OgwaluMapesa
JF-Expert Member
- May 24, 2008
- 10,942
- 428
LICHA ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na serikali yake kumkana, Mnajimu maarufu nchini, Sheikh Yahya Hussein, ameibuka na kusema kwamba hahitaji kibali katika kumwekea "ulinzi wa majini" mtu anayempenda - Rais Jakaya Kikwete.
Akizungumzia kauli za viongozi wa CCM na Serikali kwamba hawatambui "ulinzi wa majini" aliosema atautoa kwa Kikwete, Sheikh Yahya, amesema: "Sihitaji kibali cha yeyote kumuwekea rais wangu ulinzi wa majini."
Sheikh Yahya, ambaye amekuwa akitoa kauli tata kuhusiana na Kikwete hata kabla ya kampeni kuanza, alisema, jana, jijini, kuwa anachozungumzia yeye si uchawi wala ushirikina; bali ni mambo ambayo yapo na hayakwepeki.
"Kila mtu anazaliwa na jini. Hata Slaa (Dk.Willibrod Slaa, Mgombea urais wa CHADEMA) ana jini anaitwa Subiani. Nakwambia sihitaji kumshirikisha mtu katika hili," alisema Sheikh Yahya Hussein na kumkabidhi simu mwanae aliyejitambulisha kwa jina la Hassan, ambaye naye alisema;
"Sheikh alisema binafsi hahitaji kumshirikisha mtu katika hili. Serikali iendelee na ulinzi wake na yeye atatoa ulinzi wake. Mbona hao walinzi walikuwapo lakini akaanguka? Matatizo yale si ya kiafya. Sheikh anafanya kwa kuwa anampenda na hutasikia tena anaanguka."
Awali Sheikh Yahya alinukuliwa katika taarifa yake akisema kwamba atatoa ulinzi usioonekana kwa macho kumkinga Rais Kikwete ili mtu yeyote asijaribu kumfanyia ‘mchezo' wowote kama ilivyotokea Jangwani.
Sheikh Yahya alisema katika taarifa hiyo ya kuwa amefikia hatua hiyo kutokana na uchungu alionao kwa nchi na kwa Rais Kikwete anayempenda.
Kufuatia kauli hiyo, Dk. Slaa alikemea kauli hiyo na kusema: "Nchi haiwezi kuongozwa na uchawi. Haiongozwi na imani za watu, kila mtu ana imani yake, lakini tusifike mahali tukaongoza nchi kwa uchawi."
Alimtaka Rais Jakaya Kikwete kumkemea Sheikh Yahya kwa kauli hiyo iliyotolewa juzi Dar es Salaam, la sivyo wananchi wataamini mnajimu huyo anatumiwa na CCM kuleta hofu katika jamii.
Dk. Slaa aliwakumbusha wananchi kuwa mwanzoni mwa mwaka huu, Sheikh Yahya alisema mtu yeyote atakayegombea urais na Kikwete atakufa na kuongeza: "Sisi wengine ni majabali, hatuogopi kufa kwa ushirikina."
Tayari serikali imesema haihusiki na hoja ya ‘ulinzi' usioonekana kwa Rais Kikwete, kama ilivyotangazwa na Sheikh Yahaya.
Hata hivyo, Sheikh Yahya alisema hakuwa anazungumzia uchawi wala nguvu za giza, "bali majini ambao ni viumbe kama sisi, isipokuwa wao wameumbwa kwa moto na sisi tumeumbwa kwa udongo na wametajwa katika vitabu vyote vitakatifu vya Waisalamu na Wakristo na Mwenyezi Mungu amesema tushirikiane nao".
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kampeni za CCM, Abdulrahman Kinana, alisema Rais Kikwete ni muumini wa Dini ya Kiislamu, ambaye anaamini Mungu na hivyo hahusiki kwa vyovyote na kauli ya Sheikh Yahya.
Kauli hiyo ya Sheikh Yahya imeibua mjadala mkali; huku baadhi ya wananchi wakitaka uchunguzi wa kina ufanyike kuangalia kama kuna fedha za umma zinazotumika kugharamia masuala ya ushirikina.
Baadhi ya wananachi hao, wakiwamo viongozi wa dini, wamekemea tabia ya baadhi ya viongozi kukimbilia katika imani za ushirikina baadhi wakitumia raslimali za umma katika kugharamia imani hizo.
Rais Kikwete amepata kuanguka hadharani mara tatu; mara ya mwisho ikiwa ni wakati akizindua kampeni yake ya urais, hivi karibuni, katika viwanja vya Jangwani, Dar es Salaam.
Alipata pia kukiri hadharani kwamba alimsaidia Sheikh Yahya fedha za kwenda matibabuni nje ya nchi.
Akizungumzia kauli za viongozi wa CCM na Serikali kwamba hawatambui "ulinzi wa majini" aliosema atautoa kwa Kikwete, Sheikh Yahya, amesema: "Sihitaji kibali cha yeyote kumuwekea rais wangu ulinzi wa majini."
Sheikh Yahya, ambaye amekuwa akitoa kauli tata kuhusiana na Kikwete hata kabla ya kampeni kuanza, alisema, jana, jijini, kuwa anachozungumzia yeye si uchawi wala ushirikina; bali ni mambo ambayo yapo na hayakwepeki.
"Kila mtu anazaliwa na jini. Hata Slaa (Dk.Willibrod Slaa, Mgombea urais wa CHADEMA) ana jini anaitwa Subiani. Nakwambia sihitaji kumshirikisha mtu katika hili," alisema Sheikh Yahya Hussein na kumkabidhi simu mwanae aliyejitambulisha kwa jina la Hassan, ambaye naye alisema;
"Sheikh alisema binafsi hahitaji kumshirikisha mtu katika hili. Serikali iendelee na ulinzi wake na yeye atatoa ulinzi wake. Mbona hao walinzi walikuwapo lakini akaanguka? Matatizo yale si ya kiafya. Sheikh anafanya kwa kuwa anampenda na hutasikia tena anaanguka."
Awali Sheikh Yahya alinukuliwa katika taarifa yake akisema kwamba atatoa ulinzi usioonekana kwa macho kumkinga Rais Kikwete ili mtu yeyote asijaribu kumfanyia ‘mchezo' wowote kama ilivyotokea Jangwani.
Sheikh Yahya alisema katika taarifa hiyo ya kuwa amefikia hatua hiyo kutokana na uchungu alionao kwa nchi na kwa Rais Kikwete anayempenda.
Kufuatia kauli hiyo, Dk. Slaa alikemea kauli hiyo na kusema: "Nchi haiwezi kuongozwa na uchawi. Haiongozwi na imani za watu, kila mtu ana imani yake, lakini tusifike mahali tukaongoza nchi kwa uchawi."
Alimtaka Rais Jakaya Kikwete kumkemea Sheikh Yahya kwa kauli hiyo iliyotolewa juzi Dar es Salaam, la sivyo wananchi wataamini mnajimu huyo anatumiwa na CCM kuleta hofu katika jamii.
Dk. Slaa aliwakumbusha wananchi kuwa mwanzoni mwa mwaka huu, Sheikh Yahya alisema mtu yeyote atakayegombea urais na Kikwete atakufa na kuongeza: "Sisi wengine ni majabali, hatuogopi kufa kwa ushirikina."
Tayari serikali imesema haihusiki na hoja ya ‘ulinzi' usioonekana kwa Rais Kikwete, kama ilivyotangazwa na Sheikh Yahaya.
Hata hivyo, Sheikh Yahya alisema hakuwa anazungumzia uchawi wala nguvu za giza, "bali majini ambao ni viumbe kama sisi, isipokuwa wao wameumbwa kwa moto na sisi tumeumbwa kwa udongo na wametajwa katika vitabu vyote vitakatifu vya Waisalamu na Wakristo na Mwenyezi Mungu amesema tushirikiane nao".
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kampeni za CCM, Abdulrahman Kinana, alisema Rais Kikwete ni muumini wa Dini ya Kiislamu, ambaye anaamini Mungu na hivyo hahusiki kwa vyovyote na kauli ya Sheikh Yahya.
Kauli hiyo ya Sheikh Yahya imeibua mjadala mkali; huku baadhi ya wananchi wakitaka uchunguzi wa kina ufanyike kuangalia kama kuna fedha za umma zinazotumika kugharamia masuala ya ushirikina.
Baadhi ya wananachi hao, wakiwamo viongozi wa dini, wamekemea tabia ya baadhi ya viongozi kukimbilia katika imani za ushirikina baadhi wakitumia raslimali za umma katika kugharamia imani hizo.
Rais Kikwete amepata kuanguka hadharani mara tatu; mara ya mwisho ikiwa ni wakati akizindua kampeni yake ya urais, hivi karibuni, katika viwanja vya Jangwani, Dar es Salaam.
Alipata pia kukiri hadharani kwamba alimsaidia Sheikh Yahya fedha za kwenda matibabuni nje ya nchi.