Sheria hutambua ndoa halali ni ile iliyofanyiwa sherehe tu!

sulphadoxine

JF-Expert Member
Nov 1, 2010
2,257
645
KATIKA jamii ya makabila mengi ya Kiafrika kumekuwepo mtazamo kwamba mwanaume akishalipa mahari kwa ajili ya kumuoa mwanamke fulani hata kama yeye mwenyewe hana habari au hapendi, atapaswa akubali na kwamba hiyo itakuwa ni ndoa halali.

Kutokana na mtazamo huo, wamekuwa wakijitokeza wajanja wachache katika jamii au makabila hayo, hasa wazazi, kuamua kupeana mahari bila vijana wao kujua au mtu mzima kuamua kutoa mahari ili kumuoa binti yeyote bila hata binti mwenyewe kujua.

Pengine suala hilo ndilo limefanya kuwepo kwa tabia ya watoto wadogo wa kike kuolewa bila hata wenyewe kujua. Inashangaza kuna kabila hapa nchini ambapo mwanamme mtu mzima eti anaweza akafanya “booking” ya ujauzito ikiwa mama mhusika atajifungua mtoto wa kike. Mwanaume huyo anaweza kulipa kabisa mahari.

Yawezekana mtazamo huo bado upo, ingawa kwa uchunguzi wangu hivi sasa umepungua kutokana na ndoa za kimila kuwa chache na badala yake ndoa nyingi kufungwa kidini na kiserikali ambapo, ahadi za ndoa lazima zitolewe mbele ya watu ambao walishatangaziwa kuwepo kwa tukio hilo ikiwemo kualikwa katika sherehe ili wawe mashahidi.

Ni kutokana na hali hiyo, Sheria ya Ndoa ya Mwaka 1971, inasisitiza kwamba ndoa halali lazima ishuhudiwe na watu walao wawili ambao sio pamoja na yule anayefungisha ndoa hiyo. Ushuhuda huo ndio unaotambulika kuwepo kwa sherehe ya ndoa ambayo kwa kawaida yaweza kuendelea miongoni mwa ndugu na jamaa katika kumbi mbali mbali.

Kwa hiyo ikitokea utata katika kuwepo kwa ndoa kinachoangaliwa sio cheti tu cha ndoa kama ambavyo hivi sasa imezoeleka, bali pia upande usiotambua kuwepo kwa ndoa unaweza ukasema kwamba hakukuwa na watu walioshuhudia ndoa husika kufungwa au kisheria ni kwamba hakukuwa na “sherehe ya ndoa”.
 
Hata kigezo cha kutoa mahari hata ikiwa ni ya kiasi gani na pengine hata kama ni kwa makubaliano ya wazazi wa pande mbili husika au mtoa mahari na mzazi wa binti au mwanamke anayeolewa, haina nguvu kisheria. Viapo vya ndoa kanisani au msikitini lazima viendane na sherehe yake ambapomuhimu zaidi ni kuwepo kwa mashahidi.

Msimamo huo umewekwa umesisitizwa kisheria katika uamuzi wa Rufani ya Shauri la Rufani Namba 49 la Mwaka 1983 (Mahakama Kuu, Dodoma) lililoamuliwa na Jaji William Maina mnamo 11 Februari 1984 lililowahusu Ramadhani Ramadhani na Sundi Andalu. Kulikuwa na maelezo mahakamani kwamba mrufani (Bw. Ramadhani) awali alimshtaki mjibu rufani (Bw. Andalu) katika Mahakama ya Mwanzo ya Ilongero huko Dodoma.

Madai ya mrufani ambaye katika mahakama ya chini alikuwa ni mlalamikaji yalikuwa ni kwamba alikuwa ameshamlipa mjibu rufani mahari, ng'ombe watatu, ili kuoa binti yake. Kwamba binti mhusika baadae aliolewa na mtu mwingine wakati ndoa ya awali na mrufani ikiwepo. Binti huyo alidaiwa kuolewa tena kwa Bw. Alute.

Katika mahakama ya mwanzo mlalamikaji aliomba alipwe fidia na mlalamikiwa. Mahakama ikakubali ikitambua kwambandoa ilikuwepo kwa mahari iliyolipwa. Mlalamikiwa (Bw. Andalu) akakata rufaa katika Mahakama ya Wilaya ambako akashinda.

Hakimu wa Mahakama ya Wilaya alisema kwamba hakuona kama kulikuwa na ndoa kati ya Bw. Ramadhani na Bi. Zainabu. Kwamba Bwa. Andalu alikuwa sahihi kumuoza binti yake kwa mwanamume mwingine.

Bw. Ramadhani hakuridhika na uamuzi wa Mahakama ya Wilaya ndipo akakata rufaa Mahakama Kuu. Suala lililojadiliwa kisheria mbele ya Jaji Maina lilikuwa kama ni kweli ndoa ilikuwepo kati ya Bw. Ramadhani na Zainabu. Kwa vile hakukuwa na cheti cha ndoa, mrufani alidai kwamba alimuoa Zainabu mwaka 1973 chini ya utaratibu wa kimila na akawa amelipa mahari.

Mjibu rufani, Bw. Andalu akapinga kuwepo kwa ndoa yoyote kati ya mrufani na binti yake. Mjibu rufani akasema mrufani alichokifanya awali ni kumchukua binti yake na kwenda naye huko Arusha bila yeye kutaarifiwa.
 
kwa uelewa wa layman, ukimwambia sherehe anafikiri ni ile cherekochereko pilau kuku ndizi viazi minyama na disco siku ya ndoa......si dhani kama sherehe ni lazima...wanaposema marriage contract must be celebrated, wanamaana kuwa wanaohitajika ni mashahidi au wasimamizi wa ndoa ambao bila hao ndoa haiwezi kufungwa. chukua mfano unapoenda kanisani kufunga ndoa, mchungaji au padre amekuwa delegated na authority ya kufungisha ndoa kwa niaba ya Msajili mkuu wa ndoa wa kuleeee RITA...sijui wanamuita Administrator General au nani nimesahau....anapofungisha ndoa hiyo, hafungishi ndoa hiyo yeye kama mtumishi wa dini, anakuwa amevaaa joho la mtumishi wa selikali, mtumishi wa Mungu anakuwa amepewa power kufungisha kwaniaba tu ya msajili mkuu, na kitu hicho. cha kuelewa ni kwamba, celebration of marriage kwa minajiri ya taratibu za dini si muhimu sana, cha muhimu ni kwamba ndoa ilitangazwa, hakukuwa na objection kwa siku 21, kuna mashahidi, wanandoa hawajawahi kuwa na ndoa kabla, wanandoa wanao uwezo walau kufanya tendo la ndoa mara moja baada ya kujaza mkataba wa ndoa, hakuna mazingira yeyote yanayoweza kuifanya ile ndoa iwe "voidable" ....hapa simaanishi void,.....ikiwa na maana, ndoa inayotangulika na kufanywa kama haikuwepo kabisa...etc. yakitimia hayo tu, ndoa imeshafungwa, na meaning ya celebration ndio hii.

zaidi ya hayo, iwe ndoa ya bomani kwa mkuu wa wilaya, iwe msikitini, kanisani etc, au iwe ni ile ya customary ambayo walikuja kuisajili kule RITA baada ya taratibu zao za kimila etc, ndoa zote hizo zina status sawasawa kabisa, hakuna bora zaidi wala yenye hadhi tofauti na zingine....kupeleka kanisani au msikitini huo ni urembo tu...ndio maana hata ndoa ya watu wa kijijini walioooana kimila, wanalazimishwa na sheria kusajili ile ndoa kwa msajili mkuu, na wakishafanya hivyo tu watakuwa wamepata cheti cha ndoa. mpoooooooooo!
 
Back
Top Bottom