Shairi ya Harusi

eRRy

JF-Expert Member
Jun 12, 2009
1,125
204
Wapendwa JF! Asalam Aleykum... Bwana Asifiwe!Kuna Rafiki yangu anafunga pingu za Maisha mwezi huu wa sita. Anahitaji shairi! Nisaidieni kwa hilo plz!:help:
 
ulimkubalia nini wakati uliona ww huwezi kumtungia?? ni vema umwambie mapema kuwa umeshindwa!!
 
Nafumbua macho yangu, kukuangaza Kipenzi
Waridi la moyo wangu, daima nitakuenzi
asante kwa kuja kwangu, na kunipa lako penzi
KARIBU mpenzi Wangu.Karibu moyoni mwangu

Ni moyo wa namna gani, shujaa alokuwa nao
Ule usiotamani, kupendwa na wapendao
Mgumu Kiasi gani?, Usivutwe na Sumaku
Nguvu Ilo Mapenzini, aijua hata Kuku
SEMBUSE MIMI KABWELA, MTOTO WA KITANZANIA?.

Uzuri wako Kipenzi, Mithili ya mbalamwezi
Kwako nimeshikwa ganzi, kwa hakika sijiwezi
Kwangu ondoa Simanzi, usihofu laazizi.
Karibu Mpenzi wangu, Karibu Moyoni Mwangu

Tumuombe Mwenyezi Mungu, ndoa atie baraka
Atwondoshee Ukungu, Atujalie fanaka
Niwe wako uwe wangu, siku zote kwa hakika!
Karibu Mpenzi wangu, Karibu Moyoni Mwangu


Mpenzi niko tayari, KWANI SABABU NINAYO!
Mpenzi Sitahayari, KWANI NIA NINAYO!
Na Tuianze Safari, KWANI UWEZO NINAO!
Karibu Mpenzi wangu, Karibu Moyoni Mwangu


Hilo Shairi ukilitumia Ukipata Mijihela yoyote huko ya Kutuzwa , Ukipenda Unikumbuke Mwanao. hahahah!
 
ulimkubalia nini wakati uliona ww huwezi kumtungia?? ni vema umwambie mapema kuwa umeshindwa!!

AAh Susy! Mi nilimkubalia Kujitahidi Kuitafuta. Sikumpa Uhakika!
 
Nafumbua macho yangu, kukuangaza Kipenzi
Waridi la moyo wangu, daima nitakuenzi
asante kwa kuja kwangu, na kunipa lako penzi
KARIBU mpenzi Wangu.Karibu moyoni mwangu

Ni moyo wa namna gani, shujaa alokuwa nao
Ule usiotamani, kupendwa na wapendao
Mgumu Kiasi gani?, Usivutwe na Sumaku
Nguvu Ilo Mapenzini, aijua hata Kuku
SEMBUSE MIMI KABWELA, MTOTO WA KITANZANIA?.

Uzuri wako Kipenzi, Mithili ya mbalamwezi
Kwako nimeshikwa ganzi, kwa hakika sijiwezi
Kwangu ondoa Simanzi, usihofu laazizi.
Karibu Mpenzi wangu, Karibu Moyoni Mwangu

Tumuombe Mwenyezi Mungu, ndoa atie baraka
Atwondoshee Ukungu, Atujalie fanaka
Niwe wako uwe wangu, siku zote kwa hakika!
Karibu Mpenzi wangu, Karibu Moyoni Mwangu


Mpenzi niko tayari, KWANI SABABU NINAYO!
Mpenzi Sitahayari, KWANI NIA NINAYO!
Na Tuianze Safari, KWANI UWEZO NINAO!
Karibu Mpenzi wangu, Karibu Moyoni Mwangu


Hilo Shairi ukilitumia Ukipata Mijihela yoyote huko ya Kutuzwa , Ukipenda Unikumbuke Mwanao. hahahah!
Limetulia sana litawasaidia na wengineo watakaotaka shairi
 
mwambie kuwa hapa ndo kesha fika shairi tu atalipata aonane nami kwani anakiasi gani cha malipo ya hilo shairi?



kingine mwambie kuwa mm ni mama shughuli yaani MC kwenye sherehe mbalimbali na vileviile natengeneza keki na kadi za harusi asinikose kwenye hizo huduma pls usisahau mkuu
Wapendwa JF! Asalam Aleykum... Bwana Asifiwe!Kuna Rafiki yangu anafunga pingu za Maisha mwezi huu wa sita. Anahitaji shairi! Nisaidieni kwa hilo plz!:help:
 
[h=3]shairi la harusi[/h]
1.
Msigeuze harusi, zikawa ni kivumbasi,
Isirafu damisi, kwa shehe na makasisi,
Mjukuu Ibilisi, kisirani na nuksi,
Harusi kama hadithi, huishia muflisi.
2.
Ndoa ibada halisi, walisema waasisi,
Jambo lataka kiasi, si kushibisha nafusi,
Haliafiki Qudusi, mwingi wa kutanafusi,
Harusi kama hadithi, huishia muflisi.
3.
Nikahi ni fahirisi, utangulizi hukisi,
Lakudumu majilisi, pasiwe na wasiwasi,
Kaskazi au kusi, vyote kupata nemsi,
Harusi kama hadithi, huishia muflisi.
4.
Ikifanywa kwayo kasi, ya riha na anisi,
Hutia doa jeusi, katika moyo mkwasi,
Na kuleta uyabisi, kila kiungo kuhisi,
Harusi kama hadithi, huishia muflisi.
5.
Harusi kama libasi, wawili ni mahsusi,
Huleta hawa fususi, ya woto na utesi,
Hawapendwi maharusi, kipendwancho ni harusi,
Harusi kama hadithi, huishia muflisi.
6.
Hili lataka kiasi, hakika si wasiwasi,
Isirafu si nemsi, muulize Abunuwasi,
Na vitabu kadurusi, uone yake nakisi,
Harusi kama hadithi, huishia muflisi.
7.
Harusi si kiharusi, jasho na wingi kamasi,
Lataka bora ususi, mambo yenu kuasisi,
Yasiyoleta nuksi, balaa nayo mikosi,
Harusi kama hadithi, huishia muflisi.
8.
Harusi kitu halisi, hakichanganywi najisi,
Haumo kwenye kamusi, uchafu nao utesi,
Vinginevyo wasiwasi, na mgeni Ibilisi,
Harusi kama hadithi, huishia muflisi.
9.
Haitaki kandarasi, kuufanya uhandisi,
Huumeza ubinafsi, jumuiya kuasisi,
Ikawa yenye wepesi, umoja na urahisi,
Harusi kama hadithi, huishia muflisi.
10.
Humkataa chunusi, anayezusha mikosi,
Huyakimbia maasi, kwa mbio zake farasi,
Ili kutunza asasi, na kumkana ibilisi,
Harusi kama hadithi, huishia muflisi.
11.
Huchongwa moja libasi, ya kukaa maharusi,
Hawa zikatanafusi, huba ikawa msosi,
Pendo kuwa ni hadithi, simulizi kila mosi,
Harusi kama hadithi, huishia muflisi.
12.
Ila ikiwa najisi, haitokwisha mikosi,
Yatazidi na maasi, kusambaratika nafusi,
Ndoa ikawa nuksi, na familia kuhasi,
Harusi kama hadithi, huishia muflisi.
 
Back
Top Bottom