Shellukindo: Dk. Rashid ni mtovu wa nidhamu

Ngongo

JF-Expert Member
Sep 20, 2008
18,921
31,161
MWENYEKITI wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, William Shellukindo ameitafsiri hatua ya mkurugenzi mkuu wa Shirika la Umeme(Tanesco), Dk. Idrissa Rashid kutangaza kuachana na mpango wa kununua mitambo ya kuzalisha umeme wa dharura ya kampuni ya Dowans kuwa ni kukosa nidhamu kwa kuwa ameingilia mamlaka ya waziri husika.


Akizungumza na Mwananchi jana jijini Dar es Salaam, Shellukindo alisema: "Kitendo cha Dk. Rashid kutangaza kwamba nchi itaingia gizani na Tanesco isilaumiwe, ni utovu wa nidhamu kwa sababu haikuwa kazi yake kutangaza hilo, bali kazi ya Waziri wa Nishati na Madini.


"Tena hakupaswa kabisa kutoa kauli hiyo. Yeye ni mtendaji tu wa shirika la Umma... hana mamlaka ya kutangaza kwamba nchi itaingia gizani kwa kuwa hiyo ni kazi ya Waziri mwenye dhamana na Nishati na Madini."


Alisema Dk. Rashid anawajibika kwa waziri na kwamba chochote anachohitaji kufanya kuhusu masuala ya umeme kama tatizo hilo, ni lazima awasiliane na waziri husika, na si kwa matakwa yake.


Alisema kuwa Dk. Rashid alipaswa kupeleka taarifa kwa waziri juu ya uamuzi huo na waziri ndiye aliyestahili kutangaza hatua hiyo badala ya mkurugenzi huyo wa Tanesco na kuongeza kuwa katika kikao kijacho cha Bunge, kamati yake itamuita Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja ili atoe maelezo kwa kamati kama walikubaliana na Dk.Rashid kabla ya kutoa tamko hilo.


"Yawezekana alikubaliana na Dk. Rashid na kama ni hivyo basi aseme hivyo," Shellukindo alifafanua.


"Hata Waziri mwenyewe hana mamlaka ya kutoa kauli kama hiyo bila ya kuwasiliana na kupata ushauri wa Baraza la Mawaziri. Sasa je yeye Dk. Rashid alipata wapi mamlaka hayo," alihoji Shellukindo.


Alisema baada ya Dk. Rashid kutangaza Tanesco imejitoa katika suala la ununuzi wa mitambo hiyo, alipaswa kupeleka taarifa wizarani ili wizara iangalie hatua za kufanya, lakini kutokana na utovu wa nidhamu alionao, aliamua kutoa kauli mbaya na yenye kuwapa wananchi mfadhaiko.


Shellukindo pia alisema kauli hiyo ya Dk. Rashid inaweza kuwachonganisha wananchi na wabunge endapo nchi itaingia gizani na kwamba ukweli wa mambo hayo utajulikana baada ya kamati yake kukutana na waziri katika vikao vya mwezi ujao.


"Kamati yangu ndiyo yenye mamlaka ya kukutana na waziri, hata tunapomwita kwenye kamati, anaweza kuongozana na watu wa Tanesco lakini waziri ndiye mzungumzaji mkuu," alisema Shellukindo ambaye amekuwa na msimamo mkali katika sakata la ununuzi wa mitambo ya Dowans.


"Kutokana na hali hiyo hata Kamati ya Hesabu ya Kudumu ya Mashirika ya Umma bado haina mamlaka ya kukutana na waziri moja kwa moja kwa sababu, wao wanahusika na hesabu za mashirika ya ndani na wana mamlaka ya kukutana na Tanesco tu na kuhoji chochote kuhusiana na hesabu za shirika hilo na si waziri," aliongeza Shellukindo.


Kauli ya mwenyekiti huyo imekuja siku nne baada ya Dk. Rashid kutangaza kujitoa rasmi katika sakata la ununuzi wa mitambo ya kufua umeme wa dharura ya kampuni ya Dowans Tanzania Limited iliyorithi mkataba kutoka kampuni hewa ya Richmond Development LLC.


Mbali na Dk Rashidi kutangaza kujitoa, alisema yeye na Tanesco wasije kulaumiwa pale inchi itakapokuwa giza na hospitali, viwanda pamoja na vyuo vikishindwa kutoa huduma nchini.


Kauli hiyo ya Shellukindo ilitanguliwa na kauli za wananchi wa kada mbalimbali wakiwemo wasomi na wanasiasa waliomtaka Mkurugenzi huyo Mtendaji wa Tanesco ajiuzuru wadhifa alionao kutokana na kauli yake hiyo.


Katika maoni yao wananchi hao walisema Dk Rashid alikuwa na kazi ya kuandaa mpango wa muda mfupi na mrefu, ili kuweka uhai na ufanisi ndani ya shirika hilo kwa sababu ni shirika pekee linalotegemewa na wananchi wote, lakini ameshindwa kazi yake.

Source:Mwananchi
 
Dr Rashid.

It Seems you have something to answer here!

All is not going in your way!!

Anything which took place is not yet clear in the public you want to lets know ....to clear this mess!!??

Karibu... tunakusikiliza!!!
 
Unajua watanzania tuna matatizo sana. Yani badala kuzungumzia ni jinsi gani tunaweza kupambana na tatizo hili la umeme, tunazungumzia kwani hilo tamko hakulitoa waziri.

Hivi swala ni nchi kuwa gizani au ni nani anayetakiwa kutamka nchi itakuwa gizani?
 
Ushaona mtoto akitangaza ndoa ya wazazi wake? Mimi sijui degree yake ya falsafa inamsaidiaje Dr Idris, amechemka kwa kastatement kake kalikojaa hasira. Anatishia watanzania kuingia gizani wakati 10% tu ndio wanaonufaika moja kwa moja na kaumeme ka Tanesco. Mitambo ya Dowans sio alfa na omega, alipaswa kutoa mbadala wa Dowans na sio kususia kabisa, kama ameshindwa kazi ajiuzuru wengine wafanye kazi, asitikise kiberiti
 
Taaluma ya manunuzi ya umma bado kueleweka katika wabongo wengi hata pamoja na wabunge wenyewe na pamoja na Shelukindo. Katika sababu zilizofanya hata na ED kupigwa chini ni pamoja na kusema sheria ya manunuzi hakifuatwa na nukuu inasema Tanesco ni PE (Procurement Entity) na lazima iwe huru kufanya maamuzi ya manunuzi si kama ilivyoingiliwa na serikali (Waziri) katika kufanya manunuzi ya kununua mitambo ya Richmond na watu tayari wamewajibika.

Sasa leo Shelukindo anakataa kwamba Tanesco sio PE na msemaji wa mwisho ni Waziri. Wakati mwingine siasa na chuki zinatufanya tupoteze integrity ya kufikiri hata kwa vitu vya kawaida, ikumbukwe hata procurement audit report ya Tanesco iliwekwa humu tukaisoma na wakaguzi walionyesha ni namna gani wizara inaingilia katika maamuzi.

Sheria ya manunuzi inasema notification of award ifanywe na mkuu wa PE na Idrisa kwa capacity yake ni mkuu wa PE na sheria ina mruhusu kusema kuhusu PE pamoja mchakato wa manunuzi yeye ni sehemu ya kwanza ya appeal ya process. Labda kama kuna ambalo tunataka atoke basi tuliseme kuliko kutafuta sababu wakati sheria ya manunuzi haimtaji waziri wa nishati katika structure ya manunuzi ya Tanesco.

Kama waziri anasauti sasa hivi kwanini wa mwanzo waliwajibishwa! Si sawa kuwachia wanasiasa wafanye maamuzi technical, wengi wao si wajuzi wa hayo mambo na hawana uzoefu wowote kikubwa zaidi wameshatuumiza sana katika maamuzi yao mashirika waachiwe board husika. Kama Idrisa hafai basi hafai sio kuingiza waziri wakati wajuzi wa mambo ya umeme wako Tanesco.
 
Kamati ya Ulinzi ya Bunge kumkaanga Dk. Rashid

2009-03-10 11:03:26
Na Waandishi Wetu


Kauli ya Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Nchini (Tanesco), Dk. Idris Rashid, kwamba nchi itagubikwa na kiza katika siku za usoni kutokana na kukosekana umeme, imeanza kumgeuka na sasa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama imeeleza kwamba, itamwita ili kumhoji kuhusu kauli hiyo.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Wilson Masilingi, alisema wamefikia hatua hiyo kwa vile umeme ni suala nyeti linalogusa moja kwa moja usalama wa nchi, hivyo hawawezi kuacha kauli nzito kama hiyo ya Dk. Rashid ipite hivi hivi bila kufanyiwa kazi.

Masilingi ambaye pia ni Mbunge wa Muleba Kusini (CCM), alisema hayo alipozungumza na Nipashe jana.

``Nitaita kamati yangu kujadili kauli yake (Dk. Rashid) kisha baadaye tutamwita ili tumhoji, kwani umeme ni usalama wa nchi,`` alisema Masilingi.

Alisema bosi huyo wa Tanesco hana mamlaka ya kutoa kauli kama hiyo na kwa vile kamati yake inashughulika na masuala ya ulinzi na usalama wa nchi, wanachelea kuwajibika endapo hujuma yoyote inaweza kufanywa kutokana na kauli hiyo.

Ijumaa wiki iliyopita, Dk. Rashid aliitisha mkutano na waandishi wa habari na katika jumla ya maelezo yake, alidiriki kutamka kwamba: ``Wananchi wa Tanzania watafanya maamuzi yao hapo ambapo nchi itakuwa imegubikwa na kiza, mahospitali hayatoi huduma, viwanda havizalishi, wanafunzi vyuoni wanashindwa kusoma kwa sababu tulishindwa kufanya maamuzi.``

Kauli hiyo aliitoa alipokuwa akitangaza uamuzi wa Tanesco kufuta nia yake ya kununua mitambo ya kufua umeme ya kampuni ya Dowans na kueleza kwamba upotoshaji wa kisiasa kuwa chanzo cha kufikia uamuzi huo.

Dk. Rashid alisema hali ya ukuaji wa uchumi nchini inafanya ongezeko la mahitaji ya umeme kwa kiwango cha megawati 75 kila mwaka, kwa sasa kuna nakisi ya megawati 150 na kama hali hiyo ikiendelea bila kuwapo na uzalishaji wa ziada, nakisi itakuwa megawati 225 ifikapo Desemba mwaka huu.

Wakati hayo yakijiri, Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Francis Kiwanga, alisema jana kuwa kama itafikia nchi kuingia kiza, basi menejimenti na Bodi ya Wakurugenzi wa Tanesco watapaswa wote kuwajibika.

Kiwanga alisema watawajibika kwa vile tishio la ukosefu wa umeme lilijulikana muda mrefu na hakuna hatua za makusudi zilizochukuliwa kudhibiti hali hiyo.

Kuhusu menejimenti ya Tanesco kupuuza maagizo ya Bodi, Kiwanga alisema wajumbe wa Bodi walitakiwa wachukue hatua mapema na si kulalamika hivi sasa.

Alisema kinachosababisha hali hiyo, ni muingiliano wa kiutendaji kati ya Ikulu na Bodi ya Wakurugenzi wa Tanesco.

``Kwani Dk. Rashid si mara ya kwanza kwenda kinyume na Bodi. Mara ya kwanza alishindwa kazi akataka kujiuzulu, Ikulu ikaingilia kati na kujenga mazingira ya yeye kutowajibika,`` alisema Kiwanga.

Naye Rashid alipotafutwa na Nipashe kuzunguzia hatua hizi mpya zinazolengwa kwake, alisema amefunga mjadala wa kuzungumzia sakata la ununuzi wa mitambo ya Dowans.

Akizungumza na Nipashe kwa njia ya simu jana, Mkurugenzi huyo alisema hivi sasa hataki kabisa kuzungumza na waandishi wa habari.

``Sitaki kuzungumza na waandishi wa habari sasa, nilishafunga mjadala huo,``alisema.

Dk. Rashidi alimtaka mwandishi, iwapo ana jambo lingine lisilohusiana na Dowans awasiliana na Idara ya Mawasiliano ya Tanesco ili apatiwe ufafanuzi.

Hata hivyo, alipoulizwa kwamba haoni kuwa madai ya yeye kukosa nidhamu yaliyotolewa na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, William Shellukindo, yanamgusa yeye binafsi, Mkurugenzi huyo alionekana kukasirirka.

``Kama ni langu binafsi basi ni mimi binafsi, nimekataa kuzungumza, siongei na waandishi mimi, nenda idara ya mawasiliano,`` alisema na kukata simu.

Chimbuko la Dowans ni mkataba wa mradi wa ufuaji wa umeme wa dharura wa megawati 100 kati ya serikali/Tanesco na Kampuni ya Richmond uliofikiwa mwaka 2006. Richmond baada ya kushindwa kuutekeleza mradi huo iliuuza kwa Dowans.

Mkataba wa Richmond ulizua mvutano kiasi cha kusababisha Bunge kuunda Kamati Teule kuchunguza ikiongozwa na Mbunge wa Kyela, Dk. Harrison Mwakyembe, ripoti yake ilimfanya Waziri Mkuu, Edward Lowassa, ajiuzulu.

Pia mawaziri Nazir Karamagi (Nishati na Madini) na Dk. Ibrahim Msabaha (Ushirikiano wa Afrika Mashariki) nao walijiuzulu kwa kashfa hiyo.

Katika maazimio ya Bunge yaliyofikiwa baada ya kuwasilishwa kwa taarifa ya Kamati ni kuvunjwa kwa mkataba wa Richmond ambao ulikuwa umeuzwa kwa Dowans.

Dowans imefungua kesi mahakama ya ushuluhishi mjini Paris na Tanesco nayo imefungua kesi Mahakama ya Biashara kuomba Dowans isihamishe mitambo yake kutokana na kesi iliyoko Paris.

Mapema wiki iliyopita, Spika wa Bunge, Samuel Sitta, aliitaka serikali kuepuka na nia ya kutaka kununua mitambo ya Dowans ambayo amesisitiza kuwa ni michakavu.

Sitta alisema kununua mitambo hiyo kutaibua upya sakata la kampuni ya kufua umeme wa dharura iliyoibua utata ya Richmond Development LCC ya Marekani.

Alisema hakuna sababu ya kununua mitambo hiyo kwa Sh. bilioni 90 kwani fedha hizo zinatosha kabisa kununua mitambo mipya ambayo inapatikana kirahisi sehemu mbalimbali duniani.

Aidha, alisema haiingii akilini serikali kung`ang`ania kununua mitambo ya Dowans ambayo tayari imelishitaki Tanesco kwenye Baraza la Kimataifa la Usuluhishi huko Paris, Ufaransa na kwamba mitambo hiyo ni sehemu ya kufunguliwa kwa kesi hiyo.

SOURCE: Nipashe
 
Dr Idrisa kwa mara ya pili nakuomba andika barua ya kujiuzuru kwa mh Rais wa jamhuri ya muungano ya Tanzania.
Kama huwezi sema nikusaidie kui draft. Wananchi wa danganyika hawajakuelewa na hawatakuelewa.
 
Dr Idrisa kwa mara ya pili nakuomba andika barua ya kujiuzuru kwa mh Rais wa jamhuri ya muungano ya Tanzania.
Kama huwezi sema nikusaidie kui draft. Wananchi wa danganyika hawajakuelewa na hawatakuelewa.

Presidential appointees wanapofanya makosa na wanapojifanya wao ni wasemaji wa serikali responsibility inakuwa mikononi mwa anayemteua. Rais anaonesha weakness kwa kuruhusu kila mtu kuwa msemaji wa serikali, na anaonesha weakness zaidi kwa kushindwa kumwajibisha Dr Rashid. Inaonekana kuna jambo analoliogopa.
 
Tanzania tutafika kweli? ikiwa boss wa Tanesco hana mamlaka ya kuongelea kupatikana au kukosekana kwa umeme ni hatari hii.

Ndio maaana, miaka karibia hamsini ya uhuru umeme wa matatizo, kumbe hata boss wa umeme hauruhusiwi kuongelea upatikanaji au ukosekanaji wa umeme wake. Duhhh, makubwa haya jamani, hawa watunga sheria tunawatowa wapi hawa jamani? hawa ndio hawa hawa tunaowachaguwa kututetea na kutuwekea mambo sawa? Ndio maana wengi wao utawakuta wanalala sehemu nyeti kama kwenye vikao vya bunge, wakiamka wanakurupuka tu na mambo waliyo yaota kwenye ukumbi wa bunge na si waliyoyasikia au kuyafanyia kazi kwa kina. Wananishangaza sana! Leo wanasema boss wa umeme hafai kuongelea mambo ya umeme? Nashangaa, nashangaa, nashangaa!
 
kamati ya ulinzi ya bunge kumkaanga dk. Rashid

2009-03-10 11:03:26
na waandishi wetu


kauli ya mkurugenzi mtendaji wa shirika la umeme nchini (tanesco), dk. Idris rashid, kwamba nchi itagubikwa na kiza katika siku za usoni kutokana na kukosekana umeme, imeanza kumgeuka na sasa kamati ya bunge ya mambo ya nje, ulinzi na usalama imeeleza kwamba, itamwita ili kumhoji kuhusu kauli hiyo.

Mwenyekiti wa kamati hiyo, wilson masilingi, alisema wamefikia hatua hiyo kwa vile umeme ni suala nyeti linalogusa moja kwa moja usalama wa nchi, hivyo hawawezi kuacha kauli nzito kama hiyo ya dk. Rashid ipite hivi hivi bila kufanyiwa kazi.

Masilingi ambaye pia ni mbunge wa muleba kusini (ccm), alisema hayo alipozungumza na nipashe jana.

``nitaita kamati yangu kujadili kauli yake (dk. Rashid) kisha baadaye tutamwita ili tumhoji, kwani umeme ni usalama wa nchi,`` alisema masilingi.

Alisema bosi huyo wa tanesco hana mamlaka ya kutoa kauli kama hiyo na kwa vile kamati yake inashughulika na masuala ya ulinzi na usalama wa nchi, wanachelea kuwajibika endapo hujuma yoyote inaweza kufanywa kutokana na kauli hiyo.

Ijumaa wiki iliyopita, dk. Rashid aliitisha mkutano na waandishi wa habari na katika jumla ya maelezo yake, alidiriki kutamka kwamba: ``wananchi wa tanzania watafanya maamuzi yao hapo ambapo nchi itakuwa imegubikwa na kiza, mahospitali hayatoi huduma, viwanda havizalishi, wanafunzi vyuoni wanashindwa kusoma kwa sababu tulishindwa kufanya maamuzi.``

kauli hiyo aliitoa alipokuwa akitangaza uamuzi wa tanesco kufuta nia yake ya kununua mitambo ya kufua umeme ya kampuni ya dowans na kueleza kwamba upotoshaji wa kisiasa kuwa chanzo cha kufikia uamuzi huo.

Dk. Rashid alisema hali ya ukuaji wa uchumi nchini inafanya ongezeko la mahitaji ya umeme kwa kiwango cha megawati 75 kila mwaka, kwa sasa kuna nakisi ya megawati 150 na kama hali hiyo ikiendelea bila kuwapo na uzalishaji wa ziada, nakisi itakuwa megawati 225 ifikapo desemba mwaka huu.

Wakati hayo yakijiri, mkurugenzi mtendaji wa kituo cha sheria na haki za binadamu (lhrc), francis kiwanga, alisema jana kuwa kama itafikia nchi kuingia kiza, basi menejimenti na bodi ya wakurugenzi wa tanesco watapaswa wote kuwajibika.

Kiwanga alisema watawajibika kwa vile tishio la ukosefu wa umeme lilijulikana muda mrefu na hakuna hatua za makusudi zilizochukuliwa kudhibiti hali hiyo.

Kuhusu menejimenti ya tanesco kupuuza maagizo ya bodi, kiwanga alisema wajumbe wa bodi walitakiwa wachukue hatua mapema na si kulalamika hivi sasa.

Alisema kinachosababisha hali hiyo, ni muingiliano wa kiutendaji kati ya ikulu na bodi ya wakurugenzi wa tanesco.

``kwani dk. Rashid si mara ya kwanza kwenda kinyume na bodi. Mara ya kwanza alishindwa kazi akataka kujiuzulu, ikulu ikaingilia kati na kujenga mazingira ya yeye kutowajibika,`` alisema kiwanga.

Naye rashid alipotafutwa na nipashe kuzunguzia hatua hizi mpya zinazolengwa kwake, alisema amefunga mjadala wa kuzungumzia sakata la ununuzi wa mitambo ya dowans.

Akizungumza na nipashe kwa njia ya simu jana, mkurugenzi huyo alisema hivi sasa hataki kabisa kuzungumza na waandishi wa habari.

``sitaki kuzungumza na waandishi wa habari sasa, nilishafunga mjadala huo,``alisema.

Dk. Rashidi alimtaka mwandishi, iwapo ana jambo lingine lisilohusiana na dowans awasiliana na idara ya mawasiliano ya tanesco ili apatiwe ufafanuzi.

Hata hivyo, alipoulizwa kwamba haoni kuwa madai ya yeye kukosa nidhamu yaliyotolewa na mwenyekiti wa kamati ya bunge ya nishati na madini, william shellukindo, yanamgusa yeye binafsi, mkurugenzi huyo alionekana kukasirirka.

``kama ni langu binafsi basi ni mimi binafsi, nimekataa kuzungumza, siongei na waandishi mimi, nenda idara ya mawasiliano,`` alisema na kukata simu.

Chimbuko la dowans ni mkataba wa mradi wa ufuaji wa umeme wa dharura wa megawati 100 kati ya serikali/tanesco na kampuni ya richmond uliofikiwa mwaka 2006. Richmond baada ya kushindwa kuutekeleza mradi huo iliuuza kwa dowans.

Mkataba wa richmond ulizua mvutano kiasi cha kusababisha bunge kuunda kamati teule kuchunguza ikiongozwa na mbunge wa kyela, dk. Harrison mwakyembe, ripoti yake ilimfanya waziri mkuu, edward lowassa, ajiuzulu.

Pia mawaziri nazir karamagi (nishati na madini) na dk. Ibrahim msabaha (ushirikiano wa afrika mashariki) nao walijiuzulu kwa kashfa hiyo.

Katika maazimio ya bunge yaliyofikiwa baada ya kuwasilishwa kwa taarifa ya kamati ni kuvunjwa kwa mkataba wa richmond ambao ulikuwa umeuzwa kwa dowans.

Dowans imefungua kesi mahakama ya ushuluhishi mjini paris na tanesco nayo imefungua kesi mahakama ya biashara kuomba dowans isihamishe mitambo yake kutokana na kesi iliyoko paris.

Mapema wiki iliyopita, spika wa bunge, samuel sitta, aliitaka serikali kuepuka na nia ya kutaka kununua mitambo ya dowans ambayo amesisitiza kuwa ni michakavu.

Sitta alisema kununua mitambo hiyo kutaibua upya sakata la kampuni ya kufua umeme wa dharura iliyoibua utata ya richmond development lcc ya marekani.

Alisema hakuna sababu ya kununua mitambo hiyo kwa sh. Bilioni 90 kwani fedha hizo zinatosha kabisa kununua mitambo mipya ambayo inapatikana kirahisi sehemu mbalimbali duniani.

Aidha, alisema haiingii akilini serikali kung`ang`ania kununua mitambo ya dowans ambayo tayari imelishitaki tanesco kwenye baraza la kimataifa la usuluhishi huko paris, ufaransa na kwamba mitambo hiyo ni sehemu ya kufunguliwa kwa kesi hiyo.

Source: Nipashe
shelukindo + mwakyembe = wapenda sifa na umaarufu wa kudakiaaaa....

Hawana jipya bali kuendeleza kasi na nguvu ya kuturudisha nyumaaa zaidiiiiiii
 
Back
Top Bottom