Sheria ya gari kugonga treni imeshafutwa Ulaya

supersembe

Member
Aug 23, 2022
33
51
Majuzi imetokea ajali ya gari kugongana na kichwa cha treni hilo Singida. Lawama zote zikaelekezwa kwa dreva wa treni. Wenzetu Ulaya wametumia teknolojia tena ya bei rahisi kubadili mambo. Makutano yote ya barabara kuu na reli yamepewa vizuizi vya automatic, kufunga beria ya barabara, kupiga kengele na kuwasha taa nyekundu mara treni ikifika mita 100 kabla ya makutano.

Gharama husika kwa kila kizuizi ni usd 2000 sawa na sh. 5m. Tujiulize kwa nini TRC isinunue hiyo mitambo na kuokoa maisha ya watanzania. TRC imebaki na uzembe chini ya sheria iliyopitwa na wakati eti treni haigongi bali inagongwa.

Vipi SGR ikianza kazi, mfumo wa vivuko utatumia beria ya namna gani? Wabunge wetu paza sauti ili sheria zetu zibadilike na teknolojia.

Kila mkitembea Ulaya fanya utafiti, tutaokoa maisha ya watanzania.
 
Hizo order za USD sijui milion 5 jao hao majamaa jawataki hata kuzisikia maana humo change sasa inakuwaje
 
Tanzania wanunue kitu kitoke Nje ya Nchi hawawezi kuleta bill ndogo hivyo hizo Kilimo kwanza bei tunayopewa inazidi hata Range Rover Vellar ya 2023...
Kati ya Sheria ya kipuuzi hiyo ni moja wapo madereva wa Treni wanawasha moto mpaka kwenye vivuko vya magari kama vile Treni haina Speed ndogo...
Botswana walikua na sheria ya ukigonga Ng'ombe wewe uliegonga ndio unatakiwa kulipa Ng'ombe ila baadae wakaamua kuifuta na kuelekeza ng'ombe wote hawaruhusuwi kuwa bara barani kama ilivyokua hapo mwanzo sasa hivi ajali za kugonga ng'ombe zimepungua maana hawalipwi wao ndio wanatakiwa kumlipa mwenye gari...
 
Juzi hiyo hiyo pia vyombo vya habari vililiripoti gari ya mheshimiwa DC wa chamwino iliigonga treni eneo la Iyumbu mkoani Dodoma na kusababisha majeruhi. Kimsingi nadhani wakati Sheria ikitungwa, usafiri wa Treni ulikuwa ni moja ya tegemeo kuu kwa maeneo mengi ya nchi yetu na pia idadi ya magari/ vivuko vya barabara ilikuwa ni ndogo kulinganisha na sasa.

Zama zimebadilika. Sisi kama nchi hatuna budi kujielekeza katika KUTHAMINI UHAI kwa kuondoa Sheria zinazoweza kuchochea uzembe wa baadhi ya watendaji wa Shirika letu la Reli. Badala yake watakiwe kubuni mbinu za kuepusha matukio ya ajali za mara kwa mara kwenye vivuko.
 
Nchi gani?
Bunge gani?
Bunge hili hili mbunge anatuhumiwa tuhuma nzito mpaka anaondolewa uwaziri na bado ni mbunge?
Chama gani?
Hiki hiki wanateuwa Makonda?
Bro, ukiona alama ya reli punguza tu mwendo. Nobody cares about you but yourself.
 
Acha uongo

Umeandika ili kujistify kile unafikiria

Ni ulaya ipi hiyo makutano yote ya reli na barabara yamewekwa vizuizi?? Umekosea kutumia neno "maeneo yote" yapo maeneo mengi sana hayana vizuizi

Pia kuhusu gharama ya teknolojia ni mil 5, huu nao ni uongo mkubwa sana. Huwa mnaandika kujifurahisha au ni basi tu?

Mwisho kabisa, kwa dereva yoyote ni lazima kusimama kwenye makutano ya reli na barabara, narudia hii ni LAZIMA, treni iwe inapita au haipiti ni lazima usimame
Leo ukisema makutano yote ya reli na barabara yawekwe na vizuizi kesho utasema pia kwenye zebra zote pia waweke vizuizi.

Fuata sheria za barabarani, simama kwenye reli inapopita, simama kwenye zebra.

Ahsante
 
Nchi gani?
Bunge gani?
Bunge hili hili mbunge anatuhumiwa tuhuma nzito mpaka anaondolewa uwaziri na bado ni mbunge?
Chama gani?
Hiki hiki wanateuwa Makonda?
Bro, ukiona alama ya reli punguza tu mwendo. Nobody cares about you but yourself.
Maipende kulalamika, sheria zinataka usimame kwenye reli, hii ni lazima wala sio hiari
 
Majuzi imetokea ajali ya gari kugongana na kichwa cha treni hilo Singida. Lawama zote zikaelekezwa kwa dreva wa treni. Wenzetu Ulaya wametumia teknolojia tena ya bei rahisi kubadili mambo. Makutano yote ya barabara kuu na reli yamepewa vizuizi vya automatic, kufunga beria ya barabara, kupiga kengele na kuwasha taa nyekundu mara treni ikifika mita 100 kabla ya makutano.

Gharama husika kwa kila kizuizi ni usd 2000 sawa na sh. 5m. Tujiulize kwa nini TRC isinunue hiyo mitambo na kuokoa maisha ya watanzania. TRC imebaki na uzembe chini ya sheria iliyopitwa na wakati eti treni haigongi bali inagongwa.

Vipi SGR ikianza kazi, mfumo wa vivuko utatumia beria ya namna gani? Wabunge wetu paza sauti ili sheria zetu zibadilike na teknolojia.

Kila mkitembea Ulaya fanya utafiti, tutaokoa maisha ya watanzania.
Mbona hilo liliwahi kufanyika Dar es Dalaam kwenye makutano ya reli na mtaa wa Msimbazi, ila kizuizi kiligongwa sana. Tatizo la madereva wa tanzania ni wamezoea uongo, yaani wasipomuona askari watapita tu, hao bodaboda hupita pembeni ya kizuizi kama wafanyavyo kwenye taa.
 
Juzi hiyo hiyo pia vyombo vya habari vililiripoti gari ya mheshimiwa DC wa chamwino iliigonga treni eneo la Iyumbu mkoani Dodoma na kusababisha majeruhi. Kimsingi nadhani wakati Sheria ikitungwa, usafiri wa Treni ulikuwa ni moja ya tegemeo kuu kwa maeneo mengi ya nchi yetu na pia idadi ya magari/ vivuko vya barabara ilikuwa ni ndogo kulinganisha na sasa.

Zama zimebadilika. Sisi kama nchi hatuna budi kujielekeza katika KUTHAMINI UHAI kwa kuondoa Sheria zinazoweza kuchochea uzembe wa baadhi ya watendaji wa Shirika letu la Reli. Badala yake watakiwe kubuni mbinu za kuepusha matukio ya ajali za mara kwa mara kwenye vivuko.
Upo sahihi
 
Juzi hiyo hiyo pia vyombo vya habari vililiripoti gari ya mheshimiwa DC wa chamwino iliigonga treni eneo la Iyumbu mkoani Dodoma na kusababisha majeruhi. Kimsingi nadhani wakati Sheria ikitungwa, usafiri wa Treni ulikuwa ni moja ya tegemeo kuu kwa maeneo mengi ya nchi yetu na pia idadi ya magari/ vivuko vya barabara ilikuwa ni ndogo kulinganisha na sasa.

Zama zimebadilika. Sisi kama nchi hatuna budi kujielekeza katika KUTHAMINI UHAI kwa kuondoa Sheria zinazoweza kuchochea uzembe wa baadhi ya watendaji wa Shirika letu la Reli. Badala yake watakiwe kubuni mbinu za kuepusha matukio ya ajali za mara kwa mara kwenye vivuko.
Nimeona kule, lakini reply imefungwa, sijui shida imekuwa nini?
 
Back
Top Bottom