Sheikh Mawinda: Sikumaanisha Lissu auawe

Sheikh Mawinda: Sikumaanisha Lissu auawe

Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maridhiano Dar es Salaam, Sheikh Mohamed Mawinda, amesea kauli yake kuhusu wanaovunja amai nchini aliyoitoa Julai 5, 2025 haikumaanisha kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu auawe.

Akizungumza katika uzinduzi wa kanisa la Arise and Shine uliofanyika Julai 5, 2025 na kuhudhuriwa na Rais Samia Suluhu Hassan jijini Dar es Salaam, Sheikh Mawinda ambaye pia ni kada wa CCM, alisisitiza umuhimu wa amani, akirejea kauli aliyowahi kuitoa Lissu ya kukinukisha na kusema kuwa amefikishwa mahakamani ili kuipima. "Acha mtu akate kichwa chako lakini nchi hii ibaki salama," alisema.
Soma zaidi: Sheikh Mawinda

Lakini akizungumza na The Chanzo leo, Sheikh Mawinda amesema hakumaanisha kuwa Lissu auawe.

Sikiliza:
View attachment 3398020
Hawa masheikh huwa wanawapata wapi au mtu tu mwenye ujasiri wa kuongea na kufuga mandevu kama kichaa huko msikitini anapewa usheikh
 
...akirejea kauli aliyowahi kuitoa Lissu ya kukinukisha na kusema kuwa amefikishwa mahakamani ili kuipima. "Acha mtu akate kichwa chako lakini nchi hii ibaki salama," alisema.
Na huyo shekhe Mawindo pia inafaa aburuzwe mahakamani ili kauli yake ya "kukata kichwa" ikapimwe huko, au mkuki kwa nguruwe?
 
Back
Top Bottom