BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,005
Na Mwandishi Wetu
Mwananchi
10/7/2009
MBUNGE wa Maswa, John Shibuda (CCM), ameendelea kuwa mwiba kwa Baraza la Mawaziri, baada ya kuhoji mantiki ya rasimu ya itifaki ya matumizi ya Mto Zambezi, iliyowasilishwa na Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Profesa Mark Mwondosya kwenye Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama.
Awali Shibuda aliwahi kuhoji bungeni tafsiri ya uzalendo kwa Baraza la Mawaziri ambalo mwenyekiti wake ni Rais; kutokana na nchi kuingia katika mikataba mingi mikubwa ya kifisadi ambayo hupita kwenye chombo hicho kikuu cha maamuzi.
Jana, Shibuda aliendeleza msimamo huo baada ya kumbana Mwandosya kwa kuhoji mantiki ya rasimu ya itifaki hiyo kwa nchi alipoiwasilisha kwenye kamati hiyo kujadiliwa, akitaka maelezo ya kina ikiwemo athari na manufaa yake.
Kwa mujibu wa habari kutoka ndani ya kikao hicho cha kamati, Shibuda ambaye alichelewa kuingia ukumbini, alitaka ufafanuzi na kutishia kuwa ikipita bila ufafanuzi huo, ataipinga bungeni.
Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Musa Azzan Zungu, alipoulizwa kuhusu hilo, kwanza alishtuka na kuhoji kwa kusema: "Ehee... we nani kakwambia hivyo?"
Zungu alifafanua akisema: "Taarifa ninayoweza kukwambia ni kwamba, kweli waziri aliwasilisha rasimu hiyo na kesho (leo) kikao kinaendelea njoo".
Awali, Waziri Mwandosya alipoulizwa alitaka mwandishi awasiliane na Zungu ambaye ni Makamu Mwenyekiti kwani yeye alikwishaiwasilisha kwenye kamati.
Lakini vyanzo hivyo huru, vilifahamisha kuwa Shibuda alichelewa kuingia, alipoingia alipitia rasimu hiyo ya matumizi ya Mto Zambezi inayohusu bonde lake, lakini akataka kile alichokiita mchanganuo wa mambo muhimu.
Vyanzo hivyo huru viliongeza kwamba, Profesa Mwandosya alisema tayari suala hilo limejadiliwa kwenye Baraza la Mawaziri; lakini Shibuda, akasisitiza chombo hicho cha maamuzi ni mhimili tofauti na bunge.
Kwa mujibu wa duru hizo, Shibuda alitaka waziri aandae mchanganuo wa rasimu hiyo, ikiwa ni pamoja na kuona maeneo makuu ambayo nchi itanufaika.
"Alichosema ni kwamba, anataka mantiki ya kilichoandikwa, si maandishi akidai kuwa nchi hii ni tajiri wa mikataba mibovu, hivyo alitaka kujua faida na hasara," kilifafanua chanzo hicho.
Vyanzo hivyo vilidai zaidi kwamba, alitaka kuona uchambuzi huo wa kina ili kuachana na dhana ya kupitisha rasimu za kimataifa kwa sababu mbalimbali, ama kwa urafiki wa viongozi waliopo madarakani.
"Anachokisema ni kwamba, itifaki za kimataifa hazipaswi kupitishwa kwa sababu, labda ya urafiki wa viongozi waliopo madarakani; kwani kama akija kiongozi mwingine na mikataba hiyo ikawa na utata, inaweza kuwa na athari kwa nchi yetu," kilifafanua chanzo kingine.
Alipoulizwa kuhusu hilo, Shibuda, alisema: "Mimi sina mamlaka ya kuzungumzia mambo ya ndani ya kamati, muulize Zungu," alisema na kukata simu.
Mto Zambezi ambao ni wa nne kwa urefu barani Afrika, unatumika kama chanzo kikuu cha kuzalisha umeme katika nchi za kusini mwa Afrika.
Mpaka sasa mto huo una mabwawa makubwa na miradi midogo ya kuzalisha umeme, ambao unatumika kwa nchi za Zambia, Angola, Zimbabwe, Msumbiji na Afrika Kusini.
Mabwawa makubwa ya kuzalisha umeme ambayo ni Cabbora lililoko Msumbiji na Kariba lililoko mpakani mwa Zambia na Zimbabwe na miradi midogo ya kuzalisha umeme ipo kwenye mto huo katika maporomoko ya Victoria mpakani mwa Zambia na Zimbabwe.
Kumekuwepo mikakati ya umeme unaozalishwa katika mto huo kutaka utumike katika nchi zote za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (Sadc) ambayo Tanzania ni mwanachama. Mara kadhaa Rais Jakaya Kikwete amezungumzia kuwepo kwa uwezekano wa nchi yetu kupata umeme kutoka Zambia ambao kwa asilimia kubwa unazalishwa katika Mto Zambezi.
Mwananchi
10/7/2009
MBUNGE wa Maswa, John Shibuda (CCM), ameendelea kuwa mwiba kwa Baraza la Mawaziri, baada ya kuhoji mantiki ya rasimu ya itifaki ya matumizi ya Mto Zambezi, iliyowasilishwa na Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Profesa Mark Mwondosya kwenye Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama.
Awali Shibuda aliwahi kuhoji bungeni tafsiri ya uzalendo kwa Baraza la Mawaziri ambalo mwenyekiti wake ni Rais; kutokana na nchi kuingia katika mikataba mingi mikubwa ya kifisadi ambayo hupita kwenye chombo hicho kikuu cha maamuzi.
Jana, Shibuda aliendeleza msimamo huo baada ya kumbana Mwandosya kwa kuhoji mantiki ya rasimu ya itifaki hiyo kwa nchi alipoiwasilisha kwenye kamati hiyo kujadiliwa, akitaka maelezo ya kina ikiwemo athari na manufaa yake.
Kwa mujibu wa habari kutoka ndani ya kikao hicho cha kamati, Shibuda ambaye alichelewa kuingia ukumbini, alitaka ufafanuzi na kutishia kuwa ikipita bila ufafanuzi huo, ataipinga bungeni.
Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Musa Azzan Zungu, alipoulizwa kuhusu hilo, kwanza alishtuka na kuhoji kwa kusema: "Ehee... we nani kakwambia hivyo?"
Zungu alifafanua akisema: "Taarifa ninayoweza kukwambia ni kwamba, kweli waziri aliwasilisha rasimu hiyo na kesho (leo) kikao kinaendelea njoo".
Awali, Waziri Mwandosya alipoulizwa alitaka mwandishi awasiliane na Zungu ambaye ni Makamu Mwenyekiti kwani yeye alikwishaiwasilisha kwenye kamati.
Lakini vyanzo hivyo huru, vilifahamisha kuwa Shibuda alichelewa kuingia, alipoingia alipitia rasimu hiyo ya matumizi ya Mto Zambezi inayohusu bonde lake, lakini akataka kile alichokiita mchanganuo wa mambo muhimu.
Vyanzo hivyo huru viliongeza kwamba, Profesa Mwandosya alisema tayari suala hilo limejadiliwa kwenye Baraza la Mawaziri; lakini Shibuda, akasisitiza chombo hicho cha maamuzi ni mhimili tofauti na bunge.
Kwa mujibu wa duru hizo, Shibuda alitaka waziri aandae mchanganuo wa rasimu hiyo, ikiwa ni pamoja na kuona maeneo makuu ambayo nchi itanufaika.
"Alichosema ni kwamba, anataka mantiki ya kilichoandikwa, si maandishi akidai kuwa nchi hii ni tajiri wa mikataba mibovu, hivyo alitaka kujua faida na hasara," kilifafanua chanzo hicho.
Vyanzo hivyo vilidai zaidi kwamba, alitaka kuona uchambuzi huo wa kina ili kuachana na dhana ya kupitisha rasimu za kimataifa kwa sababu mbalimbali, ama kwa urafiki wa viongozi waliopo madarakani.
"Anachokisema ni kwamba, itifaki za kimataifa hazipaswi kupitishwa kwa sababu, labda ya urafiki wa viongozi waliopo madarakani; kwani kama akija kiongozi mwingine na mikataba hiyo ikawa na utata, inaweza kuwa na athari kwa nchi yetu," kilifafanua chanzo kingine.
Alipoulizwa kuhusu hilo, Shibuda, alisema: "Mimi sina mamlaka ya kuzungumzia mambo ya ndani ya kamati, muulize Zungu," alisema na kukata simu.
Mto Zambezi ambao ni wa nne kwa urefu barani Afrika, unatumika kama chanzo kikuu cha kuzalisha umeme katika nchi za kusini mwa Afrika.
Mpaka sasa mto huo una mabwawa makubwa na miradi midogo ya kuzalisha umeme, ambao unatumika kwa nchi za Zambia, Angola, Zimbabwe, Msumbiji na Afrika Kusini.
Mabwawa makubwa ya kuzalisha umeme ambayo ni Cabbora lililoko Msumbiji na Kariba lililoko mpakani mwa Zambia na Zimbabwe na miradi midogo ya kuzalisha umeme ipo kwenye mto huo katika maporomoko ya Victoria mpakani mwa Zambia na Zimbabwe.
Kumekuwepo mikakati ya umeme unaozalishwa katika mto huo kutaka utumike katika nchi zote za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (Sadc) ambayo Tanzania ni mwanachama. Mara kadhaa Rais Jakaya Kikwete amezungumzia kuwepo kwa uwezekano wa nchi yetu kupata umeme kutoka Zambia ambao kwa asilimia kubwa unazalishwa katika Mto Zambezi.