shangingi la Sh155milioni kwa Sh6 milioni

shangingi la Sh155milioni kwa Sh6 milioni

saitama_kein

JF-Expert Member
Joined
Oct 29, 2009
Posts
981
Reaction score
100
KATIBU Tawala wa Mkoa wa Kilimanjaro, Hilda Gondwe anadaiwa kuomba auziwe kwa Sh6 milioni gari la serikali aina ya Toyota Landcruiser VX lililonunuliwa miaka mitatu iliyopita kwa Sh96 milioni.

Mwishoni mwa mwaka jana, gari hilo lenye namba za usajili STK 1867 lililokuwa likitumiwa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro (RC), Monica Mbega lilikarabatiwa na kampuni ya Toyota ya jijini Dar es Salaam kwa Sh11 milioni.

Kwa kawaida magari ya serikali huwa hayalipiwi kodi, lakini kama gari hilo lingenunuliwa kwa bei ya soko, kuingizwa nchini na kulipiwa kodi mbalimbali ikiwamo ile ya 0ngezeko la Thamani(VAT), lingekuwa na thamani ya Sh155.7 milioni.

Shangingi lenye bei kama hiyo likiingizwa nchini linatakiwa kulipiwa Sh24 milioni kama kodi ya uagizaji (Import duty), Sh23.7 milioni kama VAT na Sh12 milioni ambazo ni kodi ya ushuru wa forodha.


Source: Mwananchi


 
hospitali ngapi zingejengwa na iyo hela ya shangingi moja? hii ndo tz bwana.
 
Kila mtu anakula urefu wa kamba yake jamani huyo mdogo sana
anachofanya ukiangalia na wauwaji wa bot............................
Mama ningekuwa mimi ningeizinisha mawili kabissa
 
Nimechoka kushangaaa.....
Mambo ya nchi hii ukiyafuatilia sana unaweza
pata cancer.......

Wacha wale tu.............
 
Nimechoka kushangaaa.....
Mambo ya nchi hii ukiyafuatilia sana unaweza
pata cancer.......

Wacha wale tu.............

The cry of a defeated soldier! Mtawaachia tu...shida ipo wapi?
 
he he mi sishangai sana kwa sababu nimeona wangine wakiuziwa kwa two millioni toyota land cruiser tena inayokata mbuga kama kawaida, na usishangae ukisikia mwaka juzi huyo mtu aliuziwa nyingine kama hiyo au nissani patrol. zis is only in TZ bwana.
 
Jamani hii serikali vipi manake hili gari jipya kabisa hakuna hata value for money gari limetumika miaka 3 jamani RAS kilimanjaro
unatuumiza we mama vipi lakini mbona hatukuelewi..........................
 
hivi jamani tanzania aina wenyewe hivi akuna watanzania ni lini basi watanzania wataamka kutoka usingizini nilini watanzania wataanza kuwawajibisha watawala wao wanaowadanganya kama watoto inauma sana tena sana kila mtu kujigemea anavyotaka
 
Back
Top Bottom