Shahada ya elimu kufanya Kazi benki

Shahada ya elimu kufanya Kazi benki

Ziltan

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2011
Posts
2,735
Reaction score
7,010
Heshima mbele wakuu,
mimi ni mwl miaka 8 kazin,nna shahada ya elimu baada ya kujiendeleza toka certificate grade A,nna jamaangu kaahidi kunisaidia kupata nafasi ya kazi benki,
nnaomba msada wa mawazo je niende huko kwa kutegemea kupata unafuu wa maisha na future nzuri ya kazi au ni yaleyale kwa kuzingatia kuwa kule mi sio taaluma yangu hivyo ntafanyishwa kazi za kawaida siku zote,
msaada tafadhali,
 
Endelea na kazi yako miaka uliyokaa kazni inakuruhusu bank ni utumwa huwi free kama ulivyo ila ungekuwa ndio unaenda kuanza kazi ya ualim nngekushauri uende bank ila kwa apo sikuungi mkono
 
Muulize atakutafutia kazi gani afu ujue na maslahi yake kisha linganisha na uliko then fanya uamuzi
 
Angalia maslahi ya sasa na baadaye...utulie kisha ufanye maamuzi sahihi..nakutakia kila heri.
 
Endelea na kazi yako miaka uliyokaa kazni inakuruhusu bank ni utumwa huwi free kama ulivyo ila ungekuwa ndio unaenda kuanza kazi ya ualim nngekushauri uende bank ila kwa apo sikuungi mkono

Huu u free unaosemwa ni wa nini haswa ? Wa bongo sisi wavivu sana ndio maana tunaongelea u free, mi nakubaliana na mtu ambaye anaongolea u free kama anaanza kujaribu kujiajiri kwa sababu ukitaka kujiajiri you need to have a network, na kujenga network ni ngumu sana kwa hiyo ni vizuri kujenga hiyo network ukiwa kwenye ajira so km unahitaji upate muda kwa ajili ya self business that's gud lakini km hauna issue u free is useless
 
Usione fahari kuambiwa unafanya kazi benki wakati maslahi ni finyu.
Jaribu kutafiti kipato unachokipata kwenye kazi ya ualimu na huko benki wapi maslahi yake ni mazuri na baada ya hapo ndio ufanye uamuzi sahihi.
 
using'ang'anie kitu ambacho hakina maslahi kwako, umeanza vizuri tangu grade A to shahada, una malengo mazuri na unahitaji kufanikiwa kwa kile unachokifanya, sasa cha kufanya angalia maslahi ya ualimu na yale ya bank wapi kunalipa kama ni bank beba virago kimbilia mama /baba usilaze damu, hata ukiwa bank teller na unapata kilicho sawa usijali fanya, kule bank hakuna cha ualimu, wala nini nafasi za bank ni multpurpose kila msomi wa shahada anaweza fanya ni kuelekezwa tu,.mbona mimi ni sociologist lakini field yangu nilifanyia NMB tena loan department, all the best!
 
using'ang'anie kitu ambacho hakina maslahi kwako, umeanza vizuri tangu grade A to shahada, una malengo mazuri na unahitaji kufanikiwa kwa kile unachokifanya, sasa cha kufanya angalia maslahi ya ualimu na yale ya bank wapi kunalipa kama ni bank beba virago kimbilia mama /baba usilaze damu, hata ukiwa bank teller na unapata kilicho sawa usijali fanya, kule bank hakuna cha ualimu, wala nini nafasi za bank ni multpurpose kila msomi wa shahada anaweza fanya ni kuelekezwa tu,.mbona mimi ni sociologist lakini field yangu nilifanyia NMB tena loan department, all the best!

nashukuru mkuu,
 
bank teller

Jiendeleze kwenye ualimu. Bank teller haitakuwa kazi ya uhakika kwako, kwenye kupunguza wafanyakazi wewe utakuwa wa kwanza kupunguzwa kwani hauna taaluma yeyote ya ki-bank. Ualimu ni kazi stable ingawa kwa sasa haina malipo mazuri lakini kwa miaka michache ijayo mambo yanaweza kubadilika.
 
Yaani hujajua kuwa unaingizwa mjini au kuvikwa mkenge siyo? Mwanangu Ziltan piga chaki au ushauri achana na mambo ya Benki vinginevyo kama una jina kama vile Kikwete Mkapa Lowassa Mwinyi, Mungai, Luhanjo, Sumaye, Msekwa, Makamba, Karume, Kigoda na mengine mengi ya hovyo.
 
Jiendeleze kwenye ualimu. Bank teller haitakuwa kazi ya uhakika kwako, kwenye kupunguza wafanyakazi wewe utakuwa wa kwanza kupunguzwa kwani hauna taaluma yeyote ya ki-bank. Ualimu ni kazi stable ingawa kwa sasa haina malipo mazuri lakini kwa miaka michache ijayo mambo yanaweza kubadilika.

kujiendeleza kwa sasa naona sio inshu sana, maake utaparangana wee hadi labda unapata masters then unarudi kukaa tu bila kuwa na inshu yoyote zaid ya kuendelea kupiga chaki,system inaangalia inamjua nani na sio una vyeti gan
 
kasome kwanza iue hiyo education piga master ya kitu kingine dizain ualimu wenyewe ushauchoka but ndio kazi ambayo unaweza kujiendeleza kimasomo kiurahisi. nenda huko benk uone kama watakuruhusu ukasome
 
Mi mwl mwenzio nimemaliza last year degree sijawahi waza kwenda bank labda kwingine niko kazini mwaka wa 7 soo umenizidi kidogo badilisha tu muundo wa utumishi uanze kuvuta pay na kama ulishafika d1 bac itakufaa hapo baadae taaluma yako ila bank ndugu yangu sikushauri banktellers hawana mishahara mikubwa kiivyo. Twende tukafundishe mwl

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
Mi mwl mwenzio nimemaliza last year degree sijawahi waza kwenda bank labda kwingine niko kazini mwaka wa 7 soo umenizidi kidogo badilisha tu muundo wa utumishi uanze kuvuta pay na kama ulishafika d1 bac itakufaa hapo baadae taaluma yako ila bank ndugu yangu sikushauri banktellers hawana mishahara mikubwa kiivyo. Twende tukafundishe mwl

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums

ualimu ni umaskini,hakika ninajionea sasa,
 
Heshima mbele wakuu,
mimi ni mwl miaka 8 kazin,nna shahada ya elimu baada ya kujiendeleza toka certificate grade A,nna jamaangu kaahidi kunisaidia kupata nafasi ya kazi benki,
nnaomba msada wa mawazo je niende huko kwa kutegemea kupata unafuu wa maisha na future nzuri ya kazi au ni yaleyale kwa kuzingatia kuwa kule mi sio taaluma yangu hivyo ntafanyishwa kazi za kawaida siku zote,
msaada tafadhali,

umeahidiwa kazi gani huko bank, hilo ndiyo muhimu maana inawezekana anataka kukubeba japo sio kazi yako
 
Omba likizo isiyo na malipo kwenye ualimu. Kisha nenda benki. Ukiona unamudu basi endelea huko huko na ukiona hakufai unarudi kwenye chaki.
 
Back
Top Bottom