Shamba la hekari mbili za mahindi lafyekwa, ni baada ya mkulima kurudia kosa alilofanya mwaka jana

Rare Sapphire

JF-Expert Member
Jul 24, 2021
576
1,626
1702738691924.png

Kufuatia shamba la mahindi zaidi ya hekari mbili kufyekwa wilayani Mpanda Mkoa wa Katavi, Mkuu wa wilaya hiyo, Jamila Yusuph amesema mahindi hayo yalipandwa kinyume cha sheria.

Amesema kulingana na sheria ndogo za manispaa hiyo, hakuna mwananchi anayeruhusiwa kupanda mazao yanayovuka urefu wa goti katikati ya mji kwani ni kuhatarisha usalama wa raia na mali zao.

Licha ya sheria kukataza hivyo, mkulima ambaye mahindi yake yamefyekwa, amerudia kosa alilotenda mwaka jana na kusamehewa, huku akitakiwa kulipa faini lakini mwaka huu tena amerudia kosa hilo.

Mwananchi
 

Kufuatia shamba la mahindi zaidi ya hekari mbili kufyekwa wilayani Mpanda Mkoa wa Katavi, Mkuu wa wilaya hiyo, Jamila Yusuph amesema mahindi hayo yalipandwa kinyume cha sheria.

Amesema kulingana na sheria ndogo za manispaa hiyo, hakuna mwananchi anayeruhusiwa kupanda mazao yanayovuka urefu wa goti katikati ya mji kwani ni kuhatarisha usalama wa raia na mali zao.

Licha ya sheria kukataza hivyo, mkulima ambaye mahindi yake yamefyekwa, amerudia kosa alilotenda mwaka jana na kusamehewa, huku akitakiwa kulipa faini lakini mwaka huu tena amerudia kosa hilo.

Mwananchi
Mbona kunavyoonekana ni shambani?
 
Kuliko kuyafyeka hayo mahindi! Wangerejea kanuni za usalama!
Kama mahindi hayo yanatishia usalama, wangeweka migambo eneo hilo walinde hadi yaive then wayataifishe kama sehemu ya fidia ya gharama za ulinzi ambao umetumika kuongeza ulinzi eneo hilo hatarishi!

Mkulima angeelewa somo vizuri maana yangekuwa chini ya serikali, halafu .wangemsweka ndani hadi pale mahindi yatapoiva ndo wanamwachia!
Hii ingepeleka meseji nzur sana kuliko kuyafyeka kama bangi!
Kufyeka chakula ni laana! Wamekosea sana kufyeka!
 
Ndio shida ya maviongozi yasiyo na akili, yasiyo na maono.

Wangeweza adhabu yenye kumuumiza na kufaidisha wengine.
Wangeweza kuacha yakuwe, wavune wao, watie kwemye ghala la taifa, ama wauze wafanyie jambo la kiserikali, mfano kujenga darasa ama kununua madawati etc.
Ama wangevuna na kupeleka kwa watoto yatima wa wilaya husika.
 
Back
Top Bottom