Tafakari: Uvamizi wa shamba la Kenyatta na shambulio la Lissu

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,802
Jana Machi 27, shamba la familia ya Rais Mstaafu wa Kenya Uhuru Kenyatta lilivamiwa na uharibifu pamoja na wizi kufanyika. Shambani humo moto mkubwa uliwashwa; miti ya mbao na nguzo ilikatwa na wizi wa mali mbalimbali wakiwemo mamia ya kondoo ulifanyika.

Tundu Lissu, mnamo Septemba 7, 2017 alishambuliwa kwa risasi na 'watu wasiojulikana' kulikokuwa nyumbani kwake Area D, jijini Dodoma. Lissu alipata maumivu makali na shambulio hilo limemuachia 'ulemavu' wa kudumu mwilini na akilini mwake.

Ni utaratibu wa dunia nzima kuwa makazi na mali za viongozi wakuu wastaafu kulindwa kwa namna yoyote. Hata makazi yao baada ya kustaafu hulindwa na askari wanaobadilishana zamu kila uchao. Sasa Kenyatta wawili wameshakuwa marais wa Kenya.

Ni utaratibu wa nchi yetu kuwa makazi ya Mawaziri, Ofisi ya Spika na Wabunge kule Dodoma hulindwa kila uchao kwa ajili ya kuhakikisha usalama wa viongozi wetu hao. Lissu alikuwa Mbunge na alikuwa akiishi kwenye makazi yaliyokuwa na ulinzi mkali, Area D.

Wakati wa uvamizi wa shamba la Kenyatta jana hakukuwa na wala hawakufika maafisa wa usalama-kama polisi kwa ajili ya kulinda shamba hilo dhidi ya uvamizi huo. Hata Septemba 7, 2017 Area D wakati wa shambulio la Lissu haikuwa na ulinzi kama ilivyokuwa kawaida yake. Inashangaza na kutafakarisha.

Raila Odinga si wa kupuuzwa!

Mzee Tupatupa wa Lumumba ( safarini Nairobi, Kenya)
 
Kinachotokea huko Kenya ni sehemu ya siasa za mvutano kati ya Raila na Rutto...
brazaj

Mkuu nyomi hizi ni kubwa mno kujaribu kuuhalalisha kirahisi rahisi mgogoro kihivyo.

Screenshot_20230326-222358.jpg


Zingatia polisi walihusika Jana kupiga waandishi na kushadadia shamba la uhuru kuhujumiwa:
 
Concern ya mtoa mada haijaeleweka kwako, na haita eleweka kwa wengi wenye akili ndogo.
Ni mpuuzi na mpumbavu kama wewe ndio anayeweza kushindwa kuona anachotaka kuelewesha....ambacho hakuna. Zaidi ya kuweka correlation ya Ruto na Hayati. Sasa nenda ukabishe huko na akili yako unayoita akili
.. Mie ndio nilichoambulia hapo. Usinichagulie tafsiri.
 
Ni mpuuzi na mpumbavu kama wewe ndio anayeweza kushindwa kuona anachotaka kuelewesha....ambacho hakuna. Zaidi ya kuweka correlation ya Ruto na Hayati. Sasa nenda ukabishe huko na akili yako unayoita akili
.. Mie ndio nilichoambulia hapo. Usinichagulie tafsiri.
Mzee hujaelewa narudia tena hujaelewa ingawa unataka kujifanya umeeelewa.
 
Aende mahakamani.
Nenda mahakamani
....haya wewe ndie unaejifanya umeelewa, umeelewa nini? manake sijaona umebandika lelote lenye kuonyesha huo uwerevu unaojipachika....Nieleweshe
Hebu kaa pemben kwanza muda wa remedial bado mzee.
 
Back
Top Bottom