Blaki Womani
JF-Expert Member
- Feb 28, 2011
- 11,228
- 13,449
Hili la tetemeko linatatiza sanaHuu ni uongo wa hali ya juu. Uingereza pekee yake imetoa shilingi 6.7 billion kusaidia wahanga wa tetemeko la ardhi iweje Serikali iseme zimekusanywa bilioni 5 tu!? List ya wachangiaji wote na kiasi walichochanga iwekwe hadharani mara moja ili kama kuna wizi umefanywa katika pesa hizi basi hao wezi wanaanikwe hadharani kwa kuiba pesa za wahanga wa tetemeko.
Kuna tetesi kwamba zinatarajiwa kujenga nyumba za watumishi makao mapya Dodoma .Huu ni uongo wa hali ya juu. Uingereza pekee yake imetoa shilingi 6.7 billion kusaidia wahanga wa tetemeko la ardhi iweje Serikali iseme zimekusanywa bilioni 5 tu!? List ya wachangiaji wote na kiasi walichochanga iwekwe hadharani mara moja ili kama kuna wizi umefanywa katika pesa hizi basi hao wezi wanaanikwe hadharani kwa kuiba pesa za wahanga wa tetemeko.
Hawana aibu wanasubiri tuzo za Forbes.ni Aibu
OVA
Mkuu BAK huu ni uchochezi na kumbuka mkuu hajaribiwi
Walishaaambiwa wajitetemekee na wajenge nyumba zao wenyewe
Usimchokoze mkuu
Mkuu BAK huu ni uchochezi na kumbuka mkuu hajaribiwi
Walishaaambiwa wajitetemekee na wajenge nyumba zao wenyewe
Usimchokoze mkuu
Mkuu Mr Rocky ahsante sana Mkuu. Hawa jamaa kwa kutotaka maovu yao yaanikwe hadharani wakaamua kulishusha hadhi neno "uchochezi" hivyo kila anayeanika uovu wao hadharani basi "huwachonganisha wananchi na Serikali" yao. Hata CAG naye ni mchochezi siku awamu hii maana kaanika hadharani ukwapuzi wa nyumba za Serikali, uongo Bungeni wa upotevu wa mabilioni ya pesa wizara ya ujenzi na pia ununuzi wa boti la MV ufisadi. Anavutiwa pumzi tu ili atimuliwe na nafasi yake apewe kikaragosi mwingine ambaye hataweza kuanika uovu wowote ndani ya Serikali ili kulinda ajira yake. Tembo hawatufai Mkuu. Salam zangu nyingi kwa familia yote Mkuu.
Kenya, uganda, uingereza, wafanya biashara, taasis na wananchi michango yao ni tsh4.7bln? Kuna walakin hapoPesa iliyochangwa ni bilion 16 mpaka sasa......
Hizo zingine ni polojo tu............
Za watu wasimuogopa mungu.....
Nashukuru sana mkuu Bak byzo I.T Tunaogopa sana kucomment kwenye maeneo kama haya maana hatuna mil 7 za kwenda kujilipia faini na ushaona kule bungeni wanalalamika hata hiyo faini wanasema ni ndogo hivyo kesi kama hiyo unaweza ukajikuta unadaiwa mil mia
Yuende hivyo hivyo mkuu tutafika na tutaona tunaelekea wapi
Asante kwa salam na wewe salam kwa familia
![]()
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameongea na Mabalozi na Wawakilishi wa wafanyabishara Ikulu jijini Dar es Salaam kutoa taarifa ya tatemeko la ardhi na maafa yaliyotokea tarehe 10 Septemba 2016.
Waziri Majaliwa amewaomba wawakilishi hao kutoa misaada mbalimbali ili kuungana na Serikali kuwasaidia walioathirika mkoani Kagera.
Shilingi 1.4 bilioni zimekusanywa katika harambee iliyoandaliwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ili kusaidia wananchi waliopata maafa ya tetemeko la ardhi mkoani Kagera Jumamosi iliyopita.
Kiasi hicho ni fedha taslimu na ahadi zimetolewa na wafanyabiashara na mabalozi wanaoziwakilisha nchi mbalimbali nchini.
Baadhi ya Taasisi na Balozi zilizo ahidi kutoa michango ni:-
= TBL Wamechangia Milioni 100
= Azania Group Wanatanguliza Milioni 20
= Wafanyabiashara wa Mafuta wa rejareja watakusanya Milioni 250 na watakabidhi ijumaa ya week hii
= Kagera Sugar wanatoa Milioni 100 na tani 10 za sukari.
= Serengeti wanatoa saruji mifuko 800
= Pepsi Cola 50 Millioni
= Hatiamaye Regnald Mengi anatoa mchango wake wa Milioni 110.
= Protas Ishengoma anatoa msaada wa Milioni 5.
= GBP, MOIL na OILCOM wameahidi kujenga shule mbili (Ihungo na Nyakato) zilizoharibiwa vibaya.
= Puma wanachangia 50 Milioni
= Agusta Tanzania wanatoa Milioni 10
= Camel Oil wanachangia mifuko 1,000 ya Cement
= Tippa waachangia milioni 20
= Orexy wanachangia Milioni 50
= Waislamu wa madhehebu ya Al-Shafy, Ijumaa na Adhuhuri wanachangia Milioni 1.
= Sahara Tanzania wanachangia Milioni 20
Wizara ya Mambo ya Nje watafanya matembezi ili kuhamashisha uchangishaji wa fedha na wataanzia Polisi Oysterbay.
MAJUMUISHO:
Waziri Charles Mwijage nafanya majumuisho ya fedha zilizopatikana ni kama ifuatavyo:
1. Fedha taslimu ni Milioni 646,
2. Ahadi ni Milioni 705,
3. Dola za Kimarekani 10,000
4. Yuro 10,000.
5. Mfuko ya Sementi zaidi ya 2800,
6. Ahadi ya ujenzi wa Shule mbili ndani ya siku 30.
JUMLA KUU, Bilioni 1 na Na Zaidi ya Milioni 300
======


Dikteta kumbe ni tapeli na mpenda dhuruma.Pesa za waathirika kazichimbia ale mke wake.
Laana itawatafuna maisha.yao yoteHahahahha kabla ya kufahamu ni kiasi gani kimechangwa at least watuambie hizo ambazo wanasema wanazo watueleze zimefanya kazi gani so far...., then ndio tuje kwenye kutajiana majina na amount. Hii serikali ya CCM sijui hii laana ya wizi nani kawaachia. sijui kwa kweli