Sex ni afya

mzambia

JF-Expert Member
Dec 31, 2010
885
60
SEX NI AFYA
Wengi huja na sababu lukuki linapokuja suala la kuwa mwili mmoja (kwenye ndoa) “mara kichwa kinauma” au “nimechoka sana leo” au “sijisikiii vizuri”lengo ni kukwepa SEX.

Hata hivyo tafiti nyingi zinaonesha kuwa kuna faida kubwa sana kupata huduma ya tendo la ndoa angalau mara mbili au tatu kwa wiki, kumbuka too much is harmful

FAIDA SEX KWA AFYA YA MWILI
Huimarisha immune system kwenye mwili.
Wanandoa ambao hushiriki angalau mara mbili kwa wiki walionesha kiwango kikubwa cha antibody zinazosaidia kupigana na magonjwa.

Huongeza umri wa kuishi.
Wanaume ambao walikuwa wanafika kileleni (orgasm) zaidi ya miaka 10 wali- boost uwezo wa kuishi miaka zaidi kuliko wale ambao walikuwa na hawafiki kileleni.

Hupunguza uwezokano wa kupata prostate cancer.
Wanaume ambao wali ejaculate zaidi ya miaka 35 walikuwa na asilimia 33 pungufu kupata prostate cancer.

Hupunguza cholesterol (mafuta)
Kutokana na zoezi la kufanya mapenzi (sex) ni zoezi tosha kuweza kupunguza cholesterol na kuondokana na kupata magonjwa ya moyo.

Huimarisha mzunguko wa damu mwilini
Tunapofanya mapenzi mapigo ya moyo huongezeka na mzunguko wa damu huwa na speed zaidi na damu huongezekana maradufu kwenye ubongo na sehemu zingine za mwili na matokeo ni mzunguko wa damu kuwa mzuri mwili mzima.

Huongeza uwezo wa kukua (growth)
Watafiti wengi wanakiri kwamba sex huongeza uwezekano wa mifupa kukua na kuimarisha repair ya tishu kwenye mwili.

Huimarisha uwezo wa kunusa
Baada ya sex, kuzalishwa kwa homoni ya prolactin huongezeka na huwezesha stem cells zilizopo kwenye ubongo kuzalisha neurons ambazo husaidia kunusa vizuri.

Hupunguza maumivu (pain relief)
Unapokaribia kufika kileleni kiwango cha homoni za oxytocin huongezeka mara tano zaidi kuliko kiwango cha kawaida, matokeo ni kutolewa kwa endorphins ambayo hupunguza maumivu ya kila kitu kuanzia kichwa, arthritis nk.

Huimarisha kibofu cha mkojo
Wakati wa sex unatumia muscles zile zile unatumia kukojoa (urine), kutumia mara kwa mara kwa hii misuli huwezesha kuwa na uwezo wa kuthibiti kibofu cha mkojo.

Huimarisha uke
Wanawake ambao huamua kutoshiriki sex wanakuwa na uwezekano wa kujisikia maumivu wakati wa SEX (vaginal atrophy) kwa kushiriki mara kwa mara uke huwa mwepesi kutoa lubricant na hakuna maumivu.
Hapa kuna kanuni “use it or lose it!

Husaidia healing ya vidonda
Baadhi ya evidence zinapendekeza kwamba sex huweza kusaidia vidonda kupona haraka, ushahidi ni kwamba homoni za oxytocinhusaidia vidonda kupona kwa regeneration ya seli mwilini na oxytocinhuzalisha pale ukishiriki sex.

Hupunguza uwezekano wa kupata cancer ya matiti.
Wanawake ambao hawajawahi kuzaa walionekana kuwa na uwezekano mkubwa wa kupata cancer ya matiti, hii ina maana kwamba kujihusisha na sex hupunguza kupata cancer ya matiti.

FAIDA YA SEX KWA AFYA YA AKILI

Hupunguza stress
Sex huweza kupunguza stress kwa kupunguza kiwango cha masumbuko (anxiety) na kuongeza relaxation na kusaidia kuwa na usingizi mzuri.

Hupambana na depression
Wanawake ambao walijihusisha na sex kwa kuwa contact na semen walikuwa less depressed kuliko wale wambao hawakufanya.

Hupambana na kuthibiti alama za kuzeeka
Sex hufanya mtu kuonekana kijana zaidi.
Katika utafiti mmoja watu ambao walishiriki sex zaidi ya mara 3 kwa wiki walionekana ni vijana zaidi ya miaka 10 pungufu ukilinganisha na wale ambao walikwepa sex.

Huimairsha kujisikia upo fit
Dakika 30 za kufanya mapenzi huweza kuchoma kiasi cha 150 calories.
Na mtu anayeshiriki sex kila mara 3 kwa wiki huweza kupunguza kilo 2.5 za uzito kwa mwaka. Pia sex huweza kunyumbua misuli na kupelekea mtu kuwa fit, pia hekaheka za milalo mbalimbali huweza kufanya contractions ya mapaja, mikono, mabega, shingo, tumbo, kifua, mgongo, ******, miguu, kiuno na pia sex huzalisha testosterone ambayo huimarisha mifupa na misuli.

Husaidia nywele kung’aa na ngozi kuwa imara
Sex huongeza kiwango cha estrogen ambayo husaidia nywele kung’aa na ngozi kuwa imara kwa mwanamke.

Husaidia meno kuwa imara
Mara nyingi kabla ya sex wahusika hujitahidi kusafisha meno (brushing) kwa njia hii una kuwa imeimarisha afya ya kinywa.
Pia wakati wa sex hasa maandalizi huhusisha kissing ambayo hufanya kazi nzuri kusafisha meno na fizi.
Seminal plasma zinazozalishwa huwa na zinc, calcium na madini mengine muhimu kwa afya ya meno.


FAIDA YA SEX KWA AFYA YA UZAZI
Husaidia kuwa na mzunguko mzuri za siku za mwanamke.
Wanawake ambao hujihusisha na sex angalau siku moja kwa wiki huwa na mzunguko wa siku uliosawa tofauti na wale ambao hutoa visingizio.

Huimarisha fertility
Kwa kuwa kushiriki sex hufanya mzunguko kuwa regular inakuwa rahisi mwanamke kushika mimba na kuzaa tofauti na mwanamke akiwa na mzunguko wa siku ambao ni irregular.

FAIDA KATIKA KIROHO
Watafiti wengi wanakiri kwamba kuna sexual energy kama energyzingine ambayo wakati wa sex ikiunganishwa kati ya mwanaume na mwanamke hasa wakati wa kufika kileleni huweza kuwaunganisha wawili in deepest part of of selves.
Na hii energy (non physical) huweza kuimarisha maeneo mengine ya maisha yetu, hutufanya kujisikia ni kitu kimoja na kuwa strongerzaidi katika nafsi na mahusiano kwa ujumla.
Hivyo matokeo ni kujisikia vizuri wewe mwenyewe, mwenzi wako na maisha kwa ujumla.

TAHADHARI:
Hii mada ni kwa ajili ya kupeana habari tu (ndiyo maana hakunareference links, ingawa unaweza mwenyewe ku- Google),
Jambo la msingi ni kwamba kuna umuhimu wa hali ya juu sana kuzingatia kwamba hapa tunazungumzia sex katika ndoa tu na si zaidi ya hapo.
Pia ni muhimu kuzingatia kwamba ili kushiriki sex ni muhimu kuangalia afya ya mwenzi wako, maadili na kutii sheria na amri za Mungu otherwise badala ya sex kukupa afya inaweza kukuua kimwili na kiroho.

FANYA SEX UONGEZE UPENDO DAIMA
 
yote mazuri ya mada yanaharibiwa na kipengele hicho cha "TAHADHARI" wengine hatujakidhi hicho kipengele cha "NDOA" sasa ndio tukose "AFYA"?
 
ngoja niiprint nikawasambazie watoto wa secondari/shule za kata muone kazi yake
 
Huwa sina kawaida ya kusoma thread ndefu ila hii nimeisoma yote imetulia sana mkuu big up.
 
Wale ambao hatuna ndoa, tutakuwa hatuna afya mpaka tupate ndoa au?
Hebu tusaidieni na sisi tupate hiyo afya, kama tunafanya kwa afya kwani kuna dhambi hapo?
Nauliza tu jamani. Sex kwa afya hata na mume wa mtu?? Si kwa afya?
Kwani vibaya kuupatia mwili afya?
 
Safi sana mkuu!! hivi ndo vitu ambavyo jamii yetu baadhi yetu inabidi tuvipate kila wakati ili kujimaarisha katika masuala ya afya na ndoa.
 
Vp mastabeshen??inaleta yote haya??coz wengine hatujaanza sex tunasubiri ndoa na umri unazidi kwenda
 
Kazi ipo kama Sex ni Afya basi hata asiye na mke au mume anafanya kwa afya.
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom