Kenyan
JF-Expert Member
- Jun 7, 2012
- 414
- 313
Polisi wamelazimika kutumia mabomu ya machozi kutawanya Vijana wa Kimaasai maarufu kama 'morans' baada ya kuvamia ardhi ya Uhuru Kenyatta iliyoko Kedong', kaunti ya Narok.
Duru za kuaminika zinasema kuwa wiki iliyopita Mbunge wa Eneo hilo Ken Aramat, aliapa kuongoza morans katika harakati za kuikomboa ardhi ya Wamaasai inayomilikiwa na familia ya Kenyatta.
Kitendo hiki kinakuja yapata siku mbili tu baada ya shamba la Kenyatta lililoko Ruiru kaunti ya Kiambu kuvamiwa na mamia ya mbuzi aina Dorper kuibwa.
Kwa sasa mashamba yote hayo mawili yapo chini ya ulinzi mkali wa maafisa wa polisi.
Duru za kuaminika zinasema kuwa wiki iliyopita Mbunge wa Eneo hilo Ken Aramat, aliapa kuongoza morans katika harakati za kuikomboa ardhi ya Wamaasai inayomilikiwa na familia ya Kenyatta.
Kitendo hiki kinakuja yapata siku mbili tu baada ya shamba la Kenyatta lililoko Ruiru kaunti ya Kiambu kuvamiwa na mamia ya mbuzi aina Dorper kuibwa.
Kwa sasa mashamba yote hayo mawili yapo chini ya ulinzi mkali wa maafisa wa polisi.