Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,316
- 33,111
Mhariri Mtendaji wa gazeti la MwanaHalisi, Saed Kubenea
Serikali imeshauriwa kukutana na viongozi wa kampuni ya Hali Halisi ili kujadili namna ya kulifungulia gazeti la Mwanahalisi kutokana na Dk. Steven Ulimboka kuweka wazi ofisa usalama wa taifa anayedaiwa kuhusika na kutekwa kwake.
Alisema sababu walizotumia viongozi wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kulifungia gazeti la hilo sio za kweli akidai kilichoandikwa na gazeti hilo kilikuwa ni ukweli ambao umethibitishwa na Dk. Ulimboka.
Dk. Ulimboka kupitia wakili wake aliweka wazi kwamba Ofisa wa Usalama wa Taifa alihusika katika kutekwa kwake na kwamba ofisa huyo ni mdau mkubwa wa tukio hilo tunasikitika kwamba hadi leo jeshi la polisi na serikali hawajachukua hatua yoyote ya kisheria kwa ofisa huyo na washirika wake alisema Albani.
Alisema wadau mbalimbali walitegemea kusikia serikali inatoa tamko kwamba imepata uhakika kuhusu ofisa wake kukiuka maadili ya ajira yake na ingetangaza inachukua hatua gani za kisheria dhidi yake kwa kuhusika katika makosa ya jinai.
:: IPPMEDIA
CHANZO: NIPASHE
''Mheshimiwa Mkuu wa nchi Rais wetu J.K. Hebu liachie hili gazete wasamehe wahusika kwa heshima yako mkuu Rais wetu Mtukufu''.Mzizimkavu