Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 57,103
- 128,723
Wanabodi,
Huu ni uzi wa swali kuhusu Serikali Yetu Kuitwa "Sinister" na "Authoritarian", Jee ni Kweli?. Kama Sii Kweli, inamaanisha ni uongo!, Tusikubali Uongo Huu!, Tuukanushe, maana uongo ukisemwa sana bila kukanushwa, mwisho wake hugeuka kuwa kweli!. Na uzalendo ni pamoja za kutokubali nchi yako isemwe vibaya kwa kuzushiwa uongo na media za nje, huku sisi wenyewe, tumenyamaza tuu!. Kunyamaza huku kutapelekea dunia kuamini yote yanayosemwa kuhusu Tanzania ni kweli.
Nakiri kupandisha uzi huu kutokana na bandiko la Mkuu Return Of Undertaker
Gazeti la Uingereza laimulika serikali ya Magufuli na kusema ...
Jarida la Africa Confidential toleo la 58, story number 20 lililochapishwa Oktoba 6, limesema hivi kuhusu Tanzania.
Vol 58 No 20
Published 6th October 2017
"Magufuli on the warpath
6TH OCTOBER 2017
An assassination attempt against an opposition leader raises suspicions about sinister government tactics
When 40 bullets were pumped into the car carrying Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) member of parliament Tundu Lissu outside his Dodoma home on 7 September, claims of the country's descent into authoritarianism suddenly became more credible".
Hawa jamaa wamesema serikali yetu ni "sinister" na pia inaendesha nchi kwa mtindo wa "authoritarianism"!. Haya sio maneno mazuri kwa serikali iliyoingia madarakani kwa ushindi halali katika sanduku la kura, kupitia uchaguzi ulioendeshwa na Tume huru ya Uchaguzi, hivyo uchaguzi ulikuwa ni huru na wa haki, hivyo matokeo ni halali, na nchi yetu inaendeshwa kwa kufuata misingi ya katiba, na kuheshimu utawala wa sheria.
Ikulu yetu, Waziri Mwakyembe na Idara yetu ya Habari, tusikalie kuyafungia tuu magazeti ya ndani kwa kutoa habari za kweli msiopendezwa nazo, huku tukikaa kimya wakati habari za uongo kuhusu nchi yetu zikienezwa na media za nje!, habari yoyote ambayo sii ya kweli, kuihusu Tanzania na rais wetu, ikitolewa, tusikae kimya, ikanushwe!, vinginevyo itaonekana ni kweli!.
Mbona Kikwete alipotuhumiwa kwa kitu kitu kidogo tuu, kuhongwa suti, Ikulu yetu ilikanusha, kwa nini hizi media za nje, zinaituhumu serikali yetu kwa mambo makubwa, na mabaya hivi, halafu serikali yetu imekaa kimya, imenyamaza?.
Hata kama serikali imenyamaza, lets say iko too bize na mambo muhimu zaidi kwa taifa, hivyo haina time na vituhuma hivi vya media za nje, jee wako wapi Watanzania walendo wa kweli wa kuitetea nchi yetu yetu inaposemwa vibaya?!.
Mimi naomba kujipambanua kuwa ni Mtanzania Mzalendo, na kwa mujibu wa fani yangu, kazi yangu na uwezo wangu ni kuandika tuu au kusema!, rais wetu alipotuhumiwa kuhongwa suti nilisema.
Tuhuma za Rais wetu kuhongwa suti: Marekani ituombe radhi ...
Hata kelele kuhusu udikikiteta wa Magufuli ziliposhika kasi nilisema
Udikiteta: Uongo Ukisemwa Sana na Kuachwa Bila Kukanushwa Hugeuka ...
Magufuli aliposemwa vibaya na SABC, nilisema
Serikali ikanushe uongo huu wa SABC kumsema vibaya Rais wetu ...
Magufuli aliposemwa vibaya kuhusu Mimba za utotoni, pia nilisema
Je, Huku Sio Kudhalilishwa Kwa Rais Wetu na Media za Nje?. Jee ...
Na sasa hapa serikali yetu inaposemwa vibaya, nimeandika na kushauri tusikubali, tusikae kimya, tukanushe unless kama yanayosemwa kuihusu serikali yetu ni kweli!.
Mungu ibariki Tanzania.
Jumapili Njema.
Paskali.
Huu ni uzi wa swali kuhusu Serikali Yetu Kuitwa "Sinister" na "Authoritarian", Jee ni Kweli?. Kama Sii Kweli, inamaanisha ni uongo!, Tusikubali Uongo Huu!, Tuukanushe, maana uongo ukisemwa sana bila kukanushwa, mwisho wake hugeuka kuwa kweli!. Na uzalendo ni pamoja za kutokubali nchi yako isemwe vibaya kwa kuzushiwa uongo na media za nje, huku sisi wenyewe, tumenyamaza tuu!. Kunyamaza huku kutapelekea dunia kuamini yote yanayosemwa kuhusu Tanzania ni kweli.
Nakiri kupandisha uzi huu kutokana na bandiko la Mkuu Return Of Undertaker
Gazeti la Uingereza laimulika serikali ya Magufuli na kusema ...
Jarida la Africa Confidential toleo la 58, story number 20 lililochapishwa Oktoba 6, limesema hivi kuhusu Tanzania.
Vol 58 No 20
Published 6th October 2017
"Magufuli on the warpath
6TH OCTOBER 2017
An assassination attempt against an opposition leader raises suspicions about sinister government tactics
When 40 bullets were pumped into the car carrying Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) member of parliament Tundu Lissu outside his Dodoma home on 7 September, claims of the country's descent into authoritarianism suddenly became more credible".
Hawa jamaa wamesema serikali yetu ni "sinister" na pia inaendesha nchi kwa mtindo wa "authoritarianism"!. Haya sio maneno mazuri kwa serikali iliyoingia madarakani kwa ushindi halali katika sanduku la kura, kupitia uchaguzi ulioendeshwa na Tume huru ya Uchaguzi, hivyo uchaguzi ulikuwa ni huru na wa haki, hivyo matokeo ni halali, na nchi yetu inaendeshwa kwa kufuata misingi ya katiba, na kuheshimu utawala wa sheria.
Ikulu yetu, Waziri Mwakyembe na Idara yetu ya Habari, tusikalie kuyafungia tuu magazeti ya ndani kwa kutoa habari za kweli msiopendezwa nazo, huku tukikaa kimya wakati habari za uongo kuhusu nchi yetu zikienezwa na media za nje!, habari yoyote ambayo sii ya kweli, kuihusu Tanzania na rais wetu, ikitolewa, tusikae kimya, ikanushwe!, vinginevyo itaonekana ni kweli!.
Mbona Kikwete alipotuhumiwa kwa kitu kitu kidogo tuu, kuhongwa suti, Ikulu yetu ilikanusha, kwa nini hizi media za nje, zinaituhumu serikali yetu kwa mambo makubwa, na mabaya hivi, halafu serikali yetu imekaa kimya, imenyamaza?.
Hata kama serikali imenyamaza, lets say iko too bize na mambo muhimu zaidi kwa taifa, hivyo haina time na vituhuma hivi vya media za nje, jee wako wapi Watanzania walendo wa kweli wa kuitetea nchi yetu yetu inaposemwa vibaya?!.
Mimi naomba kujipambanua kuwa ni Mtanzania Mzalendo, na kwa mujibu wa fani yangu, kazi yangu na uwezo wangu ni kuandika tuu au kusema!, rais wetu alipotuhumiwa kuhongwa suti nilisema.
Tuhuma za Rais wetu kuhongwa suti: Marekani ituombe radhi ...
Hata kelele kuhusu udikikiteta wa Magufuli ziliposhika kasi nilisema
Udikiteta: Uongo Ukisemwa Sana na Kuachwa Bila Kukanushwa Hugeuka ...
Magufuli aliposemwa vibaya na SABC, nilisema
Serikali ikanushe uongo huu wa SABC kumsema vibaya Rais wetu ...
Magufuli aliposemwa vibaya kuhusu Mimba za utotoni, pia nilisema
Je, Huku Sio Kudhalilishwa Kwa Rais Wetu na Media za Nje?. Jee ...
Na sasa hapa serikali yetu inaposemwa vibaya, nimeandika na kushauri tusikubali, tusikae kimya, tukanushe unless kama yanayosemwa kuihusu serikali yetu ni kweli!.
Mungu ibariki Tanzania.
Jumapili Njema.
Paskali.