Kurzweil
JF-Expert Member
- May 25, 2011
- 6,622
- 8,399
Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu kupitia ukurasa wake wa Twitter ameeleza yafuatayo kufuatia kifo cha Mwanafunzi kinachodaiwa kutokana na kipigo kutoka kwa Mwalimu
NUKUU:
Nimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha mtoto Sperius Eradius aliyekuwa darasa la 5 S/Msingi Kibeta, Bukoba ambapo kimehusishwa na adhabu ya kupigwa na Walimu wake. Ninatoa pole kwa wazazi/walezi, ndugu na marafiki wa marehemu.Mungu awape moyo wa ustahimilivu
Kufuatia wazazi wa mtoto kutokuwa na imani na uchunguzi uliofanywa na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Kagera, Wizara yangu imetuma mtaalamu bingwa wa uchunguzi (Pathologist) toka Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Bugando kwa ajili ya kwenda kufanya upya uchunguzi wa mwili wa marehemu
Tayari mtaalamu huyo ameshawasili Kagera leo asubuhi kwa ajili ya kuanza uchunguzi mpya. Ninatoa wito kwa familia, ndugu na wananchi kuwa watulivu ktk kipindi hiki ambapo uchunguzi wa kibingwa unaendelea. Tutahakikisha kuwa uchunguzi unafanyika kwa ufanisi ili haki itendeke
Aidha nitumie fursa hii kuwataka Wazazi/Walezi na Walimu kutambua wajibu mkubwa tulionao wa kuwafundisha na kuwalea watoto wetu kwa kuzingatia sheria na taratibu tulizojiwekea. Vitendo vya ukatili dhidi ya watoto havikubaliki katika jamii yetu na ni kinyume cha sheria za nchi
Kama jamii tunao wajibu wa kuhakikisha mtoto anaishi, kukua na kuendelezwa ktk mazingira salama na rafiki kwa mujibu wa Sheria ya Mtoto ya 2009.
NINALAANI VIKALI Vitendo vya Ukatili vinavyofanywa dhidi ya watoto ktk jamii. Tutawafuatilia na kuwachukulia hatua wanaohusika
NUKUU:
Nimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha mtoto Sperius Eradius aliyekuwa darasa la 5 S/Msingi Kibeta, Bukoba ambapo kimehusishwa na adhabu ya kupigwa na Walimu wake. Ninatoa pole kwa wazazi/walezi, ndugu na marafiki wa marehemu.Mungu awape moyo wa ustahimilivu
Kufuatia wazazi wa mtoto kutokuwa na imani na uchunguzi uliofanywa na Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Kagera, Wizara yangu imetuma mtaalamu bingwa wa uchunguzi (Pathologist) toka Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Bugando kwa ajili ya kwenda kufanya upya uchunguzi wa mwili wa marehemu
Tayari mtaalamu huyo ameshawasili Kagera leo asubuhi kwa ajili ya kuanza uchunguzi mpya. Ninatoa wito kwa familia, ndugu na wananchi kuwa watulivu ktk kipindi hiki ambapo uchunguzi wa kibingwa unaendelea. Tutahakikisha kuwa uchunguzi unafanyika kwa ufanisi ili haki itendeke
Aidha nitumie fursa hii kuwataka Wazazi/Walezi na Walimu kutambua wajibu mkubwa tulionao wa kuwafundisha na kuwalea watoto wetu kwa kuzingatia sheria na taratibu tulizojiwekea. Vitendo vya ukatili dhidi ya watoto havikubaliki katika jamii yetu na ni kinyume cha sheria za nchi
Kama jamii tunao wajibu wa kuhakikisha mtoto anaishi, kukua na kuendelezwa ktk mazingira salama na rafiki kwa mujibu wa Sheria ya Mtoto ya 2009.
NINALAANI VIKALI Vitendo vya Ukatili vinavyofanywa dhidi ya watoto ktk jamii. Tutawafuatilia na kuwachukulia hatua wanaohusika