GLN. ulikuwa umejiandaa nini?
naomba unitungie la talaka
Limetulia sana litawasaidia na wengineo watakaotaka shairiNafumbua macho yangu, kukuangaza Kipenzi
Waridi la moyo wangu, daima nitakuenzi
asante kwa kuja kwangu, na kunipa lako penzi
KARIBU mpenzi Wangu.Karibu moyoni mwangu
Ni moyo wa namna gani, shujaa alokuwa nao
Ule usiotamani, kupendwa na wapendao
Mgumu Kiasi gani?, Usivutwe na Sumaku
Nguvu Ilo Mapenzini, aijua hata Kuku
SEMBUSE MIMI KABWELA, MTOTO WA KITANZANIA?.
Uzuri wako Kipenzi, Mithili ya mbalamwezi
Kwako nimeshikwa ganzi, kwa hakika sijiwezi
Kwangu ondoa Simanzi, usihofu laazizi.
Karibu Mpenzi wangu, Karibu Moyoni Mwangu
Tumuombe Mwenyezi Mungu, ndoa atie baraka
Atwondoshee Ukungu, Atujalie fanaka
Niwe wako uwe wangu, siku zote kwa hakika!
Karibu Mpenzi wangu, Karibu Moyoni Mwangu
Mpenzi niko tayari, KWANI SABABU NINAYO!
Mpenzi Sitahayari, KWANI NIA NINAYO!
Na Tuianze Safari, KWANI UWEZO NINAO!
Karibu Mpenzi wangu, Karibu Moyoni Mwangu
Hilo Shairi ukilitumia Ukipata Mijihela yoyote huko ya Kutuzwa , Ukipenda Unikumbuke Mwanao. hahahah!
Wapendwa JF! Asalam Aleykum... Bwana Asifiwe!Kuna Rafiki yangu anafunga pingu za Maisha mwezi huu wa sita. Anahitaji shairi! Nisaidieni kwa hilo plz!:help:
GLN. ulikuwa umejiandaa nini?
naomba unitungie la talaka