Sheikh Suleiman Takadir na Benard Membe ''Wakorofi'' Ndani ya TANU 1958 na CCM 2020

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
20,916
30,259
SHEIKH SULEIMAN TAKADIR NA BENARD MEMBE ''WAKOROFI'' NDANI YA TANU 1958 NA CCM 2020

Ilikuwa baada ya L'Asr siku nilipokwenda nyumbani kwa Sheikh Haidar Mwinyimvua katika wanachama wa mwanzo wa TANU na mjumbe katika Halmashauri Kuu ya TANU na mmoja wa wajumbe wa Baraza la Wazee wa TANU.

Nilikuwa katika utafiti wa kuandika historia ya TANU.

Mjukuu wake ndiye alikuwa kanichukua kunipeleka kwa babu yake anieleza kisa cha Sheikh Suleiman Takadir vipi alivunja moja ya mwiko mkubwa wa TANU na adhabu yake ikawa ''kutoswa.''

Miaka ile ukifukuzwa TANU inaitwa umetoswa, yaani umetupwa baharini uliwe na papa na samaki wengine au maji yakupeleke mbali kabisa ukiwa maiti.

Niliposikia Benard Membe kafukuzwa CCM ilinijia picha ya Sheikh Suleiman Takadir jinsi alivyofukuzwa TANU mwaka wa 1958 akatengwa na jamii nzima ya Dar es Salaam, Barza maarufu iliyokuwa nyumbani kwake Mtaa wa Msimbazi ikahama na yeye akapewa jina, ''Takadiri Mtaka Dini.''

Wakati wa enzi yake ananisimulia Sheikh Haidar Mwinyimvua tumekaa ukumbini kwake nyumbani kwake nyumba ya vyumba sita ya National Housing, Magomeni Mapipa, ''Sheikh Suleiman Takadir tukimuiita Makarios kwa kuwa alikuwa sheikh mwanasiasa mpigania uhuru kama Askofu Makarios wa Cyprus.''

Sheikh Suleiman Takadir kisa chake kinatisha kiasi watu walikuwa wanaogopa kukihadithia hadi leo kwani si historia ambayo mtu atapenda kuieleza.

Kisa cha Sheikh Suleiman Takadir hakika kinatisha na katika utafiti wangu baadhi ya wana TANU nikiwauliza habari za Sheikh Takadir wakikwepa kueleza historia ya sheikh ingawa ni kisa maarufu.

Huwezi kuandika historia ya TANU na kupigania uhuru wa Tanganyika usimtaje Sheikh Suleiman Takadiri.

Wakati wake Sheikh Suleiman Takadir siku hizo si wengi walikuwa wanamfahamu Nyerere, yeye alikuwa anatangulia kupanda jukwaani katika mikutano ya mwanzo pale Mnazi Mmoja kusoma dua na kumtambulisha Nyerere kwa wananchi.

Nyerere atapanda jukwaani huku akisindikizwa na nyimbo maarufu, ''Muheshimwa nakupenda sana wallahi sina mwingiewe In Shaa Allah Mungu yuko Tanganyika tutajitawala.''

Huyo Bi. Hawa bint Maftah na Bi, Titi Mohamed na akina mama wengine wanaimba.

Wanasema wasemaji nyimbo hii ilikuwa ikimliza Nyerere kila alipoimbiwa.

Turudi kwa Makarios.

Ikutoshe tu kuwa baada ya kufukuzwa TANU Sheikh Takadiri hakuwa na maisha tena akafa akiwa mtu aliyedhalilika kupita kiasi.

Sitegemei kama Membe atapigwa pande na jamaa zake wala sidhani kama atadhalilika na atakufa kwa simanzi kwa kufukuzwa chama kama alivyokufa Sheikh Suleiman Takadiri.

Lakini Membe ikiwa kama atabahatika kuisoma historia ya TANU na historia ya Sheikh Suleiman Takadiri atajifunza mengi.

PICHA: Kulia ni Bi. Titi Mohamed, Clement Mtamila, Sheikh Suleiman Takadiri, Julius Nyerere. Nyuma kulia John Rupia, Rajab Diwani na Mama Maria Nyerere.

SHEIKH SULEIMAN TAKADIR.JPG
 
Hivi hawa Masheikh wangekabidhiwa Uhuru wa hii nchi yetu Tanganyika tungekuwa na hali gani sasa hivi?

Sent using Jamii Forums mobile app
Mtochoro,
Kwa nini wakabidhiwe masheikh uchumi wa nchi yetu ilhali wao hawana ujuzi wa kuendesha nchi?
Masheikh walikuwa na kazi ambayo waliifanya kwa ufanisi mkubwa sana.

Mathalan Sheikh Hassan bin Ameir kama Mufti wa Tanganyika yeye kazi yake ilikuwa kujenga umoja na mapenzi baina ya wananchi wawe kitu kimoja bila kujali dini zao.

Ili uelewe vyema Mufti cheo chake ni sawa na Kadinali kama vile Pengo.
Fikiria kumuona Kadinali Pengo yuko na Nyerere ubavu kwa ubavu wakati wa kupigania uhuru miaka ya 1950.

Sheikh Hassan bin Ameir alikuwa hodari sana katika hili na aliweza kuielekeza TANU katika barabara ya kuwa ''nationalist-secularist party.''

Sheikh Suleiman Takadir yeye alikuwa mwanasiasa wa jukwaa na alikuwa kati ya wazungumzaji watatu hodari wa TANU baada ya Mwalimu Nyerere, Bi. Titi Mohamed kisha Sheikh Suleiman Takadiri.

Mchango wa masheikh katika kupigania uhuru wa Tanganyika hauna mfano wake katika viongozi wa dini.
Masheikh hawakuwaogopa Waingereza.

BARAZA LA WAZEE WA TANU.jpg
 
Umetuficha kila kitu kuhusu mfanano halisi wa anguko la member ccm2020. Na shekhe takadir 1958. Mfanano wao uko tu kwenye kufukuzwa huyu tanu huyu ccm.. sababu, SABABU ipi na utuambie leo tafadhali

Sent using Jamii Forums mobile app
 
TAFUTA NA USOME HISTORIA YA UHURU WA NCHI HII ISIYOPINDISHWA KISHA UTAPATA JIBU LA SWALI LAKO LENYE CHUKI

Sinafungu,
Umemjibu nduguyo ukiwa umeghadhibika.
Mchukulie huyu kuwa ni mtu asiyeijua historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika.

Laiti angeliijua asingeandika hayo aliyoandika.

Mimi nimemueleza yale ambayo masheikh waliyafanya bega kwa bega na Mwalimu Nyerere kupigania uhuru wa Tanganyika chinu ya TANU.

Kwa kujua kuwa yeye shida yake ni masheikh nikampa mfano ambao naamini umemgusa na ndiyo maana bila shaka kawa kimya.

Nimemweleza kuwa Mufti Sheikh Hassan bin Ameir kwa nafasi yake kwa Waislam ni mfano wa Kadinali Pengo kwa Wakatoliki.

Sasa nikamuomba avute picha kuwa Kadinali Pengo mwaka wa 1950 na majoho yake amesimama bega kwa bega na Mwalimu Nyerere wanapigania uhuru wa Tanganyika.

Picha bila shaka kaipata na kaelewa.
Huyu hawezi kurejea tena hapa na dharau na kuwakejeli masheikh.
 
Mzee Mohamed Said shikamoo. Pole na mihangaiko yako mzee, binafsi ningependa kujua zaidi kuhusu huyo Mzee Haidar Mwinyimvua ni huyu huyu mwenyeji wa Bagamoyo au sie ninaem-maanisha mimi?

ᴾᵘⁿⁱˢʰ ᵒⁿˡʸ ʰᵉ ʷʰᵒ ᶜᵒᵐᵐⁱᵗᵗᵉᵈ ᵗʰᵉ ᶜʳⁱᵐᵉ
 
Waislamu wengi sana waliisaliti TANU na kujiunga na chama chao cha waislamu kilichoitwa AMNUT( All Muslim National Union) miongoni mwao ni Sulleiman Takadir na Abdul Sykes.
 
Hakuna kitu kigumu kama kumbadilisha mtu mawazo hasa yale anayoamini kuwa ni sahihi. Kuna sehemu kwenye historia ya nchi yetu tulijikwaa ndiyo maana tumejaribu kuficha mambo mengi ya msingi aidha kuficha aibu au ubaguzi.

Nafahamu kwamba kulikuwa na hili jaribu la baadhi ya waislamu waliokosa uungwana kutaka kulifanya taifa hili kuwa De Facto-Muslim State. Lakini pia kuna wakristo wa aina hiyo pia hapa nchini, walikuwepo kipindi kile na bado wapo leo hii wanaotaka nafasi nyeti za taifa hili zishikwe na wakristo tu.

Ambacho waislamu wengi waungwana wanakidai kuhusu historia ya Tanganyika siyo kingine zaidi ya kutambulika kwa uwepo wao na mchango wao (Formal Appreciation) kwenye ujenzi wa taifa hili ambao ulipuuzwa kwasababu zisizoeleweka hadi kupelekea kuzaliwa kwa hisia za kuwepo kwa udini upande wa Baba wa Taifa (Mfumo Kristo).

Hili ndilo ambalo linaiumiza nchi ya Marekani mpaka leo hii. Walipuuza mchango mkubwa wa watu weusi katika ujenzi wa lile taifa, kwasababu wao waliamini kwamba zaidi ya wahamiaji kutoka Italia, Visiwa vya Ireland na Uingereza mweusi alikuwa hana chake.

Sasa leo hii yanaanza kufumuka mambo makubwa ambayo weusi waliyafanya yaliyotakiwa kuwekwa kwenye historia lakini hayakuwekwa kwasababu za kibaguzi, wazungu wanachanganyikiwa na kuanza kupinga kwasababu waliaminishwa uongo/walipewa ukweli nusu huko mashuleni.

Katika kupinga huku kwa kisingizio cha Historical Revisionism wamekuta jamii za watu weusi na weupe zikizidi kuchukiana chini chini. Wataalamu wanajuta kwanini walichelewa kurekebisha mambo mapema.
 
waislamu wengi sana waliisaliti TANU na kujiunga na chama chao cha waislamu kilichoitwa AMNUT( All Muslim National Union) miongoni mwao ni Sulleiman Takadir na Abdul Sykes.
Laki...
Umekosea.

Kwanza kama Waislam walikuwa na chama ni TANU.

Historia ya TANU nimekuhadithia naamini Unaifahamu vyema.

AMNUT ilianzishwa na Ramadhani Mashado Plantan, Abdulwahid Abdulkarim, Abdallah Mohamed na watu wengine wachache.

AMNUT haikumvutia mtu yeyote.

Waislam walihusishwa na chama hicho kwa hilo jina hapakuwa na kingine.

Suleiman Takadir baada ya kufukuzwa TANU alibakia ndani hadi umauti.

Abdul Sykes hakujiunga na AMNUT unajua hii ilikuwa 1958 bado akikisaidia sana chama.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom