isajorsergio
Platinum Member
- Apr 22, 2018
- 4,125
- 6,250
Tuangazie sheria za mataifa mbalimbali kuhusiana na 'Ndege zisizokuwa na rubani' maarufu DRONES.
Teknolojia na matumzi ya ndege hizi inatazamiwa kupiga hatua mara mbili zaidi kwa miaka mitano ijayo, kutoka Trillioni 51.2 TZS (2020) Hadi Trillioni 102.3 TZS (2021). Matumzi makubwa yakiwa kibiashara, binafsi na kijeshi.
Kwa haraka tunaweza kuona Mmarekani mmoja kati ya saba amekwisha rusha ndege isiyokuwa na rubani. iFood inatumia drones kusambaza chakula jijini Campiñas, Brasil.
Nchini Ghana drones zinatumika kunyunyizia maeneo ya umma katika kipindi hiki cha COVID-19. Huku Israel ikiwa mzalishaji mkubwa na msabazaji wa drones kuelekea Amerika ya Kusini.
Ukraine drones zinatengenezwa kwa majaribio ya usafirishaji. Na New Zealand likiwa taifa la kwanza kusambaza chakula (Pizza delivery) mjini Whangaparaoa.
Mamlaka mbalimbali nchini Japan zinatoa mafunzo ya drones kukabiliana na matatizo mbalimbali ya kijamii.
Afrika ni taifa la Chad ambalo halina vizuizi katika matumizi ya ndege hizi. Huku Ghana urushaji wa drone bila kibali unaweza hukumiwa miaka 30 jela.
Rwanda inatumia drones kusambaza dawa na vifaa tiba, usambazaji uliokuwa unatumia masaa manne sasa ni dakika 20. Malawi likiwa taifa la kwanza Afrika kuwa na kituko cha mafunzo na uwezeshaji chenye lengo la matumizi ya drones kwa masuala ya kibinadamu.
Tanzania matumizi ya ndege hizi yakihitaji vibali na sheria zaidi zikiruhusu ndege hizi kuonekana wakati wa urushaji.
Ensenada, Mexico matumizi ya drone 1 yanawezesha kukumata waharifu 500 na kupunguza kiwango cha uharifu kwa asilimia 10%.
Takribani drones millioni 1.8 zilizosajiliwa Marekani, asilimia 71% ni matumizi binafsi na 29% matumizi ya kibiashara.
Hugo El Salvador inatumia drones kusambaza mahitaji mbalimbali nchini El Salvador. Cuba, Honduras na Belize matumizi ya ndege hizi yamepigwa marufuku.
China ni nyumbani kwa kampuni ya DJI mzalishaji na mmiliki wa mgawanyo wa nusu ya drones zote duniani.
Unatakiwa kuwa na miaka 20+ kuweza kuendesha drone yenye uzito wa kilo mbili nchini Indonesia.
Takribani rubani 5,870 ndio waliosajiliwa na mamlaka nchini Australia kuendesha drones.
Majaribio ya kwanza ya drone yalifanyika mwaka 1917 nchini Uingereza.
Iran ni marufuku kutumia drones, lakini ndio taifa la kwanza kutumia ndege hizi kijeshi. Kyrgyzstan, Uzbekistan, Syria, Iraq na Yemen drones ni marufuku.
Umoja wa Falme za Kiarabu umekuwa ukifanya majaribio ya ndege taxi.
Chile drones zinatumika kukagua maeneo ya maji na utoaji huduma ya dharura (Ugawaji life jackets) kwa watu walio maeneo hatarishi.
WaAmazonia wanatumia drones kufutilia uharifu dhidi ya mazingira na ukataji miti.
bit.ly/DronePrivacyLaws (Surfshark)
Teknolojia na matumzi ya ndege hizi inatazamiwa kupiga hatua mara mbili zaidi kwa miaka mitano ijayo, kutoka Trillioni 51.2 TZS (2020) Hadi Trillioni 102.3 TZS (2021). Matumzi makubwa yakiwa kibiashara, binafsi na kijeshi.
Kwa haraka tunaweza kuona Mmarekani mmoja kati ya saba amekwisha rusha ndege isiyokuwa na rubani. iFood inatumia drones kusambaza chakula jijini Campiñas, Brasil.
Nchini Ghana drones zinatumika kunyunyizia maeneo ya umma katika kipindi hiki cha COVID-19. Huku Israel ikiwa mzalishaji mkubwa na msabazaji wa drones kuelekea Amerika ya Kusini.
Ukraine drones zinatengenezwa kwa majaribio ya usafirishaji. Na New Zealand likiwa taifa la kwanza kusambaza chakula (Pizza delivery) mjini Whangaparaoa.
Mamlaka mbalimbali nchini Japan zinatoa mafunzo ya drones kukabiliana na matatizo mbalimbali ya kijamii.
Afrika ni taifa la Chad ambalo halina vizuizi katika matumizi ya ndege hizi. Huku Ghana urushaji wa drone bila kibali unaweza hukumiwa miaka 30 jela.
Rwanda inatumia drones kusambaza dawa na vifaa tiba, usambazaji uliokuwa unatumia masaa manne sasa ni dakika 20. Malawi likiwa taifa la kwanza Afrika kuwa na kituko cha mafunzo na uwezeshaji chenye lengo la matumizi ya drones kwa masuala ya kibinadamu.
Tanzania matumizi ya ndege hizi yakihitaji vibali na sheria zaidi zikiruhusu ndege hizi kuonekana wakati wa urushaji.
Takribani drones millioni 1.8 zilizosajiliwa Marekani, asilimia 71% ni matumizi binafsi na 29% matumizi ya kibiashara.
Hugo El Salvador inatumia drones kusambaza mahitaji mbalimbali nchini El Salvador. Cuba, Honduras na Belize matumizi ya ndege hizi yamepigwa marufuku.
Unatakiwa kuwa na miaka 20+ kuweza kuendesha drone yenye uzito wa kilo mbili nchini Indonesia.
Takribani rubani 5,870 ndio waliosajiliwa na mamlaka nchini Australia kuendesha drones.
Iran ni marufuku kutumia drones, lakini ndio taifa la kwanza kutumia ndege hizi kijeshi. Kyrgyzstan, Uzbekistan, Syria, Iraq na Yemen drones ni marufuku.
Umoja wa Falme za Kiarabu umekuwa ukifanya majaribio ya ndege taxi.
Chile drones zinatumika kukagua maeneo ya maji na utoaji huduma ya dharura (Ugawaji life jackets) kwa watu walio maeneo hatarishi.
WaAmazonia wanatumia drones kufutilia uharifu dhidi ya mazingira na ukataji miti.
bit.ly/DronePrivacyLaws (Surfshark)