Muswada mpya wa vyama vya siasa CCM ijiangalie mara mbili mbili

Bwana Kheri

Member
Oct 31, 2018
26
49
Leo ni Siku ya Uhuru. 9 December. Ni siku muhimu sana kwa nchi yetu. Pamoja na umuhimu huo, nawakumbusha Watanzania wenzangu. CCM na msiokuwa CCM. Chadema ama CUF, sote kwa pamoja tunapaswa kuuchukia muswada mpya wa vyama vya siasa kwasababu unatugawa Watanzania na hauna tija. Ingawa muswada huu utapigiwa debe sana na watu wa CCM, lakini CCM wanapaswa kujua kwamba nchi yetu sio mali binafsi ya CCM na wana CCM.

Itakapotokea siku CCM imeanguka, chama hiki kikongwe kitashindwa kujiendesha kwa sababu ya kupitisha sheria ngumu na kandamizi kwa sababu ya kuvihujumu vyama vya siasa vya upinzani. Hivyo CCM na wafuasi wake wakiwamo wabunge wao waupitishe muswada huu kama wanajua chama chao kitatawala milele, la kama kuna siku CCM itakuwa chama cha upinzani, please, Watanzania wenzangu tusikubali kabisa muswada huu upite kwa maslahi mapana ya nchi yetu bila kuangalia itikadi za vyama vyetu. Tanzania ni bora kuliko vyama vyote vya siasa.
 
Wanachokosea wana ccm ni kuamini kuwa muswada huu utaipa nguvu ccm, wasichojua ni kuwa muswada huu UNAWAPA NGUVU WATU WACHACHE sana ndani ya ccm. Wataitumia Nguvu hiyo kuwabana wengine ndani ya ccm. Wote tutakuwa wanyonge.
 
Wanachokosea wana ccm ni kuamini kuwa muswada huu utaipa nguvu ccm, wasichojua ni kuwa muswada huu UNAWAPA NGUVU WATU WACHACHE sana ndani ya ccm. Wataitumia Nguvu hiyo kuwabana wengine ndani ya ccm. Wote tutakuwa wanyonge.
Sijui kama wanalijua hili. Huwa wanagundua style muziki umeshazimwa.
 
Kama wasomi wetu wamefikia kutunga sheria za Aina hii katika Karne hii ambayo Dunia ipo kiganjani basi hatuna aja ya kusoma maana unachokisoma na unachokwenda kutenda ofisini hakifanani.

Hii ni moja ya sheria inayokwenda kuligawa Taifa na ambayo hata mwanafunzi wa mwaka wa kwanza wa sheria hawezi kudraft kitu Cha hivi.

Yapo Mambo mengine wasomi wetu wanafanya uzeeni yanawaondolea ubinadamu na kuwapa laani kwao na vizazi vyao.Huwezi kumkabidhi jukumu la kuamua siasa za nchi mtu mmoja na ukawa na akili timamu, huu ni ulimbukeni na kudhalilisha taaluma zetu.

Maprofesa badala ya kuja kulijenga Taifa wanakuja kuligawa kwa maslahi mishahara ambayo Leo wakiondoka Dunia yawezekana hata familia zao zisifaidike nayo, inakera hata kusoma
 
Kama wasomi wetu wamefikia kutunga sheria za Aina hii katika Karne hii ambayo Dunia ipo kiganjani basi hatuna aja ya kusoma maana unachokisoma na unachokwenda kutenda ofisini hakifanani.

Hii ni moja ya sheria inayokwenda kuligawa Taifa na ambayo hata mwanafunzi wa mwaka wa kwanza wa sheria hawezi kudraft kitu Cha hivi.

Yapo Mambo mengine wasomi wetu wanafanya uzeeni yanawaondolea ubinadamu na kuwapa laani kwao na vizazi vyao.Huwezi kumkabidhi jukumu la kuamua siasa za nchi mtu mmoja na ukawa na akili timamu, huu ni ulimbukeni na kudhalilisha taaluma zetu.

Maprofesa badala ya kuja kulijenga Taifa wanakuja kuligawa kwa maslahi mishahara ambayo Leo wakiondoka Dunia yawezekana hata familia zao zisifaidike nayo, inakera hata kusoma
Orodhesha mapungufu ya huo mswaada na sio kulalamika tu bila kujua kilichoondikwa kwa kufuata mkumbo tu.sheria zote zina dhima au mantiki ndani yake hakuna sheria inaytungwa ili kumkomoa mtu fulani.

Mswaada ni mzuri na utapita na kuwa sheria.
 
Kama wasomi wetu wamefikia kutunga sheria za Aina hii katika Karne hii ambayo Dunia ipo kiganjani basi hatuna aja ya kusoma maana unachokisoma na unachokwenda kutenda ofisini hakifanani.

Hii ni moja ya sheria inayokwenda kuligawa Taifa na ambayo hata mwanafunzi wa mwaka wa kwanza wa sheria hawezi kudraft kitu Cha hivi.

Yapo Mambo mengine wasomi wetu wanafanya uzeeni yanawaondolea ubinadamu na kuwapa laani kwao na vizazi vyao.Huwezi kumkabidhi jukumu la kuamua siasa za nchi mtu mmoja na ukawa na akili timamu, huu ni ulimbukeni na kudhalilisha taaluma zetu.

Maprofesa badala ya kuja kulijenga Taifa wanakuja kuligawa kwa maslahi mishahara ambayo Leo wakiondoka Dunia yawezekana hata familia zao zisifaidike nayo, inakera hata kusoma
Angesema mwanasiasa ungelalamika pia wanasiasa hawafai tunahitaji msomi,amejitokeza msomi unakurupuka tena kukashifu alichofanya.papo hapo umekuja na maneno tupu bila kusema hayo mapungufu ni yapi aliyoyasema Kabudi.yani waTanzania sijui ni nani aliyeturoga.hapo usikute wewe mwenyewe hujawahi hata kua balozi wa nyumba kumi kumi wala hujui chochote juu ya kuwaongoza watu.kwanza kwa Afrika nzima hii tulitakiwa kuipinga sheria ya mfumo wa vyama vingi.siasa huku Afrika haikutakiwa mapema kiasi hiki.huku tulitakiwa kupiga kazi kwa bidii kuliko kuongea maneno ya siasa
 
Orodhesha mapungufu ya huo mswaada na sio kulalamika tu bila kujua kilichoondikwa kwa kufuata mkumbo tu.sheria zote zina dhima au mantiki ndani yake hakuna sheria inaytungwa ili kumkomoa mtu fulani.

Mswaada ni mzuri na utapita na kuwa sheria.
Anza wewe kuweka mazuri ya huo muswada unaosema ni mzuri maana mleta mada kesha sema huwezi mpa mtu mmoja mamlaka ya kuamua siasa za nchi nzima
 
Kama wasomi wetu wamefikia kutunga sheria za Aina hii katika Karne hii ambayo Dunia ipo kiganjani basi hatuna aja ya kusoma maana unachokisoma na unachokwenda kutenda ofisini hakifanani.

Hii ni moja ya sheria inayokwenda kuligawa Taifa na ambayo hata mwanafunzi wa mwaka wa kwanza wa sheria hawezi kudraft kitu Cha hivi.

Yapo Mambo mengine wasomi wetu wanafanya uzeeni yanawaondolea ubinadamu na kuwapa laani kwao na vizazi vyao.Huwezi kumkabidhi jukumu la kuamua siasa za nchi mtu mmoja na ukawa na akili timamu, huu ni ulimbukeni na kudhalilisha taaluma zetu.

Maprofesa badala ya kuja kulijenga Taifa wanakuja kuligawa kwa maslahi mishahara ambayo Leo wakiondoka Dunia yawezekana hata familia zao zisifaidike nayo, inakera hata kusoma
Dah muheshimiwa Dr Willibrod Slaa slaa kalike huu uzi. Zinamrudia nini akili?
 
Sio yeye peke yake, wapo wengi tu ambao walikua ma Lecturers wazuri sana. Pindi wakifundisha ilikua wanafunzi hawakosi darasani.

***Dr. Ackson Tulia, Proffesor Kabudi, Dr. Harrison Mwakyembe, Dr. Clement Mashamba, Dr. Ally Posi*** (Wote ni mabingwa wa sheria na walimu wazuri)

Naomba wakumbuke mambo mliokua mkifundisha kwenye Lectures vyuoni, mlivyokua mkihimiza undergraduates juu ya swala zima na umuhimu wa ADMINISTRATIVE LAW, HUMAN RIGHTS LAW, CONSTITUTIONAL LAW, DIVISION OF POWERS, DELEGATED LEGISLATIONS.

Mungu anawaona,
 
Orodhesha mapungufu ya huo mswaada na sio kulalamika tu bila kujua kilichoondikwa kwa kufuata mkumbo tu.sheria zote zina dhima au mantiki ndani yake hakuna sheria inaytungwa ili kumkomoa mtu fulani.

Mswaada ni mzuri na utapita na kuwa sheria.
Kwanini wewe usioneshe uzuri wake?
Miswada mingi tu na mibovu ilishawahi kupitishwa!Rejea miswada ya madini,miswada ya gas NK ilipitishwa haraka haraka huku kukiwa na malalamiko kutoka upinzani!Leo kiko wapi?JPM ndio analalamikia Gas yetu kubebwa!

Nchi hii si ajabu kutengeneza sheria kwa ajili ya kuwashughulikia wapinzani,hilo lipo sana!
Hata sheria ya Takwimu ilikuwa na lengo la kuwaziba midomo wanaoihoji serikali,IMF na WB wakaingilia na sheria hiyo imefanyiwa marekebisho!
 
Mwache anatumia nafasi yake kwa sasa lakini siku akiwa nje ya kazi ndio atajua kumbe alichanganya pumba na mashudu akaacha nafaka
 
Kama wasomi wetu wamefikia kutunga sheria za Aina hii katika Karne hii ambayo Dunia ipo kiganjani basi hatuna aja ya kusoma maana unachokisoma na unachokwenda kutenda ofisini hakifanani.

Hii ni moja ya sheria inayokwenda kuligawa Taifa na ambayo hata mwanafunzi wa mwaka wa kwanza wa sheria hawezi kudraft kitu Cha hivi.

Yapo Mambo mengine wasomi wetu wanafanya uzeeni yanawaondolea ubinadamu na kuwapa laani kwao na vizazi vyao.Huwezi kumkabidhi jukumu la kuamua siasa za nchi mtu mmoja na ukawa na akili timamu, huu ni ulimbukeni na kudhalilisha taaluma zetu.

Maprofesa badala ya kuja kulijenga Taifa wanakuja kuligawa kwa maslahi mishahara ambayo Leo wakiondoka Dunia yawezekana hata familia zao zisifaidike nayo, inakera hata kusoma
Hii sheria inaonekana imetungwa na mtu anayelala na mafaili kitandani wengine wameweka signatures tu
 
Hakuna aliyeteuliwa na serekali ya CCM akabakisalama hata kama alikuwa na akili,mwenye huruma kama malaika lazima atakuwa nusu shetani.
 
Back
Top Bottom