Sheikh Ponda na uchaguzi wa Rais 2010

Sheikh Ponda na uchaguzi wa Rais 2010

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
23,282
Reaction score
33,880
SHEIKH PONDA ISSA PONDA NA UCHAGUZI WA RAIS 2010

Wakati wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 nilikuwa naishi Tanga na ikawa nimekuja Dar es Salaam.

Nimekutana na Sheikh Ponda Msikiti wa Manyema baada ya Sala ya Alasiri.

Muda mrefu tulikuwa hatujaonana tukawa tumesimama pembeni tunazungumza.

Namwangalia Sheikh Ponda namuona kadhoofu na mikono yake imejaa alama ndogo ndogo za upele.

Nikamuuliza kulikoni hali ile.

Sheikh Ponda akaniambia kuwa yeye haumwi lakini amekuwa akizunguka nchi nzima kumfanyia kampeni mgombea mmoja wa urais.

Aliponitajia jina la mgombea na chama anachotoka hakika nilipatwa na mshtuko nikataka kujua habari zile zaidi.

"Kuna njama zimesukwa dhidi ya ndugu yetu kumwangusha ili awe rais wa kipindi kimoja na mpinzani wake anaungwa mkono na watu wenye nguvu sana wengine ndani ya chama chake."

Taratibu Sheikh Ponda akanieleza hali inayomkabili huyu ndugu yetu.

"Natembea kijiji kwa kijiji nazungumza na ndugu zetu nawaeleza uamuzi tuliofikia na kuwaomba wabadilishe upigaji kura wao tumsaidie huyu ndugu yetu asifedheheshwe kwani kuanguka kwake ndiyo kuanguka kwetu."

Sheikh Ponda akaniambia alikuwa huko vijijini kwa muda mrefu anazunguka nchi nzima akibebwa kwenye baiskeli kutoka kijiji kimoja kwenda kingine na akilala misikitini.

Huku kulala kwenye hii misikiti ya vijijini ndiyo sababu ya kuumwa sana na mbu.

Nimeinamisha kichwa changu chini sina la kusema.
Wapi mtu utapata la kusema unapopambana hila kama hizi?

Nimeingiwa na simanzi kwani naujua umasikini wa watu hawa wanaompokea Sheikh Ponda lakini najua pia ari zao ndani ya dhiki zao.

Niliponyanyua kichwa changu nikamuuliza kama hao anaowafanyia kampeni wanafahamu hizi juhudi zake.

Sheikh Ponda akatingisha kichwa huku anatabasamu akaniambia kuwa hawakuwa wanajua chochote.

"Sheikh Ponda unawafanyia hisani kubwa sana hawa jamaa na In Shaa Allah ndugu yetu atapita lakini sisi hali yetu itabakia vilevile," nilimweleza Ponda.

"Hilo si kama silijui lakini kesho nitakuwa na majibu ya kumjibu Allah kuwa nilisimama na ndugu yangu pale alipokabiliwa na maadui zake kumdhuru"

Baada ya uchaguzi Sheikh Ponda alipambana na masahibu mengi na mwisho akapigwa risasi ya bega Morogoro.

Huwezi kummaliza Sheikh Ponda kwani ana mengi.
IMG-20200712-WA0143.jpg
 
Tatizo ni Shekh kujiingiza kwenye siasa.
Matokeo ya Siasa ndani ya dini ndio haya
 
Tatizo ni Shekh kujiingiza kwenye siasa.
Matokeo ya Siasa ndani ya dini ndio haya
Jingalao,
Masheikh wetu walikuwa kwenye siasa toka.enzi za TAA na ndiyo waliounda TANU.

Masheikh hawajajiingiza wamekutwa na waliokuja Dar es Salaam tayari wako katika siasa.

Soma historia ya TANU.

Mapadri ndiyo waliojitenga na siasa wakaja kuingia uhuru ushapatikana.
 
Jingalao,
Masheikh wetu walikuwa kwenye siasa toka.enzi za TAA na ndiyo waliounda TANU.

Masheikh hawajajiingiza wamekutwa na waliokuja Dar es Salaam tayari wako katika siasa.

Soma historia ya TANU.

Mapadri ndiyo waliojitenga na siasa wakaja kuingia uhuru ushapatikana.
Hoja yangu pamoja na historia hiyo jee kwa muktadha wa leo yaani hatupo tena kwenye kudai uhuru je ni sahihi kwa wao kuendelea kujiingiza kwenye siasa tena kwa kushawishi waumini kuchukua mirengo ya kisiasa?
 
Hoja yangu pamoja na historia hiyo jee kwa muktadha wa leo yaani hatupo tena kwenye kudai uhuru je ni sahihi kwa wao kuendelea kujiingiza kwenye siasa tena kwa kushawishi waumini kuchukua mirengo ya kisiasa?
Jingalao,
Unazijua Pastoral Letters za Tanzania Episcopal Conference (TEC)?
 
Nchi yetu ukiwa na vyeo viwili halafu ukawa unaongea "UKWELI (HAUPIGI MAPAMBIO), basi huwezi na usitegemee kuthaminika hata kidogo, ukiwa "SHEIKH au ASKOFU".

Mfano, Askofu Bagonza na Sheikh Ponda, ila ukiwa kama Sheikh Wa Dar (Mzee Wa Kula Bata Dubai) basi kiti chako ni uhakika mpaka 2020.
 
Alimpigania huyo mgombea si kwa sababu ya ubora sera zake bali ni kwa sababu ya dini yake. Hapa ndipo ccm wanatuweza, wakiona hali imekua mbaya kwao wanapenyeza agenda ya udini, ukabila ama ukanda huku wao wanazidi kupeta tu
Mzee,
Agenda ya udini haijapata kuondoka na ndiyo TANU waliitumia kudai uhuru.

Hujui histori ya Waislam katika TANU?
 
Jingalao,
Unazijua Pastoral Letters za Tanzania Episcopal Conference (TEC)?
Naamu nazitambua sana.
Je ,huwa zinatolewa baada ya mchakato gani?
Je, ni lazima kuwepo ushindani wa namna hii?
Je, ni sahihi kuendelea kuwepo na kutolewa kwa matumizi ya jamii?
Hapa tufikiri wote kwa fikra huru...
 
SHEIKH PONDA ISSA PONDA NA UCHAGUZI WA RAIS 2010

Wakati wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 nilikuwa naishi Tanga na ikawa nimekuja Dar es Salaam.

Nimekutana na Sheikh Ponda Msikiti wa Manyema baada ya Sala ya Alasiri.

Muda mrefu tulikuwa hatujaonana tukawa tumesimama pembeni tunazungumza.

Namwangalia Sheikh Ponda namuona kadhoofu na mikono yake imejaa alama ndogo ndogo za upele.

Nikamuuliza kulikoni hali ile.

Sheikh Ponda akaniambia kuwa yeye haumwi lakini amekuwa akizunguka nchi nzima kumfanyia kampeni mgombea mmoja wa urais.

Aliponitajia jina la mgombea na chama anachotoka hakika nilipatwa na mshtuko nikataka kujua habari zile zaidi.

"Kuna njama zimesukwa dhidi ya ndugu yetu kumwangusha ili awe rais wa kipindi kimoja na mpinzani wake anaungwa mkono na watu wenye nguvu sana wengine ndani ya chama chake."

Taratibu Sheikh Ponda akanieleza hali inayomkabili huyu ndugu yetu.

"Natembea kijiji kwa kijiji nazungumza na ndugu zetu nawaeleza uamuzi tuliofikia na kuwaomba wabadilishe upigaji kura wao tumsaidie huyu ndugu yetu asifedheheshwe kwani kuanguka kwake ndiyo kuanguka kwetu."

Sheikh Ponda akaniambia alikuwa huko vijijini kwa muda mrefu anazunguka nchi nzima akibebwa kwenye baiskeli kutoka kijiji kimoja kwenda kingine na akilala misikitini.

Huku kulala kwenye hii misikiti ya vijijini ndiyo sababu ya kuumwa sana na mbu.

Nimeinamisha kichwa changu chini sina la kusema.
Wapi mtu utapata la kusema unapopambana hila kama hizi?

Nimeingiwa na simanzi kwani naujua umasikini wa watu hawa wanaompokea Sheikh Ponda lakini najua pia ari zao ndani ya dhiki zao.

Niliponyanyua kichwa changu nikamuuliza kama hao anaowafanyia kampeni wanafahamu hizi juhudi zake.

Sheikh Ponda ajatingusha kichwa huku anatabasamu akaniambia kuwa hawakuwa wanajua chochote.

"Sheikh Ponda unawafanyia hisani kubwa sana hawa jamaa na In Shaa Allah ndugu yetu atapita lakini sisi hali yetu itabakia vilevile," nilimweleza Ponda.

"Hilo si kama silijui lakini kesho nitakuwa na majibu ya kumjibu Allah kuwa nilisimama na ndugu yangu pale alipokabiliwa na maadui zake kumdhuru"

Baada ya uchaguzi Sheikh Ponda alipambana na masahibu mengi na mwisho akapigwa risasi ya bega Morogoro.

Huwezi kummaliza Sheikh Ponda kwani ana mengi.View attachment 1504843
Nampa pongezi sana kwa waraka wake pia[emoji122][emoji122][emoji122]
 
Hoja yangu pamoja na historia hiyo jee kwa muktadha wa leo yaani hatupo tena kwenye kudai uhuru je ni sahihi kwa wao kuendelea kujiingiza kwenye siasa tena kwa kushawishi waumini kuchukua mirengo ya kisiasa?
Mimi ni Mkatoliki. Sikupendezwa na jinsi Mwadhama Kardinali Pengo alivyokuwa akiwashambulia rais Mwinyi na Kikwete, huku akiwa mpole kwa rais Mkapa na rais Magufuli. Huo ndio UDINI. Na sidhani kama anayelalamika kutotendewa haki, ndiyo anyamazishwe kwa kuitwa mdini
 
SHEIKH PONDA ISSA PONDA NA UCHAGUZI WA RAIS 2010

Wakati wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 nilikuwa naishi Tanga na ikawa nimekuja Dar es Salaam.

Nimekutana na Sheikh Ponda Msikiti wa Manyema baada ya Sala ya Alasiri.

Muda mrefu tulikuwa hatujaonana tukawa tumesimama pembeni tunazungumza.

Namwangalia Sheikh Ponda namuona kadhoofu na mikono yake imejaa alama ndogo ndogo za upele.

Nikamuuliza kulikoni hali ile.

Sheikh Ponda akaniambia kuwa yeye haumwi lakini amekuwa akizunguka nchi nzima kumfanyia kampeni mgombea mmoja wa urais.

Aliponitajia jina la mgombea na chama anachotoka hakika nilipatwa na mshtuko nikataka kujua habari zile zaidi.

"Kuna njama zimesukwa dhidi ya ndugu yetu kumwangusha ili awe rais wa kipindi kimoja na mpinzani wake anaungwa mkono na watu wenye nguvu sana wengine ndani ya chama chake."

Taratibu Sheikh Ponda akanieleza hali inayomkabili huyu ndugu yetu.

"Natembea kijiji kwa kijiji nazungumza na ndugu zetu nawaeleza uamuzi tuliofikia na kuwaomba wabadilishe upigaji kura wao tumsaidie huyu ndugu yetu asifedheheshwe kwani kuanguka kwake ndiyo kuanguka kwetu."

Sheikh Ponda akaniambia alikuwa huko vijijini kwa muda mrefu anazunguka nchi nzima akibebwa kwenye baiskeli kutoka kijiji kimoja kwenda kingine na akilala misikitini.

Huku kulala kwenye hii misikiti ya vijijini ndiyo sababu ya kuumwa sana na mbu.

Nimeinamisha kichwa changu chini sina la kusema.
Wapi mtu utapata la kusema unapopambana hila kama hizi?

Nimeingiwa na simanzi kwani naujua umasikini wa watu hawa wanaompokea Sheikh Ponda lakini najua pia ari zao ndani ya dhiki zao.

Niliponyanyua kichwa changu nikamuuliza kama hao anaowafanyia kampeni wanafahamu hizi juhudi zake.

Sheikh Ponda akatingisha kichwa huku anatabasamu akaniambia kuwa hawakuwa wanajua chochote.

"Sheikh Ponda unawafanyia hisani kubwa sana hawa jamaa na In Shaa Allah ndugu yetu atapita lakini sisi hali yetu itabakia vilevile," nilimweleza Ponda.

"Hilo si kama silijui lakini kesho nitakuwa na majibu ya kumjibu Allah kuwa nilisimama na ndugu yangu pale alipokabiliwa na maadui zake kumdhuru"

Baada ya uchaguzi Sheikh Ponda alipambana na masahibu mengi na mwisho akapigwa risasi ya bega Morogoro.

Huwezi kummaliza Sheikh Ponda kwani ana mengi.View attachment 1504843

Rais wa muhula mmoja ni JK? Maana useme wazi. Sababu hata risasi alipigwa kipindi cha awamu ya nne. Tuwe wakweli, nani anayewaonea waislamu? Mbona ni kama kila siku anatafutwa mchawi?
 
Back
Top Bottom