bayana ili vision yake ieleweke ama la hatuitaji vision private ya mtu mmoja tunahitaji vision moja ya chama kimoja inayoeleweka

alafu kabla haujaandika hebu tumia akili yako ndogo kujihoji,ni nani alikwambia kweli Dr.na Mbowe hawamtaki Zitto?ulitegemea ni nani atamwamini katika baadhi ya matendo yake yanayofahamika bayana?

Acha utoto,hata angelikuwa ni ndugu yako wa kuzaliwa hauwezi kumwamini tena kama mwanzo mpaka pale atakapo omba msamaha na kubadilika,na labda tu unadhani ni kwa nini mara hii Zitto alikabiliwa na upinzani pale jimboni kwake tofauti na ilivyokuwa awali,go and have a research,NYAMBAFUUUUUUUUUUUUUUU
 
Ujumbe wako unachonganisha watu, wabunge, na wana CDM!! hoja haikukaa vizuri. Ungeishia kusema kuwa Kamati kuu imemuengua shibuda na kumuweka fulani kwa sababu fulani; badala ya kuleta malumbano ya vikaoni ambayo hayana tija na hayaendani na hitimisho la hoja yako uliyoleta. Kwa msingi huo, naiona hoja yako imekaa kimajungu majungu tu NA INALENGO LA KUBOMOA CDM!!!

Mkuu hutaki watu tuambiwe ukweli? Suala hapa ni kama kweli kilichotokea ndicho hicho ama jamaa ameongeza chumvi. Kama alichoandika ndicho kilichotokea basi ni vema na haki nasi humu kujulishwa kilichotokea nyuma ya pazia. Mbona tulikuwa tunashangilia yaliyokuwa yakitokea nyuma ya pazia wakati CCM wanalumbana kuvuana magamba?
 
Kwa kweli Huyu Zitto haeleweki, kila controversial ya CDM lazima ahusike. Isije ikawa amepandikizwa kuiua CDM.
 
Tujuzeni yaliyojiri baada ya Zitto na Lema kutoleana uvivu! Kuna hatua zozote zilizochukuliwa?

Baada ya hapo busara za mwenyekiti zikatumika na ndipo lema akasema na heshimu tu meza kuu isingekuwa hivyo leo zitto ungetuambia usaliti huu unautoa kwanani na ni kwanini? Ndipo ikafika mahala pa kupiga kura, wanaotaka shibuda awepo alikuwa mmoja wasiyo taka walikuwa 18 na zitto, mama yake, mkumbo hawakupiga kura upande wowote ule. Acha ni seme ukweli nimefurahi sana kwa lema kujiunga na sisi kwenye kamati kuu ametutoa uoga wa kumuona fulani kama mungu hivi...
 
Back
Top Bottom