Nina mshikaji wangu huu mwaka wa tano anateseka kudai mtoto wake bila mafanikio. Stori ilikuwa hivi:
Yeye kaoana na mmarekani walikutana alipoenda huko kimasomo, bahati mbaya mkewe aligundulika ana matatizo ya uzazi hivyo hataweza kupata nae mtoto. Jamaa anapenda sana kuwa na watoto au walau mmoja. Wakaelewana na mkewe akaja bongo akamzalisha mwanamke mmoja ili baadae amchukue mwanae wakaishi nae marekani. Hii ishu mama mzazi wa mtoto aliijua kwamba anamsaidia jamaa kuzaa then mkataba unaishia hapo, lakini cha kushangaza baada ya kuzaa kambadilikia jamaa na hataki kumpa mwanae. Huu ni mwaka wa tano wanahangaika mama anawapiga tarehe. Amewageuza kitega uchumi kwa kupitia mgongo wa mtoto kwani matumizi anayodai ni makubwa sana kiasi kwamba jamaa anaelemewa kutuma pesa za matumizi kila mwezi wakati angeweza kuishi na mwanae marekani freely. Yeye na mkewe wamechanganyikiwa hawajui wafanyeje.
Kuna sheria yoyote itakayomsaidia mshkaji wangu na mkewe wa ndoa kumpata mtoto huyu. Ni kavulana kazuri na kamefanana sana na baba yake.
Thanx wakuu.
Yeye kaoana na mmarekani walikutana alipoenda huko kimasomo, bahati mbaya mkewe aligundulika ana matatizo ya uzazi hivyo hataweza kupata nae mtoto. Jamaa anapenda sana kuwa na watoto au walau mmoja. Wakaelewana na mkewe akaja bongo akamzalisha mwanamke mmoja ili baadae amchukue mwanae wakaishi nae marekani. Hii ishu mama mzazi wa mtoto aliijua kwamba anamsaidia jamaa kuzaa then mkataba unaishia hapo, lakini cha kushangaza baada ya kuzaa kambadilikia jamaa na hataki kumpa mwanae. Huu ni mwaka wa tano wanahangaika mama anawapiga tarehe. Amewageuza kitega uchumi kwa kupitia mgongo wa mtoto kwani matumizi anayodai ni makubwa sana kiasi kwamba jamaa anaelemewa kutuma pesa za matumizi kila mwezi wakati angeweza kuishi na mwanae marekani freely. Yeye na mkewe wamechanganyikiwa hawajui wafanyeje.
Kuna sheria yoyote itakayomsaidia mshkaji wangu na mkewe wa ndoa kumpata mtoto huyu. Ni kavulana kazuri na kamefanana sana na baba yake.
Thanx wakuu.