benzemah
JF-Expert Member
- Nov 19, 2014
- 1,504
- 3,034
Ujenzi wa reli ya kisasa (SGR) kipande cha tano kutoka Isaka mkoani Shinyanga hadi Mkoa wa Mwanza urefu wa kilometa 341 ukijumuisha njia kuu na njia ya kupishana kwenye stesheni unazidi kushika kasi na hadi sasa mradi huo umefikia asilimia 44.25.
Meneja mradi kipande cha tano cha SGR, Christopher Kalisti alisema wakati wa ziara ya kikazi ya siku moja ya Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa.
Alisema kuwa kazi kubwa ya msingi katika mradi huo ni ujenzi wa tuta na kuwa hadi sasa ujenzi umefikia asilimia 80 wakati mifumo mingine inayofuata juu ya tuta ikiendelea vizuri ikiwemo kutandika reli na kazi hiyo ime-fanywa kwa kilometa 24. Kalisti alisema kuwa wanaendelea kusimika nguzo kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya umeme pamoja na kupanda majani kwa ajili ya ulinzi wa matuta.
"Ujenzi wa madaraja kiujumla unaendelea vizuri, tuna mada-raja zaidi ya 600 yanayojumuisha madaraja kwa ajili ya kupitisha mifumo ya umeme, kupitisha mawasiliano, kupitisha wanyama, kupitisha binadamu, kupitisha magari, kupitisha treni ya zamani kiujumla inaendelea vizuri na tumefikia zaidi ya asilimia 60;" alisema.
Naye Waziri wa Uchukuzi, Profesa Mbarawa alisema kuwa ameridhishwa na maendeleo ya mradi huo na alitoa pongezi kwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kujitoa kwake kwa ajili ya kufanikisha ujenzi wa miradi mbalimbali ya kimkakati ikiwemo ujenzi wa reli ya kisasa (SGR).
Naye Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Christina Mdeme alisema kuwa kutokana na mkoa huo kupitiwa na mradi huo wa SGR kama mkoa wamejipanga kuzalisha zaidi kupitia sekta mbalimbali ikiwemo kilimo na mifugo.
Meneja mradi kipande cha tano cha SGR, Christopher Kalisti alisema wakati wa ziara ya kikazi ya siku moja ya Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa.
Alisema kuwa kazi kubwa ya msingi katika mradi huo ni ujenzi wa tuta na kuwa hadi sasa ujenzi umefikia asilimia 80 wakati mifumo mingine inayofuata juu ya tuta ikiendelea vizuri ikiwemo kutandika reli na kazi hiyo ime-fanywa kwa kilometa 24. Kalisti alisema kuwa wanaendelea kusimika nguzo kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya umeme pamoja na kupanda majani kwa ajili ya ulinzi wa matuta.
"Ujenzi wa madaraja kiujumla unaendelea vizuri, tuna mada-raja zaidi ya 600 yanayojumuisha madaraja kwa ajili ya kupitisha mifumo ya umeme, kupitisha mawasiliano, kupitisha wanyama, kupitisha binadamu, kupitisha magari, kupitisha treni ya zamani kiujumla inaendelea vizuri na tumefikia zaidi ya asilimia 60;" alisema.
Naye Waziri wa Uchukuzi, Profesa Mbarawa alisema kuwa ameridhishwa na maendeleo ya mradi huo na alitoa pongezi kwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kujitoa kwake kwa ajili ya kufanikisha ujenzi wa miradi mbalimbali ya kimkakati ikiwemo ujenzi wa reli ya kisasa (SGR).
Naye Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Christina Mdeme alisema kuwa kutokana na mkoa huo kupitiwa na mradi huo wa SGR kama mkoa wamejipanga kuzalisha zaidi kupitia sekta mbalimbali ikiwemo kilimo na mifugo.